Viongozi
 wa kampuni ya saruji ya Lafarge wakiwa pamoja na watendaji wa 
Halmashauri ya Jiji la Mbeya wakati wa kukabidhi mifuko 1,000 ya saruji 
kwa ajili ya mabweni yaliyoteketea ya shule ya Sekondari Iyunga.
Kaimu
 Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Mbeya Dkt. Samwel Lazaro(kushoto) 
akipokea mifuko 1000 ya saruji kutoka kwa Meneja Uajiri watu wa kampuni 
ya saruji ya Lafarge Bryson Tarimo kwa ajili ujenzi wa mabweni ya shule 
ya Iyunga yaliyoteketea kwa moto hivi karibuni.
Meneja
 Rasilimali Watu wa kampuni ya saruji ya Lafarge ya jijini Mbeya Bryson 
Tarimo akizungumza mara baada ya kukabidhi mifuko 1,000 ya saruji kwa 
ajili ya ujenzi wa mabweni ya shule ya Sekondari Iyunga ambayo hivi 
karibuni yaliteketea kwa moto,Kampuni ya Lafarge imetoa mifuko ya saruji
 yenye thamani ya shilingi milioni 14.
Mkuu
 wa shule ya sekondari ya Iyunga Edward Mwantimo akitoa neno la shukrani
 mara baada ya kukabidhiwa mifuko 1,000 ya saruji kutoka kampuni ya 
Lafarge ya jijini Mbeya kwa ajili ya ujenzi wa mabweni ya shule ya 
Sekondari Iyunga ambayo hivi karibuni yaliteketea kwa moto ambapo pia 
alielezea madhara yaliyotokana na moto uliosababisha kuungua kwa mabweni
 ya wanafunzi wa shule hiyo.
 Kampuni
 ya Saruji ya Lafarge Tanzania (Mbeya Cement Company) imetoa msaada wa 
zaidi ya mifuko 1,000 ya saruji na vifaa vingine vya ujenzi kwa shule ya
 Sekondari ya Iyunga mkoani Mbeya kufuatia mabweni ya shule hiyo kuungua
 moto hivi karibuni.
Mashine
 ya kampuni hiyo pia itatumika kufyatua zaidi ya matofali 40, 000 
yanayohitajika kukamilisha ujenzi huo na kufanya jumla ya msaada huo 
kuwa na thamani ya shilingi 14 milioni. Akizungumza kwenye makabidhiano 
ya msaada huo, Meneja Rasilimali Watu wa Lafarge Tanzania, Bryson Tarimo
 alisema “tulipata habari za kushtusha kuhusiana na tukio la moto ambao 
uliteketeza miundombinu ya shule pamoja na mali za wanafunzi. 
Tunatambua
 kwamba huu umekuwa ni wakati mgumu kwa uongozi wa shule pamoja na 
wanafunzi.” Aliongeza kusema kwamba Lafarge inaamini kwamba elimu ni 
muhimu kwa maendeleo ya mustakabali wa Tanzania na pia kwamba elimu 
itasaidia kufungua mianya ya fursa mbalimbali kwa Watanzania. Tarimo 
alieleza kwamba Lafarge ina jukumu la kujenga mabweni hayo ili 
kuwarudishia wanafunzi wa Sekondari ya Iyunga mazingira mazuri ya 
kujisomea. “Hii ni sehemu ya jukumu letu kuifikia jamii na kuisaidia 
jamii pamoja na taasisi mbalimbali zilizopo mahali tunapofanyia kazi.”
 Aliongeza:
 “Uhusiano wetu na shule hii ni mkubwa sana kwa sababu tunaelewa 
imewafundisha baadhi ya watu ambao hivi sasa wanaendesha kiwanda chetu 
na kutufanya tuendelee kuwa na mafanikio. Tunataka kuona wanafunzi 
wakirejea madarasani na walimu wakiendelea kutimiza majukumu yao kama 
kawaida kwani azma yetu ni kuona shule hii inapata mafanikio na kuwapa 
wanafunzi fursa ya kutimiza ndoto zao na kuwa na mustakabali mzuri. 
Mtazamo
 wetu ni kuona Tanzania ikiwa nchi inayotoa fursa ya elimu kwa kila 
mtoto ili watoto hawa wote kila mmoj aweze siku moja kuchangia maendeleo
 ya nchi hii.” Tarimo alisema kwamba Lafarge inajali maendeleo ya jamii 
na ina fahari kuweza kutoa msaada huu kwa shule ya Sekondari ya Iyunga 
kufuatia moto ulioteketeza mabweni ya shule hiyo. 
Tunaamini
 msaada huu utarejesha hali ya kawaida katika shule hii na sisi kama 
sehemu ya jamii hii tunapenda kuona wanafunzi hawa wakiishi katika 
mazingira salama.” Tarimo aliyaomba makampuni mengine na taasisi 
mbalimbali, watu binafsi na jamii kwa ujumla kuisaidia ujenzi wa shule 
hiyo.
No comments:
Post a Comment