TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Friday, February 3, 2012

Rais azungumza na Uongozi wa Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein,akizungumza na Uongozi na watendaji wa Wizara ya nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,katika ukumbi wa mikutano Ikulu Mjini Zanzibar jana,katika utekelezaji wa kazi za Wizra hiyo.(Picha na Ramadhan Othman Ikulu.) 02/02/2012
Watendaji wa Wizara ya Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Ikulu,wakiwa katika kikao cha siku moja cha utekelezaji wa kazi za Wizara hiyo, chini ya Mwenyekti wake Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, jana Ikulu Mjini Zanzibar.(Picha na Ramadhan Othman IKulu)

Makamu wa rais wa Jamhuri ya Muugano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa mtaalum, kuhusu ufugaji wa Kuku wa mayai, wakati alipotembelea na kuweka Jiwe la msingi katika kituo cha Shamba la Kuku kilichopo Kijiji cha Mkiu Wilaya ya Mkuranga, Mkoa wa Pwani, leo Januari 02, 2012, wakati akiwa katika ziara yake ya Mkoa wa Pwani.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akitembelea na kukagua mabanda ya kufugia kuku katika kituo hicho cha Shamba la Kuku kilichopo Kijiji cha Mkiu Wilaya ya Mkuranga akiwa katika ziara yake ya Mkoa wa Pwani, leo Januari 02, 2012.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipanda mti wa kumbukumbu katika eneo la mradi wa Ujenzi wa Kituo cha mnada wa Ng’ombe katika Kijiji cha Mkiu Wilaya ya Mkuranga, wakati akiwa katika ziara yake ya Mkoa wa Pwani leo, Januari 02, 2012.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiweka Jiwe la Msingi la mradi wa ujenzi wa Kituo cha mnada wa Ng’ombe katika Kijiji cha Mkiu Wilaya ya Mkuranga, akiwa katika ziara yake ya Mkoa wa Pwani, leo Januari 02, 2012.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akitembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa Kituo cha mnada wa Ng’ombe katika Kijiji cha Mkiu Wilaya ya Mkuranga, akiwa katika ziara yake ya Mkoa wa Pwani, leo januari 02, 2012.

A round of applause rings after President Jakaya Mrisho Kikwete has officially launched the First National Bank Tanzania (FNB-Tanzania) yesterday at the Kilimanjaro Grand Hyatt hotel in Dar es salaam. Others from left are the High Commissioner of South Africa to Tanzania, Mr Thanduyise Henry Chiliza, the CEO of FirstRand, Mr Sizwe Nxasana and the Deputy Permanent Secretary in the Ministry of Finance Ms Elizabeth Nyambibo. (Photo by State House)
President Jakaya Mrisho Kikwete makes his keynote speech during the official launch of the First National Bank Tanzania (FNB-Tanzania) yesterday at the Kilimanjaro Grand Hyatt hotel in Dar es salaam today February 2, 2012.

NA: ASHURA MOHAMED-ARUSHA
Katika harakati za kuhakikisha kuwa kunakuwepo na taarifa sahihi pamoja na takwimu juu ya unyanyasaji wa kijinsia ikiwa ni pamoja na kufanyika kwa tafiti na utunzaji wa kumbukumbu serikali kupitia wizara ya maendeleo ya jamii jinsia na watoto imewakutanisha wadau mbalimbali katika warsha kuhusu uanzishwaji wa kituo cha kitaifa cha utafiti na kumbukumbu za wanawake katika eneo la tengeru wilaya ya arumeru mkoani Arusha.
Akifungua warsha hiyo naibu katibu mkuu wa wizara ya maendeleo ya jamii jinsia na watoto Anna .T.Maembe amesema kuwa kuanzishwa kwa kituo hicho kutaiwezesha serikali kuwa na takwimu za kitaifa juu ya unyanyasaji wa kijinsia hivyo itarahisisha utatuzi wa changamoto hizo kwa kuwa watakuwa bna takwimu sahihi.
Anna amesema kuwa lengo la kuanzishwa kwa vituo vya kitaifa ni kushirikiana na kituo cha kanda katika kufanya tafiti mbalimbali,kuimarisha mahusiano,kubadilisha uzoefu ,kutunza kumbukumbu na kupashana habai zinazohusu haki za wanawake na usawa wa kijinsia.
Aidha amesema kuwa vituo hivi vitahamasisha wadau mbalimbali kuhusu usawa wa kijinsia,ulinzi na kuheshimu haki za wanawake lengo likiwa ni kuwajengea uwezo wadau mbalimbali ili waweze kufanya tafiti wa masuala ya yanayohusiana na usawa wa kijinsia na kuhakikisha kuwa wanawake wanashiriki kikamilifu na wanachangia kuleta maendeleo endelevu katika nchi wananchama hasa ziliathirika na vita.
Pia amefafanua kuwamadhumuni ya warsha hiyo ni kuwapatia taarifa juu ya uwepo wa kituo cha kanda kilichopo katika chuo cha ustawi wa jamii Tengeru kuwa ndicho kilichochaguliwa hapa nchini,kubadilishana uzoefu na kutoa mapendekezo ambayo yatasaidia kakufanikisha shughuli zitazofanywa nakituo cha utafitina kumbukumbu za wanawake.
Naye mwakilishi kutoka shirika la UNESCO Modester Munira amesema kuwa kwa kutambua umuhimu wa kutunza nyaraka tume ya taifa unesco iliona ni vyema kikaanzishwa kwa kituo hicho kwa kushirikiana na wizara ya maendeleo ya jamii jinsia na watoto hivyo amatakataarifa zitolewe kwa uwazi zaidi.

