Kamati
 ya Sheria, Maadili na Hadhi za Wachezaji ya Shirikisho la Mpira wa 
Miguu Tanzania (TFF) ilikutana Mei 26 mwaka huu ili kutoa mwongozo wa 
nini kifanyike ndani ya Yanga baada ya wajumbe wake kudhaa kujiuzulu. 
Kamati ya Uchaguzi ya Yanga ilikuwa imeomba mwongozo huo TFF.
Baada
 ya kupata taarifa rasmi kutoka Yanga, Kamati imebaini kuwa Kamati ya 
Utendaji ya Yanga imekosa akidi baada ya wajumbe wake wengi kujiuzulu 
hivyo kutokuwa na uwezo wa kufanya uamuzi kwa mujibu wa Ibara ya 32(1) 
ya Katiba ya klabu hiyo.
Hivyo,
 Kamati imetoa mwongozo kwa Kamati ya Uchaguzi ya TFF ambayo ndiyo 
msimamizi wa Kamati ya Uchaguzi ya Yanga kuwa ili Kamati ya Utendaji ya 
Yanga iwe na nguvu za kikatiba kufanya shughuli zake ikiwemo uamuzi wa 
masuala mbalimbali ndani ya klabu hiyo ni lazima iwe na akidi.
Kwa
 mujibu wa Ibara ya 29(3) ya Katiba ya Yanga nafasi zilizo wazi katika 
Kamati ya Utendaji zinatakiwa kujazwa katika Mkutano Mkuu wa Kawaida 
ujao.
Pia
 Kamati imebaini uteuzi wa kujaza nafasi zilizo wazi za wajumbe 
uliofanywa na Kamati ya Utendaji ya Yanga, Mei 21 mwaka huu ni batili 
kwa vile Kamati ya Utendaji iliyofanya uteuzi huo haikuwa na akidi. 
Ili
 kupata akidi na kufanya uamuzi Kamati ya Utendaji ya Yanga yenye 
wajumbe 13 inatakiwa kuwa na asilimia 50 ya wajumbe wote, hivyo ili 
wafanye uamuzi halali hawatakiwi kupungua saba. 
Kwa
 wajumbe ambao hawajajiuzulu; Sarah Ramadhan, Mohamed Bhinda, Tito Osoro
 na Salim Rupia kwa sasa hawawezi kufanya shughuli zozote za Yanga hadi 
nafasi zilizo wazi katika Kamati ya Utendaji zitakapojazwa.
Kama
 inavyoelekeza Katiba ya Yanga, shughuli za kila siku za klabu hiyo 
zitaendelea kufanywa na Sekretarieti ya Yanga ambayo kiongozi wake ni 
Katibu Mkuu.
Alex Mgongolwa
Mwenyekiti
Kamati ya Sheria, Maadili na Hadhi za Wachezaji
No comments:
Post a Comment