TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Sunday, May 27, 2012

TAARIFA YA KUKAMATWA KWA MADAWA YA KULEVYA AINA YA BANGI MAGUNIA 50 NA WATUHUMIWA WANNE MKOANI ARUSHA

Mkuu wa kitengo cha kuzuia na kudhibiti madawa ya kulevya Mkoa wa Arusha Mrakibu wa Polisi Hamis Warioba akiwaonyesha waandishi wa habari shehena ya mifuko 50 ya bangi iliyokuwa kwenye gari baada ya kukamatwa tarehe 23/05/2012 wilayani Longido (PICHA NA GLADNESS MUSHI -ARUSHA)
Mkuu wa kitengo cha kuzuia na kudhibiti madawa ya kulevya Mkoa wa Arusha Mrakibu wa Polisi Hamis Warioba akihoji jambo kwa watuhumiwa hao.
MNAMO TAREHE 23/05/2012 MUDA WA SAA 9:00 ALASIRI HUKO SINYA VILIMA SABA MPAKANI MWA KENYA NA TANZANIA KATIKA WILAYA YA LONGIDO, ASKARI WA JESHI LA POLISI MKOANI HAPA KWA KUSHIRIKIANA NA ASKARI WA WANYAMA PORI WALIFANIKIWA KUKAMATA WATU WANNE WAKIWA NA MIFUKO 50 YA MADAWA YA KULEVYA AINA YA BANGI KWENYE GARI AINA YA CANTER DCM LENYE NAMBA ZA USAJILI T.922 AFJ MALI YA ZEPHANIA S/O KAMBEI MKAZI WA NGARAMTONI.
MADAWA HAYO YALIKUWA YANASAFIRISHWA KUTOKA KATIKA VIJIJI VILIVYOPO KANDO YA KANDO YA MLIMA MERU KUELEKEA NAIROBI NCHINI KENYA KUPITIA NJIA ISIYO RASMI (MAARUFU KAMA NJIA YA PANYA) ILIYOPO HUKO SINYA VILIMA SABA, NA BAADA YA KUONA HIVYO RAIA WEMA WALITOA TAARIFA KWA ASKARI HAO NA HATIMAYE KUFANIKIWA KUWAKAMATA.
WATUHUMIWA WALIOKAMATWA KATIKA TUKIO HILO NI BABUU S/O LAIZER (34) MKULIMA, MKAZI WA OLDONYOSAMBU,LOMNYAKI S/O LEKIBENGI (30) MKULIMA , MKAZI WA OLDONYOSAMBU, JOHN S/O JOSHUA AMBAYE NI UTINGO NA NI MKAZI WA OLDONYOSAMBU NA EDWARD S/O MOLLEL (27) DEREVA NA NI MKAZI  WA OLDONYOSAMBU.
BADO JESHI LA POLISI MKOANI HAPA LINAENDELEA KUWAHOJI WATUHUMIWA HAO ILI KUBAINI WAHUSIKA WENGINE NA PINDI UPELELEZI UTAKAPOKAMILIKA  WATAFIKISHWA MAHAKAMANI.
IMETOLEWA NA KAMANDA WA POLISI MKOA WA ARUSHA,
KAMISHNA MSAIDIZI MWANDAMIZI WA POLISI
(SACP) THOBIAS ANDENGENYE
TAREHE 25/05/2012.

No comments:

Post a Comment