Na Lydia Churi, MAELEZO, Dodoma
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Emmanuel Nchimbi amesema Serikali inakubali kuwa wastaafu kupewa mkataba wa kuendelea kufanya kazi si sahihi na kuahidi kuwa suala hilo litafanyiwa kazi.
Akifanya majumuisho wakati wa mjadala wa Azimio la kuridhia mkataba wa vijana wa Afrika (The African Youth Charter) waziri Nchimbi alisema hatua ya wastaafu kupewa mikataba ya kuendelea na kazi inawanyima vijana haki ya kupata ajira katika taasisi mbalimbali.
Akizungumzia suala la maadili kwa vijana Mheshimiwa Nchimbi alisema hivi sasa vijana wakiwemo baadhi ya viongozi wanaotoa michango yao juu ya mambo mbalimbali katika mitandao kama vile facebook na twitter wanatumia lugha zisizojenga na badala yake aliwataka kutoa michango isiyokuwa na madhara kwa vijana wa taifa hili hasa ile inayotumia lugha zinazojenga ili kulinda maadili ya Mtanzania.
Aliwataka viongozi kuwa wa kwanza kupiga vita matumizi mabaya ya mitandao na kuacha tabia za kulipiza visasi pale wanapokosana na wenzao kwani hizo si sifa za kiongozi bora. “kiongozi bora na imara ni yule mwenye tabia ya kusamehe, alisema”.
Kuhusu mchakato wa kutafuta vazi la taifa waziri huyo alisema wizara yake inatekeleza maagizo yaliyotolewa na bunge na kuwaomba wabunge kuwa wa kwanza kuunga mkono wizara ya habari, Vijana, Utamaduni na Michezo inapotekeleza maagizo hayo. Aliongeza kuwa kamati iliyoteuliwa kutafuta vazi la taifa ni makini kwa kuwa imeundwa na watu makini waliotoka kwenye kada mbalimbali.
Awali akichangia mjadala huo, Mbunge wa Kigoma Mjini (CCM) Peter Serukamba alisema suala la wastaafu kupewa mkataba wa kuendelea na kazi halifai kwa kuwa linawanyima vijana haki yao ya kupata ajira. Alitoa mfano kuwa hivi sasa wenyeviti wa bodi wengi ni wastaafu ambapo ilipaswa nafasi hizo kuchukuliwa na vijana.
Alisema suala la uzoefu kuwa miongoni mwa sifa za kupata ajira si haki kwa kuwa linawanyima vijana nafasi ya kupata ajira hizo. Alisema vijana wawapo vyuoni hupatiwa muda wa kufanya mazoezi ya kazi na hivyo kuwa na uzoefu wa kutosha.
Bunge limeridhia mkataba wa kimataifa wa vijana isipokuwa limeridhia kwa stara ibara mbili zinazohusu sera ya taifa ya vijana na suala la vijana wa kike wanaopata ujauzito au kuolewa kabla ya kumaliza elimu zao kupewa fursa ya kuendelea na masomo.
Bunge limeridhia kwa stara ibara hizo kwa kuwa Sera ya Taifa ya Vijana kwa taratibu za nchi yetu hupitishwa na baraza la mawaziri na sheria hutungwa na bunge wakati mkataba unasema Sera itapitishwa na kukubaliwa na bunge na kufanywa sheria.
Kwa upande wa elimu kwa vijana wa kike waliopata ujauzito masomoni, mkataba unataka wasichana wa kike wanaopata ujauzito masomoni kuepwa firsa ya kuendelea na masomo wakati sheria za nchi yetu bado haziruhusu vijana wa kike waliopata ujauzito masomoni kuendelea na masomo.

No comments:

Post a Comment