TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Thursday, December 31, 2015

MSANII TEKNO MILES KUNOGESHA TAMASHA LA JOHNNIE WALKER “GROWN & SEXY THE GOLD FINALE”




Akizungumza wakati wa mkutano na waandishi wa habari, uliofanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es salaam,Meneja chapa wa pombe kali SBL Shomari Shija alisema, “Tumeamua kulidhamini Tamasha hili kama njia mojawapo ya kujumuika na kufurahi kwa pamoja na wateja wetu wa chapa za Johnnie Walker katika kuuaga rasmi mwaka huu wa 2015.

Bw. Shija aliongeza kuwa katika Tamasha la mwaka huu ambalo ni la mwisho katika historia ya mfululizo wa matamasha ya Grown and Sexy waliona ni vema kumleta msanii maarufu toka Nigeria “Tekno Miles” ambaye aliwasili jana usiku mida ya saa nane akitokea Nigeria tayari kwa kulipamba Tamasha hilo. Msanii huyo ambaye anatamba na vibao mbalimbali kwenye anga ya muziki hivi sasa kama Shoki, Duro na Wash atatumbuiza laivu kwenye Tamasha hilo ambalo litafanyika siku ya mkesha wa mwaka mpya katika ukumbi wa King Solomon uliopo Namanga, Msasani karibu na Best Bite.

Sambamba na uwepo wa msanii huyo wengine wataopamba Tamasha hilo ni Dj Maarufu “Young Guru” ambaye ni Dj rasmi wa msanii Jay Z toka Marekani ambaye ataisimamia shoo hiyo vilivyo pamoja na malkia wa uswazi mwanadada “Shaa” kisura wa Tamasha hilo ambaye atasherehesha shughuli nzima katika usiku wa tukio.

Kwa upande wake Msanii Tekno alisema anafurahia kusherekea mkesha wa mwaka mpya akiwa Tanzania na kuahidi kuporomosha burudani ya nguvu kwa mashabiki wake watakaojitokeza kushuhudia Tamasha hilo la kufunga mwaka.

No comments:

Post a Comment