TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Sunday, May 27, 2012

Idadi ya abiria ATCL yazidi kupaa

Na Mwandishi Wetu.
IDADI ya abiria wa Shirika la ndege la Air Tanzania (ATCL) imezidi kuongezeka kila kukicha kutokana na wananchi kuonyesha uzalendo na imani kwa kampuni hiyo , Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa ATCL Paul Chizi amesema.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa waandishi wa habari jana Chizi alisema kutokana na imani hiyo, kampuni yake imejizatiti kuleta mabadiriko makubwa katika sekta ya usafiri wa anga kupitia mpango  wa maendeleo wa miaka mitano wa shirika hilo.
Chizi alisema tangu uzinduzi wa safari za Dar es Salaam-Kilimanjaro-Mwanza wiki moja iliyopita kwa kutumia ndege ya aina ya Boeing 737-500,kampuni yake imekuwa ikijaza abiria takribani 106 katika kila safari kwa siku tatu mfulilizo ikiwemo na siku ya jana hali ambayo inaashiria kuwa wananchi wameanza kuwa na imani na huduma zinazotolewa na shirika lake.
 “Ndege yetu kwa takribani siku tatu zilizopita imekuwa ikija katika safari zote za Dar es Salaam-Kilimanjaro-Mwanza . Sikujua kuwa tutakuwa na uwezo wa kurejea na kupata mapokezi ya namna hii kwa haraka kutokana na kuwa kuna watoa huduma wengine katika njia hii .
 “Baada ya wananchi kuonyesha imani na uzalendo,tutaendelea na kuongeza nguvu zetu katika kutoa huduma zetu kwa wakati na kwa bei nafuu. Nawaomba wananchi kuendelea na uzalendo wanaouonyesha kwa faida ya kampuni yetu na nchi nzima kwa ujumla,” alisema.
Chizi alisema kuwa mipango ya kampuni hiyo ya kupata ndege nyingine ambayo itatumika katika safari za kimataifa katika miezi mitatu mpaka sita ijayo inaenda vizuri na kuongeza kuwa kampuni itatoa taarifa kamili wakati muafaka utakapofika.
“Kutokana ukweli kuwa tunatarajia kuanza safari za kimataifa, ni dhahiri kuwa ndege ambayo  tunategemea kuleta lazima iwe kubwa,” aliongeza.
Alisema kuwa kampuni yake kwa sasa imejikita katika utekelezaji wa mpango wake wa maendeleo wa miaka mitano utakaosaidia kuongeza ubora katika kampuni hiyo na kuboresha utoaji huduma kwa ujumla.
“Tutajikita katika kuongeza ubora wa huduma tunazozitoa na vilevile kuchukua nafasi ile tuliyoipoteza hapo nyuma. Tunamatarajio ya kupata ndege nyingine ya Boeing na mazungumzo yameshaanza na tumefikia pazuri,” alisema.
Kurudi kwa huduma za ndege ya ATCL kumeanzisha  vita ya viwango vya bei za usafiri wa anga bada ya ATCL kutoza bei ya shilingi 199,00 kwa safari zake kwenda na kurudi (return ticket) na kusababisha watoa huduma wengine wakiwemo Precision Air nao kupunguza gharama zao ile ilikukabiriana na ATCL.

No comments:

Post a Comment