TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Monday, February 23, 2015

WAZIRI MKUU AAHIDI BWAWA LA KUTUNZIA MAJI NYANZWA

indexWAZIRI MKUU Mizengo Pinda amesema anakubaliana na ombi la wakazi wa Nyanzwa na Igunda wilayani Kilolo, mkoani Iringa kuhusu ujenzi wa bwawa la kuhifadhia maji yatakayovunwa msimu wa mvua ili yasaidie kuongeza eneo la mradi wa umwagiliaji.
Ametoa kauli hiyo mwishoni mwa wiki wakati akiwahutubia wakazi wa vijiji vya Nyanzwa na Igunda, mara baada ya kukagua mradi wa umwagiliaji wa Nyanzwa ambao ni maarufu kwa kilimo cha vitunguu.
“Huu mradi ni wa siku nyingi. Nimewauliza wataalamu niliokwenda nao wakasema ujenzi wa bwawa ndiyo suluhisho pekee la kuokoa mradi huu na kwamba ni jambo linalowezekana kama fedha zipo.”
Aliutaka uongozi wa mkoa uandae mpango kazi na wauweke kwenye bajeti ya mwaka ujao wa fedha ili mradi huo uweze kuombewa fedha kwenye bajeti kuu ya Serikali.  ia aliwataka wakazi wa eneo hilo wakitunze chanzo cha maji kwa kuweka mipaka ili watu wasikivamie na hatimaye kukiharibu.

“Tengeni eneo kwa kuweka mipaka. Mkurugenzi simamia uwekaji wa mipaka kwenye chanzo hiki ili tukilinde kwani uharibifu wa mazingira utakiharibu kabisa,” alisisitiza.
Akiwa katika ukaguzi wa eneo la mradi, Waziri Mkuu alikutana na mkulima mmoja wa vitunguu Bw. Furaha Ngalali (32) ambaye alimweleza kwamba mwaka jana alifanikiwa kulima ekari tatu za vitunguu ambazo zilimpatia kiasi cha milioni 6/- huku kila gunia akiwa ameliuza kwa sh. 70,000/-.
“Gharama kwa kila ekari ni karibu sh. 600,000/- kwa hiyo kwa ekari tatu ni sh. milioni 1.8/-. Tukivuna vitunguu tunaandaa bustani ya mbegu na pia humu tunapanda maharage,” alisema Bw. Ngalali alpoulizwa Waziri Mkuu analima eneo hilo mara ngapi kwa mwaka.
Alipoulizwa soko la vitunguu wanapata wapi, Bw. Ngalali alisema wanunuzi huwa wanavifuata huko huko Nyanzwa na kwamba wengi wao hutoka Dar es Salaam, Mbeya na Songea. Kijiji cha Nyanzwa kipo umbali wa kilometa 36 kutoka Ruaha Mbuyuni ilipo barabara kuu ya kuelekea Dar es Salaam na Mbeya.
Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amewataka wakazi wa vijiji vya Nyanzwa na Igunda wajikite kwenye ufugaji wa nyuki kwani hauna gharama kubwa na unawawezesha wananchi kuinua kipato chao kwa haraka.
“Wakati mkisubiri ujenzi wa bwawa ili muongeze uzalishaji wa mbogamboga ni vema mkaangalia suala la ufugaji nyuki… licha ya kutumika kama sehemu ya kujiingizia kipato, pia ufugaji nyuki ni njia mojawapo ya utunzaji wa misitu,” alisema.
“Hapa mlipo kuna msitu mkubwa wenye migunga na mibuyu mingi tu. Yote hii imechanua maua mengi mno. Lazima tutumie uwepo wa misitu hii kama fursa ya kipekee ya kujiingizia kipato kwa kuweka mizinga ya nyuki. Unaweza usipate mahindi au vitunguu lakini asali ikawasaidia kuwapa kipato. Hivi sasa lita moja ya asali imefikia sh. 15,000/- hadi sh. 20,000/- na tena mtapata nta ambayo pia ina bei nzuri tu,” alisema.
Alisema kwa sasa asali inauzwa kwa bei ghali kwenye nchi mbalimbali baada ya kuongezeka kwa mahitaji yake na hasa ikizingatiwa kwamba inatumika kama dawa ya kutibu magonjwa mbalimbali na pia kwenye baadhi ya vipodozi.
Mapema, akisoma taarifa mbele ya Waziri Mkuu, Mtendaji wa Kijiji cha Nyanzwa, Bw. Hekima Masanula alisema skimu ya umwagiliaji ya Nyanzwa ilijengwa mwaka 1960 wakati huo kwa kutumia banio la miti na magunia ya mchanga. Ilikuja kuboreshwa miaka ya 90 kwa ufadhili kutoka Jumuiya ya Ulaya na Serikali ya Sweden.
“Hata hivyo, skimu hii ambayo inahudumia wakulima 3,469 wakiwemo wanaume 1,662 na wanawake 1,807; inakabiliwa na uhaba wa maji kwani ni hekta 256 tu ambazo zinamwagiliwa kwa sasa wakati eneo lote la mradi ni hekta 940,” alisema Bw. Masanula.
Alisisitiza ombi la kujengewa bwawa kama njia pekee ya kuwakwamua wakazi hao kutokanana shida ya maji inayowapata hasa wakati wa kiangazi.

No comments:

Post a Comment