TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Tuesday, January 31, 2012

SHULE YA MSINGI MGABE YAPATIWA MSAADA WA MADAWATI NA BENKI YA KCB WENYE THAMANI YA MILIONI 6 NA LAKI 5



Benki  ya KCB Tanzania imetoa ime kabidhi msaada wa vifaa mbalimbali vya shule kwa shule ya Msingi Mugabe,Sinza Maalum na Shule ya Uhuru mchanganyiko wenye thamani ya zaidi ya  sh. Milioni 18.4.
Akikabidhi msaada huo mwenyekiti wa bodi ya benki hiyo Dokta Edmund Mndolwa alitaja miongoni mwa vifaa hivyo ni madawati,vywakula ,vifaa vya michezo na vinginevyo.

Dkt.Mndolwa allisema  nsaada huo unaonesha ni kwa jinsi gani benki yake inazingatia wajibu wake wa kusaidia jamii inayoizunguka kupitia sekta ya elimu,afya ,mazingira na maafa mbalimbali ili kupunguza umasikini nchini.
Amewataka kutunza vifaa hivyo ili viweze kudumu kwani ni vya gharama na viweze kutumika na wanafunzi wengine kwa manufaa ya jamii nzima.
“Napenda kuchukua fursa hii kuwafahamnisha kwamba Benki ya KCB inatoa huduma mbalimbali kwa wananchi 

wanoizunguka,tunaamini kuwa jamii inayotuzunguka nayo itatuunga mkono kwa kuchangamkia huduma zetu ambazo ni pamoja na kufungua akaunti,kuchukua mikopo ya nyumba na biashara”alisema .
Akizungumza kwa niaba ya wanajumuiya ya Mugabe shule ya Msingi, Mwalimu Mkuu  wa Shule hiyo ya Sinza Maalum Bw.Asafu Mahelele alisema  pamoja na msaada huo bado wanakabiliwa na changamoto ya vifaa vya kufundishia ikiwemo Vitabu vya Kiada, Uchakavu wa
Mapaa ya Majengo ya Shule na ubovu wa Miundombinu ya vyoo vya Walimu na Wanafunzi na kudai kuwa watayatunza ili yaweze kutumiwa kwa muda mrefu.
"Tunashukuru kwa msaada huu mdogo kutoka benki hii ya KCB,bado tuna changamoto nyingi zinazotukabili ikiwemo  ukosefu mkubwa wa vitabu vya kiada ,uchakavu wa mapaa ya majengo ya shule  yetu na ubovu wa miundombinu ya vyoo vya walimu na wanafunzi"alisema Bw.Mkiramwene.
KCB Tanzania ndiyo benki kongwe kuliko zote Afrika Mashariki ikiwa iliyoanza kuanzishwa Zanzibar mwaka 1896 na badae kusambaa Mombasa ,Nairobi, na kurudi nchini mwaka 1997.
Baadhi ya Walimu wa Mugabe, Wanafunzi pamoja na Wafanyakazi wa KCB Benki wakiwa kwenye Moja ya Madawati yaliyokabidhiwa leo.
Viongozi mbalimbali wa Serikali, wanafunzi wa shule ya Mugabe na Maafisa wa Benki ya KCB katika picha ya pamoja.

No comments:

Post a Comment