TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Monday, August 4, 2014

WAZIRI MKUU MHE. MIZENGO PINDA ATEMBELEA BANDA LA HALMASHAURI YA WILAYA YA SUMBAWANGA KATIKA MAADHIMISHO YA NANENANE NYANDA ZA JUU KUSINI JIJINI MBEYA LEO

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mizengo Pinda akisalimiana na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga Ndugu Adam Misana alipotembelea banda la Halmashauri ya Wilaya hiyo leo tarehe 02/08/2014 katika maonyesho ya wakulima Nanenane nyanda za juu kusini Jijini Mbeya ambapo alipokelewa na viongozi waandamizi wa Serikali ya Mkoa wa Rukwa wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa huo Eng. Stella Manyanya (Pichani Kulia).
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mizengo Pinda (aliyeshika boga kushoto) akisikiliza maelezo ya kilimo bora cha maboga alipotembelea banda la Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga leo tarehe 02/08/2014 katika maonyesho ya wakulima Nanenane nyanda za juu kusini Jijini Mbeya. Kulia kwake ni Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji na Uwezeshaji Dkt. Merry Nagu na pichani kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Eng. Stella Manyanya.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mizengo Pinda akipokea maelezo kutoka kwa mjasiriamali kuhusu kilimo cha Uyoga alipotembelea banda la Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga leo 02/08/2014 katika maonyesho ya wakulima Nanenane nyanda za juu kusini Jijini Mbeya.  Wa pili kushoto ni mwanasiasa nguli nchini na Mbunge wa zamani wa jimbo la Kwela Dkt. Chrissant Mzindakaya.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mizengo Pinda wa pili kushoto akiangalia mbegu ya uyoga alipotembelea banda la Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga leo tarehe 02/08/2014 katika maonyesho ya wakulima Nanenane nyanda za juu kusini Jijini Mbeya. Wa kwanza kushoto ni mwanasiasa nguli nchini na Mbunge wa zamani wa Jimbo la Kwela Dkt. Chrissant Mzindakaya na wa pili kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Eng. Stella Manyanya.
Kilimo cha uyoga ni rahisi kwani sio lazima uwe na shamba, kama unavyoonekana pichani.
Picha ya pamoja kati ya Waziri Mkuu Mhe. Mizengo Pinda, viongozi wa serikali mkoani Rukwa na wajasiriamali wadogowadogo mara baada ya kutembelea banda la Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga leo tarehe 02/08/2014 katika maonyesho ya wakulima Nanenane nyanda za juu kusini Jijini Mbeya. Na Hamza Temba - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa @Rukwareview.blogspot.com)

No comments:

Post a Comment