TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Thursday, February 5, 2015

Jumuiya ya Afrika Mashariki mfano wa kuigwa Afrika- Rais Gauck

images Immaculate Makilika –MAELEZO ARUSHA
Rais wa shirikisho la Ujerumani,Jochim Gauck ameonesha  kufurahishwa  na utendaji wa kazi wa Jumuiya ya afrika mashariki, EAC,  na kusema  ikiwa Jumuiya hii itatimiza malengo yake iliyojiwekea basi itakua mfano bora Afrika’.
 
Rais huyo ameyasema hayo leo alipotembelea makao makuu ya jumuia ya Afrika Mashariki EAC, mjini Arusha, ikiwa ni muendelezo wa ziara yake ya siku sita nchini na kusema kuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki EAC inafaida ya kuwa na nchi zenye uchumi unaendelea kukua kwa asilimia 6 katika kipindi cha miaka 10 iliyopita.

Rais Kikwete aongoza kikao cha Baraza la Mawaziri Dodoma leo

JOVAGO yashirikiana na Tigo Pesa kwa ajili ya malipo.

index
Jovago imetangaza leo kwamba imeingia katika ushirikiano na Tigo Tanzania, kampuni ya simu inayoongoza nchini. Katika ushirikiano huu, wateja wa Tigo Pesa sasa wataweza kulipia malazi yao kupitia akaunti zao za Tigo Pesa. Hii inakuja wakati muafaka ambapo muingiliano wa malipo ya pesa kupitia simu za mkononi katika tovuti za intanet umeonekana kama kiungo muhimu katika ukuaji wa sekta ya utalii katika mitandao.

MATAWI YA SHIRIKA LA BIMA (NIC) NCHINI KOTE YAUNGANISHWA NA MKONGO WA MAWASILIANO WA TAIFA

1Mkurugenzi wa Shirika la Bima la Taifa NIC Bw. Justin Mwandu akizungumza wakati wa uzinduzi wa huduma za shirika hilo kupitia mkongo wa taifa wa mawasiliano ambapo matawi yote nchini ya shirika hilo yameunganishwa pamoja na makao makuu ili kurahisisha huduma za bima  zinazotolewa na Shirika hilo nchini kote, Amesema kwa sasa baada ya Kampuni ya simu ya TTCL kufanya kazi nzuri ya kuunganisha mtandao wa huduma za NIC nchini kote kupitia mkongo wa mawasiliano wa taifa mteja anaweza kuhudumiwa mahali popote kama vile yuko makao makuu ya NIC Dar es salaam bila kufuata huduma hiyo mbali. Hafla hiyo imefanyika kwenye makao makuu ya NIC mtaa wa Samora jijini Dar es salaam leo, Katika picha kulia ni Mkurugenzi wa shirika la simu Tanzania TTCL Dr. Kamugisha Kazaura. 2Mkurugenzi wa shirika la simu Tanzania TTCL Dr. Kamugisha Kazaura akielezea kazi nzuri iliyofanywa na shirika lake la TTCL katika kuunganisha matawi ya NIC mikoani na Makao makuu ili kuleta pamoja huduma za bima zinazotolewa na shirika hilo hapa nchini, Kushoto ni Mkurugenzi wa Shirika la Bima la Taifa NIC Bw. Justin Mwandu.

TANZANIA YASHIRIKI MKUTANO WA MWAKA WA MAFUTA NA GESI ULIOANDALIWA NA GENERAL ELECTRIC (GE) (GE OIL & GAS ANNUAL MEETING 2015)

unnamedl1Mkurugenzi Mtendaji wa TPDC, Dr. James Mataragio akiongea katika mkutano wa mwaka wa GE Oil & Gas uliofanyika Florence, Italy unnamedl4Waziri wa Nishati na Madini, Mhe. George Simbachawene (aliesimama katikati) akibadilishana mawazo na CEO wa Exxonmobil (Moja ya Kampuni kubwa ya Mafuta na Gesi duniani). Aliesimama sambamba na Waziri ni Mkurugenzi Mtendaji wa TPDC, Dr. James Mataragio na aliekaa ni Rais na CEO wa GE Oil & Gas, Lorenzo Simonelli.

TAMKO LA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII JINSIA NA WATOTO KUHUSU SIKU YA KIMATAIFA YA KUPINGA UKEKETAJI

Tanzania-Coat-of-ArmsSiku ya tarehe 6 Februari, 2015; Tanzania itaungana na nchi nyingine duniani kupinga vitendo vya ukeketaji wa wanawake na watoto wa kike unaofanywa na baadhi ya jamii hapa nchini. Vitendo vya ukeketaji ni ukatili na unadhalilisha utu na hadhi ya mwanawake. Nchini Tanzania ukeketaji ni tatizo sugu na limedumu kwa muda mrefu. Waathirika zaidi wa ukeketaji ni wasichana wenye umri kati ya miaka 15-19 na watoto wa kike. Ukeketaji unafanywa kwa vile ni sehemu ya mila na desturi za baadhi ya makabila. Katika jamii zenye imani hii, ukeketaji unafanyika kwa wasichana ili waonekane kuwa wamefikia rika la watu wazima. Aidha, kwa mangariba na wazee wa kimila kimekuwa ni kichocheo cha vitendo hivyo dhalili kwani wanategemea mapato kutokana na ukeketaji. Hapa nchini, mikoa yenye matukio ya ukeketaji ni pamoja na Manyara (71%), Dodoma (64%), Arusha (59%), Singida (51%), Mara (40%), Morogoro (21%) na Tanga (20%).

