TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Wednesday, February 1, 2012

CHAMA CHA MAPINDUZI CCM NA POSHO ZA WABUNGE

Kwa upande mwingine Chama Cha Mapinduzi kinapenda kurudia wito kilioutoa juu ya swala la posho za wabunge. CCM iliwaomba na kuwasihi wabunge na mamlaka zinazohusika na mchakato wa swala hili kuliangalia upya na kutumia busara, ikiwezekana kuachana nalo kwasasa. CCM inaupongeza na kuunga mkono msimamo wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. Jakaya Mrisho Kikwete kama ulivyonukuliwa na taarifa ya Ikulu kwa vyombo vya habari, kuwa ni vizuri wabunge wakalitafakari upya swala hili kwa masilahi mapana ya wale waliowapa dhamana ya kuwawakilisha bungeni. CCM inaendelea kuwasihi waheshimiwa wabunge walitafakari upya swala hili na busara itumike katika kuliamua huku wakifungua masikio kusikiliza sauti za Watanzania kwani huko bungeni wana wawakilisha hawa Watanzania, ni vizuri kusikiliza hiki kilio chao! Si busara kupuuza kilio cha waliokupa dhamana ya kuwawakilisha. Msimamo wa Rais Kikwete kama sehemu moja ya mamlaka inayohusika na mchakato huo ni uthibitisho wa usikivu wake kwa wananchi anaowaoongoza, yeye katimiza wajibu wake, tunawasihi waheshimiwa wabunge wetu nao walitafakari hili na kuona busara ya kuachana nalo kwasasa.

Kwa muda sasa nchi yetu imepitia kwenye tatizo kubwa la mgomo wa madaktari katika hospitali nyingi hasa za umma ambao kwa kiasi kikubwa mgomo huo umekuwa na madhara makubwa kwa watanzania masikini ambao ni wengi, kiasi cha kugharimu hata maisha yao. Chama Cha Mapinduzi kinachukua nafasi hii kuwapa pole sana wale wote walioathiriwa kwa namna moja ama nyingine na mgomo huu. Na kwakweli tunasikitishwa sana na hali inayoendelea! Chama Cha Mapinduzi kinawapongeza na kuwashukuru madakitari walioonyesha ubinadamu na uzalendo kwa kuamua kurudi kazini na ambao hawakugoma kabisa. Tunawashukuru na kuwapongeza kwani hakuna masilahi yanayovuka thamani ya uhai wa binadamu mwenzako! Tunachukua fursa hii pia kuwashukuru sana na kuwapongeza askari wetu wa jeshi la wananchi wa Tanzania kwa uamuzi wao wa kizalendo wa kuamua kuitikia wito wa serikali kwenda kwenye baadhi ya hospitali kusadia kuwatibu watanzania wenzao. Moyo huu ni wa kizalendo na wa mfano. Tunajivunia uzalendo wa jeshi letu! Tunachukua nafasi hii kuwaomba madaktari wanaoendelea na mgomo kurudi kazini huku wakiendelea na mazungumzo na serikali. Tunaamini madai yao yanawezekana kushughulikiwa ikiwa pande zote mbili zitaamua kukaa chini kwa dhati na kuzungumza. Serikali kwa upande mmoja watafute kwa makini chanzo cha mgogoro huu na kutafuta majibu, na madakitari nao kwa upande wa pili, wawe tayari kukaa mezani na kuzungumza. Tunasisitiza thamani ya maisha ya binadamu ni kubwa kuliko masilahi na madai wanayoyaomba! Serikali ni vizuri ikajenga utamaduni wa kushughulikia matatizo haya ambayo yanaathiri wananchi wengi kwa uharaka na udharura unaostahili badala ya kusubiri hali inapokuwa mbaya zaidi.

ACP Kashai akikagua kikosi cha kutuliza ghasia na mafunzo aliyo toa kukabiriana na majanga
ACP Kashai akikagua kikosi cha kupambana na majambazi kwa kutumia piki piki
Na Pardon Mbwate Mwandishi wa Jeshi la Polisi- kigoma
Askari wa mapokezi katika vituo vya Polisi hapa nchini, wametakiwa kuwa kioo cha Jeshi hilo kwa kuonyesha ukarimu na kauri nzuri wanapowahudumia wananchi wanaofika kwenye vituo hivyo ama wanapoombwa msaada mahala popote wanapoombwa kufanya hivyo.
ACP Frasser Kashai amesema hatua hiyo italiwezesha Jeshi hilo kuendelea kujenga heshma mbele ya Jamii wanayoihudumia na taifa kwa ujumla.
Akizungukia na Askari polisi, wakuu wa idala mbali mbali za polisi posti, Kamanda Kashai amesema dhamira ya Jeshi hilo ni kutaka kila askari kubadilika na kutoa huduma bora kwa wananchi. na kuwa makini katika utendaji wao wa kazi za kila siku kutoa huduma kwa mteja iliyo bora
Kamanda Kashai amesema hayo akiwa anakagua paledi ukaguzi huo uliofanyika na maafisa wake Kihenya Kihenya SSP na RCO Josephu Konyo SSP OCD Wilaya kigoma Jafeti Kibona D/SSGT Silvanusi Mazengo D/SSGT Deusidedith Magogo D/SGT Menas Temba ukaguzi huo uliowahusisha askari wa vikosi vyote pia ukaguzi huo ni pamoja na kesi wanazo peleleza na kutaka kujua wapi zimefikia na kuona hatua walizo chukua mazingila utabadili mwelekeo wa kiutendaji wakimazoea bali kuboresha huduma kwa jamii.kumarisha wawapo vituoni mwao na kuwafanya wananchi kuona kuwa vituo vya Polsi ni kimbilio la watafuta haki.
Amesema Kamanda Kashai jukumu la kuwafundisha askari ni la kila Afisa wa polisi, il askari wawe waadifu katika utendaji kazi wao na kuwaudumia wananchi wanapokwenda katika kituo cha Polisi anatarajiwa kupata huduma anayoitegemea na kwamba kama atakuwa na tatizo anaamini atapata mapokezi mazuri na kutatuliwa tatizo lake.
Kamanda Kashai amesema kutokana na mabadiliko ya mifumo ya Majeshi ya Polisi Duniani Kote, Polisi anatakiwa kumuona Raia kama sehemu ya Polisi kwani ni Raia huyo huyo atalazimika kutoa taarifa za wahalifu Polisi na hivyo kurahisisha utendaji wa Jeshi zima.sambamba na hilo ataendelea kufundisha askari kila juma tano ili kuwa na askari wazuri katika Mkoa wa Kigoma amewataka askari wote kunza siri za watoa taarifa ili kulifanya Taifa letu kuwa na amani iliyopo iendelee
Kamanda alisema kuwa washiiriki hao watalisaidia Jeshi la Polisi katika kuboresha utendaji wa kazi za Polisi katika maeneo mbalimbali hasa katika kila kata hadi tarafa kuendelea kufundisha polisi jamii katika kila maeneo waoyopangiwa.
Mafunzo hayo yanayo tolewa mala moja kwa kila wiki moja yanawashirikisha Wakuu wa Vituo vya Polisi 18 na Askari 132 wa Vyumba vya Mashtaka kutoka vituo mbalimbali vya Polisi katika Wilaya zote tatu Kigoma mjini Kasulu,na Kibondo.

No comments:

Post a Comment