Mkurugenzi Mkuu mstaafu wa Mfuko wa
Taifa wa Bima ya Afya,Emmanuel Humba akiongea na waandishi wa habari (hawapo
pichani).
Na Jacquiline Mrisho -MAELEZO
Mkurugenzi wa Mfuko wa Afya ya Jamii
akiongea na waandishi wa habari kuhusu kikao cha wanachama wastaafu wa Mfuko wa
Taifa wa Bima ya Afya.
Na Jacquiline Mrisho -MAELEZO
Mfuko
 wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) umewataka wanachama wastaafu 
wanaohudumiwa na mfuko huo kutoa maoni na ushauri wa namna ya kuboresha 
huduma zitolewazo kwa ajili yao.
Hayo
 yamesemwa leo Jijini Dar es salaam na Mkurugenzi wa Mfuko wa Afya ya 
Jamii Bw.Eugin Mikongoti alipokua akiongea na wanachama wastaafu katika 
mkutano ulioandaliwa na NHIF.
“Hatukuwahi
 kuwa na mkutano maalumu wa wanachama wastaafu,ndiyo maana mkutano huu 
kwetu ni wa kihistoria na tunaamini ni muhimu kukutana na wastaafu peke 
yao ili kutoka kwao tusikie, siyo tu huduma nzuri wanazozipata bali pia 
changamoto wanazozikabili ili kwa pamoja tuweke mkakati wa 
kuzitatua”alisema Mikongoti.
Bw.
 Mikongoti ameongeza kuwa, wakati wote wamekua wakipokea na kuzingatia 
ushauri na maoni ya wadau wake wote, kwahiyo wanatarajia mkutano huu na 
wanachama wastaafu utakua ni uwanja mzuri wa kubadilishana mawazo na 
kupata ushauri wa namna ya kuboresha zaidi huduma zao.
Aidha,Mwenyekiti
 wa kikao cha wastaafu,George Yambesi amewasihi wastaafu wenzie 
wafuatilie kwa makini na waulize maswali kwa kadiri watakavyoweza ili 
wawe na uelewa mpana kuhusu huduma za mfuko wa NHIF kwakua hii ndio 
fursa yao maana  hawapo kwenye ajira na hivyo sio rahisi kupata taarifa 
za mara kwa mara.
Pia
 Bw. Yambesi kwa niaba ya wenzake ameipongeza Serikali  kwa kuufanya 
Mfuko huu kutoa huduma za matibabu kwa wastaafu pia amewashukuru 
viongozi waasisi wa Mfuko kwa kuweka misingi bora ya kuwashughulikia 
wastaafu bila kukata tamaa.
Naye
 mmoja wa wastaafu kutoka Shirika la Utangazaji la Taifa Ngalinecha 
Ngahyoma anaishukuru NHIF kwa kuwasaidia wastaafu kupata matibabu maana 
gharama za matibabu ni kubwa bila kuwa na bima za afya wastaafu 
wasingeweza kulipia huduma hizo.


No comments:
Post a Comment