Kikao cha Baraza la Wafanyakazi OMR chafanyika leo

Rais Kikwete kuongoza kikao cha Baraza la Mawaziri Dodoma

jakayaRais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiendelea kuchapa kazi ndani ya ndege yake akiwa safarini kutoka Dar es Salaam kuelekea mjini Dodoma ambapo aliongoza kikao cha baraza la Mawaziri(Picha na Freddy Maro)

Mjumbe wa NEC Ludewa ambae ni mwenyekiti wa UVCCM wilaya hiyo afariki dunia

 Aliyekuwa MNEC  wa  wilaya ya  Ludewa  Elizabeth Haule  wa  pili kushoto enzi za uhai  wake  akiwa na viongozi  wa  wilaya  hiyo wakati wa mkutano mkuu wa wilaya ya  Ludewa mwaka jana ,kulia  ni mbunge wa  jimbo la Ludewa Deo Filikunjombe ,aliyesimama ni mwenyekiti  wa CCM wilaya  ya Ludewa Stanley Kolimba na wa kwanza  kushoto katibu  wa CCM wilaya ya  Ludewa Eliud Semauye .

MAADHIMISHO YA SIKU YA SARATANI DUNIANI

unnamedz1Mwenyekiti wa Jumuiya ya watu wanaoishi na Saratani Zanzibar Dkt. Msafiri Marjani akitoa elimu juu ya ugonjwa wa Saratani katika mkutano wa maadhimisho ya siku ya Saratani Duniani uliofanyika ofisini kwao Mpendae Zanzibar.
unnamedz2

MALIASILI NA UTALII WAENDELEA KUTANGAZA VIVUTIO VYA UTALII MAREKANI

unnamedk1Ujumbe wa Tanzania ulioshiriki katika ziara ya kutangaza vivutio vya utalii nchini katika soko la Marekani Magharibi.
unnamedk2Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Dk. Adelhelm Meru (kulia) akimpa zawadi ya kinyago Naibu Meya wa jiji la Seattle nchini Marekani Bi. Kim mara baada ya kumaliza mazungumzo yao

MKUU WA MKOA WA RUKWA ENG. STELLA MANYANYA AONGOZA SIKU YA SHERIA NCHINI MKOANI RUKWA

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Eng. Stella Manyanya kulia akihutubia katika maadhimisho ya siku ya sheria nchini Mkoni Rukwa leo tarehe 04/02/2015 katika viwanja vya Mahakama Kuu Kanda ya Sumbawanga. Kaulimbiu ya maaadhimisho hayo ikiwa “Fursa ya kupata haki: Wajibu wa Serikali, Mahakama na Wadau”. Katika hotuba yake hiyo alisema ipo haja kubwa kwa Serikali kubadili sheria zake ili lugha ya mahakamani na hukumu ziandikwe kwa kiswahili. Kwa upande wa wananchi aliwaasa kujiepusha na tabia ya kujichukulia sheria mkononi ili kudumisha amani nchini.
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Sumbawanga Mhe. Jaji Sambo akipokea gwaride la heshima kutoka kwa kikosi cha Jeshi la Polisi wakati wa maadhimisho ya siku ya Sheria Mkoani Rukwa leo tarehe 04/02/2015.

TCRA, STARTIMES WABAINISHA TATIZO LINALOPELEKEA KUTOONEKANA VIZURI KWA CHANELI ZA ITV/EATV

 Mhandisi wa Masafa kutoka  Mamlaka ya Udhibiti wa Mawasiliano nchini, TCRA, Bw Francis Mihayo (kushoto)akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya tatizo la kutoonekana vizuri kwa chaneli za ITV na EATV katika king’amuzi cha kampuni
hiyo, kulia kwake akifuatilia kwa makini ni Meneja Masoko wa kampuni hiyo, Bw David Kisaka. Katika mkutano huo Mamlaka ya Udhibiti wa Mawasiliano nchini,TCRA na StarTimes walitoa ufafanuzi juu ya tatizo linalopelekea tatizo hilo,mkutano huo uliofanyika leo katika duka la kampuni hiyo lililopo Mikocheni-Bamaga jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Ufundi wa StarTimes Tanzania, Bw Abdulkadir Mbeo (kushoto) akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya tatizo la kutoonekana vizuri kwa chaneli za ITV na EATV katika king’amuzi cha kampuni hiyo na kulia kwake
akifuatilia kwa makini ni Meneja Masoko wa kampuni hiyo, Bw David Kisaka.

