TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Tuesday, January 31, 2012

BASATA KWA KUSHIRIKIANA NA JESHI LA POLISI SASA KUDHIBITI UHARAMIA KWENYE SANAA


Na Mwandishi Wetu
Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) na Jeshi la Polisi nchini wameunda kikosikazi maalum kitakachokuwa kikifuatilia uharamia na maovu mbalimbali katika shughuli za Sanaa na Burudani. 
Kikosikazi hicho kimeundwa baada ya Jeshi la Polisi nchini kutumia Sanaa shirikishi katika kutoa elimu kwa wadau wa Sanaa kuhusu dhana ya polisi jamii na ulinzi shirikishi kwenye Jukwaa la Sanaa linalofanyika kila wiki makao makuu ya BASATA Ilala Sharif Shamba.
Akizungumza kuhusu kikosikazi hicho, Mkurugenzi wa Ukuzaji Sanaa, BASATA Bi. Vivian Shalua alisema kuwa, kazi kubwa ya kikosi hiki itakuwa ni kufuatilia maonesho yasiyokuwa na vibali, uharamia kwenye kazi za wasanii na wasanii kutoka nje wanaoingia nchini kinyume cha sheria.
Aliyataja majukumu mengine ya kikosikazi hicho kuwa ni pamoja na kudhibiti maonesho yanayodhalilisha utu na maadili ya mtanzania, kusimamia utoaji vibali kwa wasanii wa kitanzania wanaoenda kufanya maonesho nje ya nchi na majukumu mengine yatakayojitokeza.
“Kikosikazi hiki kitakuwa tayari kufuatilia taarifa yoyote ya uharamia kwenye kazi za wasanii, maonesho yanayodhalilisha utu na maadili ya mtanzania na wasanii wanaoingia ndani ya nchi na kufanya maonesho bila vibali” alisisitiza Shalua. 
Kikosikazi hicho kinaundwa na Shani Kitogo (Afisa Utamaduni Ilala), Tatia Ramadhan (Polisi, TAZARA), Afande Jeremiah (Polisi Kati), Koplo Juma Mashauri (Polisi Airport), Michael Kagondela (Idara ya Utamaduni), Afande Deus Matoro (Reli) na Afande Swai (Traffic),
Wengine ni Vivian Shalua (BASATA), Jonathan Abel na Tatu Burhan (Uhamiaji), Deus Kessy (Polisi Reli), Koplo Josephat Syllively (Polisi – Maji), Masanja Nyalali (Polisi – Airport) na PC Mwakajaby (Polisi – TAZARA)
Akizungumza kwenye Jukwaa hilo la Sanaa, Asp Edson Kasekwa kutoka Polisi Makao Makuu Kitengo maalum cha Operesheni uzuiaji uhalifu,alisema kuwa, Jeshi la Polisi linawategemea wadau wa Sanaa wakiwemo wasanii katika kutoa taarifa juu ya matukio ya uharamia na uhalifu kwa ajili ya ufuatiliaji na udhibiti.
“Ni vema Wasanii na wadau wa Sanaa kwa ujumla wakaonesha ushirikiano kwa Jeshi la Polisi katika kutoa taarifa na kudhibiti uharamia na maovu kupitia sekta ya Sanaa. Hii ndiyo maana ya dhana hii ya polisi jamii na ulinzi shirikishi ya polisi kushirikiana na jamii” alisema Afande Kasekwa.
Kikosikazi hiki kimeundwa huku kukiwa na taarifa za uwepo wa vikundi mbalimbali vinavyofanya maonesho yenye kudhalilisha utu na maadili ya mtanzania huku uharamia kwenye kazi za Sanaa ukizidi kushika kasi.

No comments:

Post a Comment