TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Wednesday, February 11, 2015

MBUNGE WA MOROGORO MJINI AWASHANGAZA WAKAZI WA MOROGORO

Mbunge wa Jimbo la Morogoro Mjini Mh Aziz Abood akisalimiana na wakazi wa Mitaa ya  Kata ya Kichangani manipaa ya Morogoro Katika Mfurulizo wa Ziara zake anazofanya katika kata Zote za Jimbi hilo kwa lengo la Kusikiliza Kero za wananchi wa Jimbo hilo .Katika Hali isiyo ya kawaida Mh Abood Amewashangaza wakazi wa Kata ya Kichangani Pale alipokataa Kuitwa  Mheshimiwa ,Mbunge huyo aliwataka wakazi hao Kumwita Mtumishi.Akilezea Zaidi Mh Abood alisema Namnukuu “Jina Mheshimiwa  Ninaitwa tu nikiwa Bungeni Lakini Nikija Kwenu Msiniite Mheshimiwa bali Mniite Mtumishi Wetu Amekuja” Wakazi hao walishangazwa na hali hiyo na kuishia kusema Tangu Uhuru Katika Wabunge wote waliowahi kuliongoza Jimbo Hilo Hakujawahi Kutokea Mbunge Kama Huyu Maana anawajali ,anawasikiliza na Ameshatatua kero Kubwa zilizokuwa zinawakabili kama Maji,Zahanati,Barabara pamoja na kuwasomesha Watoto wengi Yatima na watoto ambao wazazi wao wana maisha Duni.
Mbunge wa Jimbo la Morogoro Mjini Mh Aziz Abood Akiwa Amezungukwa na wakazi wa Mitaa ya Area Six A na B Kata ya Kichangani alipofika kuwasikiliza kuhusu Kero Mbalimbali zinazowakabili wakazi wa Kata hiyo.Wakazi hao walimweleza Mh Abood  kuwa Wanakabiliwa na Kero Kubwa ya Umeme,Maji na Barabara za Mitaa.Kuhusu Maji Mh. Abood Aliwajibu Anapambana Usiku na Mchana kutatua Kero hiyo kwa Kushirikiana na Idara ya Maji mkoa wa Morogoro. Kwa Juhudi zake Mwenyewe Ameshachimba visima Karibu Kila Kata Vyenye thamani ya Karibu shilingi  Milioni 550.Na Bado anaendelea Kutumia Kila Mbinu kuhakikisha wakazi hao wanapata Maji safi na salama. Alitoa Shilingi Milion 1 kwajili  ya Kununua Mafuta Kuwasha Mitambo ya Kuchonga Barabara za Mitaa hiyo. 
Mbunge wa Jimbo la Morogoro Mjini Mh. Aziz Abood akiongea na Mtoto Mdogo wakti wa Ziara yake aliyoifanya kata ya Kichanagani
Mbunge wa Jimbo la Morogoro Mjini Mh Aziz Abood akishiriki kukaanga Samaki 
Mbunge wa Jimbo la Morogoro Mjini Mh Aziz Abood akiwa Meza Kuu na wenyeviti wa Mitaa ya Koal A na B Kata ya Kichangani waliojitokeza Kwenye ziara hiyo Ambapo walipewa nafasi ya Kuwasalimia wananchi  na kuishia Kumsifia Mbunge huyo kwa Kumwita Ni jembe Lililo Makini na Kuwaasa wakazi wa Jimbo hilo Kuunga Mkono katika Shuguli zake Pia walimuahidi Mh Abood Kushirikiana nae bega kwa bega katika Kuwaletea wakazi wa Morogoro Maendeleo.
 

No comments:

Post a Comment