Wednesday, February 4, 2015

RAIS JAKAYA KIKWETE AKUTANA NA WAZIRI WA MAMBO YA NJE WA IRAN

ir1Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete akimlaki na kisha kufanya mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislam ya Iran, Mheshimiwa Javad Zarif na ujumbe wake Ikulu jijini Dar es salaam jana, Jumatano, Februari 4, 2015. PICHA NA IKULU ir2Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho
Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na  Waziri wa Mambo ya Nje
wa Jamhuri ya Kiislam ya Iran, Mheshimiwa Javad Zarif na ujumbe wake
baada ya kufanya mazungumzo Ikulu jijini Dar es salaam jana, Jumatano, Februari 4, 2015. PICHA NA IKULU

Establish an inclusive multi-stakeholder Education

ft1Mr. Bertin Mushi, Marketing Manager, Promasidor Tanzania Ltd and Ms. Fatma Fernandes from Abel & Fernandes Company Ltd exchanging ideas with primary school children at the Launch of Hatua Jithamini TV show.
ft2Children from different primary schools at the launch of Hatua Jithamini Show which will be aired on Star TV every Saturday at 7.30 pm to 8pm and TV1 at 11.30am.

PINDA AZUNGUMZA NA VIONGOZI WA DINI

p4Baadhi ya washiriki wa Mkutano wa viongozi wa dini wa mashauriano uliofanyika kwenye Kituo cha Mikutano cha  Kimataifa cha  Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es slaam Februari 3, 2015. (Picha na Ofisi ya Waziri mkuu)p5 Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza katika kikao cha  mashauriano cha viongozi wa dini kilichofanyika kwenye Kituo cha  Mikutano cha Kimataifafa cha Julius Nyerere jijini Dar es salaam Februari 3, 2015. Kulia ni ni Sheikh wa Mkoa wa Dar es salaam ,Alhad Salum Musa.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

MULTICHOICE YAZINDUA KING’AMUZI KIPYA CHA DStv HD

DSC_0100

Meneja Uhusiano wa MultiChoice Tanzania, Barbara Kambogi (Katikati) akifafanua jambo kwenye mkutano na wanahabari  (hawapo pichani), wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa king’amuziki kipya cha  DStv HD  leo jijini Dar. Kulia ni kwake ni Meneja uendeshaji wa Multichoice Tanzania, Ronald Shelukindo na kushoto ni Meneja Masoko wa Multichoice Tanzania, Furaha Samalu.

Na Andrew Chale
KAMPUNI ya MultiChoice Tanzania wasambazaji wa ving’amuzi vya DStv, leo imezindua king’amuzi kipya cha DStv HD ambacho kitaanza kutumika kwa mara ya kwanza hapa Nchini.
Akizungumza  na wandishi wa habari mapema leo jijini Dar es Salaam,  Meneja Uendeshaji wa MultiChoice Tanzania, Ronald Shelukindo, akielezea umuhimu wa huduma hizo alisema king’amuzi hicho kina ubora wa hali ya juu ikiwemo kuonyesha picha zenye ubora mzuri zaidi.
Pia alieleza kuwa, DStv HD mteja atapata kuona picha zenye mvuto zaidi pamoja na kiwango cha juu cha sauti Dolby Digital 5.1.
“Wateja wa DStv watafurahia ving’amuzi hivi kwa ubora wa hali ya juu  hivyo ni wakati wa kuchangamkia  ofa kwani ndio mara ya kwanza kuingia kwa Tanzania” alisema Ronald Shelukindo.
DSC_0239
Meneja uendeshaji wa Multichoice Tanzania, Ronald Shelukindo akielezea ubora wa king’amuzi hicho cha DStv HD wakati wa mkutano huo na waandishi wa habari leo jijini Dar.
Ronald Shelukindo akielezea kwa kina, alisema DStv HD, mteja anaweza kufurahia vipindi mbalimbali ikiwemo mifumo na mipangilio ya kila vipindi kwa kupendekeza atazame kipi gani, muda gani na wakati gani?.

Bunge laridhika na hali ya ulinzi na usalama wa raia

hussein
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dkt. Hussein Mwinyi akijibu swali la mbunge Bungeni Dodoma.

Wamiliki wa shule za sekondari watakiwa kuzingatia viwango vya ufaulu

kilango
Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Anna Kilango Malecela akijibu swali la Mh. Joseph Selasini Mbunge wa Rombo.
selasini
Mbunge la Mbunge wa Rombo Joseph Selasini, akiuliza swali.

Serikali yajenga barabara zenye urefu wa kilometa 42 mji wa Dodoma

jeni
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu na Bunge, Jenista Mhagama akijibu swali  Mbunge Bungeni.
………………………………………………………………………………..
Na Lorietha Laurence-Maelezo , Dodoma SERIKALI kupitia mradi wa uendelezaji miji (TSCP) imefanikiwa kujenga barabara zenye urefu wa kilometa 42 kwa mji wa Dodoma kwa msaada wa mfuko wa Benki ya Dunia. Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu na Bunge, Jenista Mhagama ameeleza hayo Bungeni Dodoma, kuwa ujenzi huo wa barabara umehusisha pia ujenzi wa mifumo ya maji ya mvua ,dampo la kisasa kwa kijiji cha Chidaya pamoja na mitambo y usombaji taka.