Rais wa
shirikisho la Ujerumani,Jochim Gauck ameonesha kufurahishwa na
utendaji wa kazi wa Jumuiya ya afrika mashariki, EAC, na kusema ikiwa
Jumuiya hii itatimiza malengo yake iliyojiwekea basi itakua mfano bora
Afrika’.
Rais huyo
ameyasema hayo leo alipotembelea makao makuu ya jumuia ya Afrika
Mashariki EAC, mjini Arusha, ikiwa ni muendelezo wa ziara yake ya siku
sita nchini na kusema kuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki EAC inafaida ya
kuwa na nchi zenye uchumi unaendelea kukua kwa asilimia 6 katika kipindi
cha miaka 10 iliyopita.



