TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Wednesday, February 25, 2015

Warioba: Ipo siku maadili yataingizwa kwenye Katiba

Mwenyekiti wa iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba 
Na Fidelis Butahe, Mwananchi
  • Amesema sheria ya maadili ya viongozi wa umma haina nguvu ya kukabiliana na mmomonyoko huo na  inakosa meno kwa sababu inasimamiwa na watu walewale wasiotaka ‘kuguswa’.

Akigusia suala la maadili na sakata la mabilioni ya fedha yaliyochotwa katika Akaunti ya Tegeta Escrow alisema, “Katika suala la escrow niliuliza nani msafi…, we subiri tu si tunakwenda katika uchaguzi mkuu viongozi watakuwa na fedha nyingi sana.”
Kura ya maoni isubiri 2016
Akizungumzia daftari wa wapigakura na upigaji wa Kura ya Maoni kupitisha Katiba Inayopendekezwa, alisema, “Nia ya kupitisha Katiba mpya mapema ilikuwa na lengo la kuitumia katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba, lakini inahitaji maandalizi. Mfano Katiba Inayopendekezwa ina sehemu ya Tume ya Uchaguzi na kama ukiipitisha, utaunda upya tume hiyo na suala hilo linahitaji muda.”
Alisema ili kufanikisha uundwaji wa tume hiyo ni lazima Bunge likutane, lakini mpaka itakapofika siku ya kuipigia kura Katiba hiyo na kuipitisha, Bunge litakuwa limekwishakaa na hakutakuwa na uwezekano wa kubadili lolote.
“Hakuna haja ya kuharakisha, ni vizuri twende taratibu ili tusije tukafanya makosa ambayo yatatuletea matatizo,” alisema.
Aliongeza, “Itakuwa vizuri kama kura ya maoni ikasitishwa mpaka mwaka 2016. Inaonekana tutalazimika kusubiri na hii inatokana na matatizo tu ya kawaida ya kutokuwa na daftari la Wapigakura.
Mgongano wa maslahi
Jaji Warioba pia aligusia kitendo cha wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba kuruhusiwa kugombea nafasi za kisiasa baada ya kumalizika kwa Bunge hilo, akisema kuwa hilo lilikuwa kosa kubwa.
“Uganda tume ilipomaliza kazi, wananchi walichagua Bunge la Katiba na sharti moja ni kwamba ukiingia katika Bunge hilo hauruhusiwi kugombea uongozi. Walijua kazi yao ni kupitisha Katiba tu,” alisema.
Alisema kosa lililofanyika nchini ni kuruhusu wabunge waliopitisha Katiba kugombea, hivyo kuwafanya baadhi kuondoa masuala ya msingi waliyoona kuwa ni kikwazo kwao katika uchaguzi.
“Nadhani hiyo ni kasoro tuliyokuwa nayo na tulipeleka watu ambao wana malengo na Katiba kwa manufaa yao binafsi,” alisema.
Kuhusu maridhiano kuelekea upigaji wa Kura ya Maoni alisema, “Suala la maridhiano lilipofika kwenye vyama vya siasa likabadilika na sasa tunazungumzia maridhiano ya vyama vya siasa. Maridhiano ya vyama vya siasa siyo lazima yawe maridhiano ya wananchi.”

No comments:

Post a Comment