TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Monday, January 30, 2012

BAYPORT KUTOA MSAADA WA VITABU KIBONDO

Bayport Manager masoko na uhusiano (aliyekaa kulia) Bwana Ngula Cheyo na bayport branch manager (aliyesimama kushoto) bwana Imani Mtewele katika uzinduzi rasmi wa huduma za jamii iitwayo ” Bayport books for schools’ katika shule ya msingi Boma iliyoko wilaya ya Kibondo mkoani Kigoma
Taasisi ya kifedha ya Bayport ,katika kampeni yake ya huduma za jamii iitwayo ” Bayport books for schools “ kutoa vitabu kwenye shule 20 katika wilaya 20 Tanzania bara sasa imezindua rasmi kampeni yake na kutoa vitabu vya darasa la kwanza katika shule ya msingi Boma iliyoko wilaya ya Kibondo mkoani Kigoma. Katika hafra hiyo mgeni ramsi alikuwa ndg Ndunduguru kwa niaba ya mkuregenzi wa halmashauri ya wilaya Kibondo. Manager masoko na uhusiano bwana Ngula Cheyo alisema Bayport iliaamua kutoa msaada wa vitabu darasa kwanza na kidato cha kwanza kwa kuwa tunaamini kumpa mtoto mwamko wa elimu ni lazima kumjengea msingi madhubuti mapema katika elimu yake ya chini yaani darasa la kwanza na kidato cha kwanza. Bayport itatoa vitabu 120 kwa kila shule za msingi ambavyo ni kwa masomo ya Sayansi,Hisabati Na kingereza pia vitabu 80 kwa kila shule za sekondari kwa masomo ya Sayansi,Hisabati na atlasi 2 Wakati huo huo Bayport ilizindua rasmi tawi Kibondo ambalo ni tawi la 60 miongoni mwa matawi yake Tanzania. Manager wa tawi la kibondo Bwana Imani Mtewele alisema kwamba amefurahi sana kwani sasa wateja wa kibondo wanapata huduma zao kwa uhakika na ukaribu zaidi.

No comments:

Post a Comment