TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Friday, February 3, 2012

Watoto wanaotoka katika mazingira hatarishi, na yatima wapewa msaada wa milioni 9 na laki sita

Na Gladness Mushi. - Arusha
Mfuko Wa maendeleo ya jamii Manispaa ya Arusha umefanikiwa kutoa msaada kwa mayatima 183 pamoja na wale ambao wanatokea mazingira hatarishi ambao unagarimu million tisa na laki sita kwa kuwapa mahitaji muimu ya shule .ikiwemo suala zima la ada
Akiongea na vyombo vya habari mapema wiki hii mratibu wa mfuko huo Bw Ernest Mkonyi alisema kuwa mfuko huo ulifikia hatua hiyo mara baada ya kuona kuwa watoto hao ambao wengi wao ni mayatima wana umuhimu wa kupata elimu zazidi.
Bw Mkonyi alisema ,kuwa suala la elimu kwa watoto hao ambao ni mayatima ni muhimu sana kwa kuwa wengi wao wanakosa haki zao za msingi za kupata elimu kwa ,kile kinachosababiswa NA MAPUNGUFU mbalimbali ndani ya jam;ii zao
Aliendelea ,kwa kusema kuwa ;hapo awali watoto hao walikuwa hawapati haki zao za msingi kwa kuwa ndani ya jamii zao hawakuweza kuwahudumia mahitaji yao ya muhimu kama vile ada kwa kuwa na hali ngumu ya maishahivyo kushindwa kumudu
“Unajua hawa watoto hawakuweza kwenda shule kwa wakati lakini sisi kama wadau wa sekta ya elimu tunamefanikiwa kuendelea kuwasaidia watoto hawa mahitaji mbalimbali kama vile ada, sare za shule na kwa sasa wanaedelea vema na masomo “alisema Bw. Mkonyi
Pia alisema kuwa watoto hao ambao kati yao ni mayatima na waliotoka katika mazingira magumu wametokea katika kata tatu ndani ya manispaa ya Arusha na kujumuisha kata za Elerai,Ungalmtd, na Sokoni one mjini hapa.
Aidha akielezea mpango makkati wa mfuko huo wa Maendeleo ya ,jamii ni kuhakikisha kiuwa wanchangia sekta ya elimu kwa ,kiwango kikubwa zaidi, huku wakiwakutanisha wazazi na walezi ambao wanajtokea mazingira ya chini kwa kuwapa mbinu za kubuni miradi iliu kujikwamua .kimaisha zaidi.
Alisema kuwa kupitia mpango huo wa kuwakutanisha utaweza kuwasidia wakazi hao na hivyo wao wenyewe kuweza kuinua na kuchangia sekta ya elimu hata kwa ,kuwasomesha watoto ambao wanatokea katika mazingira hatarishi na wengine wakiwa mayatima
Alitoa mwito kwa watanzania wote kuhakikisha kuwa jamii inatambua uwepo wa watoto yatima na wanaotokea katika mazingira hatarishi, kwa kuwapa mahitaji yao muhimu ili kuweza .kufanikisha katika kuinua kiwango cha jamii hapa nchini

No comments:

Post a Comment