TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Thursday, August 7, 2014

IPTL/PAP kuendeleza ujenzi kuendeleza ujenzi wa kanisa la Pugu Chanika SDA

 KANISA la Waadventista wa Sabato la Pugu Chanika lililopo nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam sasa linaweza kuendeleza mradi wake wa ujenzi na upanuzi wa kanisa baada ya kupata msaada wa fedha wa shilingi milioni 5 kutoka kampuni ya ufuaji umeme ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL). Msaada huo uliotolewa wakati wa ibada Jumamosi, umefufua jitihada la kanisa za kutanua na kumalizia ukumbi wa kanisa uliopo sasa pamoja na kumalizia ujenzi wa majengo mengine.

Mwakilishi kutoka IPTL ambayo ni kampuni tanzu ya Pan African Power Solutions Tanzania (PAP), Bw. Joseph Makandege, ambaye ni Katibu na Mwanasheria Mkuu wa kampuni hiyo, amesema msaada huo ni sehemu ya jitihada za kampuni yake kuunga mkono miradi mbali mbali yenye manufaa makubwa kwa kijamii.

“Baada ya kupokea maombi toka katika kanisa hilo ya kututaka kusaidia mradi huo wa ujenzi, Bodi ya wakurugenzi ya IPTL/PAP ikiongozwa na Mwenyekiti Mtendaji Bw. Harbinder Singh Sethi mara moja ilipitisha kiasi cha shilingi milioni 5 kwa kuwa inaamini kuwa taasisi za kidini zinasaidia kulijenga taifa lenye watu wanaomuogopa Mungu na hivyo kuifanya nchi iwe na mazingira mazuri ya kufanya biashara ambayo inasaidia kuleta maendeleo ya kiuchumi.

“Tunaamini kuwa katika makanisa, familia zilizotengana zinaunganishwa, waliuokosa matumaini wanapewa matumaini, na maisha ya watu yanabadilika. Inampendeza Mungu kusikia sauti za nyimbo zinazomtukuza, ujumbe madhubuti kutoka kwa wachungaji, ushuhuda wa kazi zitokanazo na Mungu, na sauti nzuri za watoto zisema Amina.

“Kampuni yetu isingeweza kukataa ombi hilo la kusaidia kanisa katika mradi ambao utatukuza kazi ya Mungu na maisha ya walio wengi katika jamii yetu yatabadilishwa kwa ujumla,” alisema Makandege. Aliliasa kanisa kutumia fedha hizo vizuri ili kuweza kufikia malengo yaliyokusudiwa.

Naye, Mchungaji wa Kanisa hilo, Gallus Gido aliishukuru IPTL/PAP kwa mchango wao ambao alisema umewagusa watu wengi na utalisaidia kanisa kuweza kuwahudumia waumini wengi wanaomtukuza na kumuomba Mungu.

"Katika kitabu cha Matendo 10:1-4, kulikuwa na mtu aliyekuwa akitoa misaada/sadaka kwa jamii yake. Siku moja Mungu alimtokea na kumwambia kwamba sala na sadaka zake zimefika mbinguni. Nataka kuwaambia IPTL/PAP kwamba mchango wao wa kuendelea kusaidia taasisi mbalimbali ya kidini na jamii kwa ujumla, utawafungulia milango mbinguni kwa ajili ya baraka zaidi," alisema.

Mchungaji aliongeza kuwa mchango wa IPTL/PAP unadhihirisha upendo wa kampuni hiyo kwa Mungu na watu, na kuhaidi kuwa atafanyakazi kwa ukaribu na kamati ya ujenzi kuhakikisha kuwa fedha hizo zinatumika vizuri kwa lengo lililokusudiwa.

No comments:

Post a Comment