TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Sunday, January 11, 2015

WAMA yajivunia mafanikio katika sekta ya elimu

index
Taasisi ya WAMA Foundation imefanikiwa kupanua fursa za elimu kwa mtoto wa kike kwa mwaka 2014.
Hayo yamesemwa na Mke wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Salma Kikwete wakati Akiongea na wenza wa mabalozi kutoka nchi mbalimbali katika ghafla fupi ya kuukaribisha mwaka mpya 2015 iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam,
Mama Salma alisema kuwa baadhi ya mafanikio yaliyofikiwa na Taasisi ya WAMA ni kukamilika kwa sekondari ya WAMA Sharaf  katika Manispaa ya Lindi.
“Ninayo furaha kuwataarifu kwamba ujenzi wa shule ya sekondari ya WAMA Sharaf umekamilika, shule ambayo itaongeza idadi ya wasichana wanaofaidika na WAMA” Alisema Mama Salma.
Aidha, aliitaja Shule ya Sekondari ya Wasichana ya WAMA Nakayama kuwa sehemu ya mafanikio ya Tasisi hiyo ambayo ina idadi ya wanafaunzi zaidi ya 400 na inatarajia kuchukua wanafunzi 90 mwaka 2015, ambao ni yatima na wanaotoka kwenye mazingira magumu.
Akiongelea kuhusu mafanikio mengine Mama Salma alisema ni pamoja na kuimarisha afya ya mama wajawazito na watoto ili kupunguza vifo, kupunguza mimba za utotoni, na kupunguza kasi ya maambukizi ya HIV toka kwa mama kwenda kwa mtoto
Mama Salma aliwashukuru wadau wote wanaofanya kazi kwa kushirikiana na WAMA wakiwemo Mashirika yasiyo ya Serikali kwa misaada na kuwaomba waendelee kushirikiana ili kutoa mabadiliko chanya katika jamii husika.
Aidha, kwa niaba ya wenza wa mabalozi waliohudhuria ghafla hiyo, Mke wa kiongozi wa mabalozi nchini Bi Celine Mpango alimpongeza Mama Salma Kikwete kwa juhudi anazofanya katika kumkomboa mtoto wa kike na mwanamke kwa ujumla.

No comments:

Post a Comment