Na Juma Mohammed,MAELEZO Zanzibar
Waziri
 wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Dk. Emmanuel Nchimbi ametua Visiwani Zanzibar
 leo ambapo amekemea vitendo vya vurugu,akiahidi Serikali kuwachukulia 
hatua ikibidi hata kuwavizia nje ya misikiti kwa wale watakaohusika na 
uvunjifu wa amani .
Waziri Nchi aliwasili Mjini Zanzibar akiwa na Mkuu wa Jeshi  la
 Polisi,Inspekta Jenerali Said Mwema kwa pamoja waliitisha mkutano 
uliowakutanisha viongozi wa Jumuiya ya Maimamu 
Zanzibar(JUMAZA),Mabalozi, Kamisheni ya Utalii, Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislam Zanzibar(JUMIKI).
“Suala
 la kufuata sheria halina mjadala,lazima kila mmoja wetu afuate na kutii
 sheria hatutawavumilia watakaovuruga amani ya nchi…maandamano yoyote 
lazima yapate kibali” Aliwaambia wadau katika mkutano huo uliofanyika 
Makao Makuu ya Polisi Zanzibar,Ziwani.
Waziri
 Nchi alisema busara ya Polisi imefikia kikomo na kwamba atashangaa sana
 akiona busara hiyo ikiendelea wakati kuna watu au kikundi kinavunja 
amani ya nchi.
“Tutashangaa
 busara ya Polisi ikiendelea wakati watu wanaumia kwa watu wengine 
kuvunja amani…hatutakubali, tutaendelea kuviziana hata nje ya misikiti 
tutawakamata” Alisisitiza Waziri Nchi.
Waziri
 huyo alisema kila mtu anawajibika kitunza amani iliyopo ambapo pia 
alisema Serikali ya Mapinduzi Zanzibar yenye mfumo wa Umoja wa Kitaifa 
imefanyakazi nzuri katika kipindi kifupi na kuwapongeza Rais wa Zanzibar
 na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,Dk. Ali Mohammed Shein, Makamu wa 
Kwanza wa Rais Maalim Seif Shariff Hamad na Makamu wa Pili wa Rais 
Balozi Seif Ali Idd.
.jpg)
No comments:
Post a Comment