TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Thursday, March 17, 2016

MBUNGE WA ILEMELA AWAITA WAKAZI WA MWANZA NDANI YA TAMASHA LA PASAKA

MBUNGE wa Ilemela, Angelina Mabula ametoa wito kwa wakazi wa jiji la Mwanza na maeneo ya karibu kujitokeza kwa wingi kwa sababu ya unyeti wa Tamasha la Pasaka linalotarajia kufanyika Machi 27 kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.

Akizungumza jana, Mabula alisema Tamasha la Pasaka ni la Watanzania wote, lakini mwaka huu wamepata bahati ya kufikiwa na ujumbe wa neno la Mungu ambao utakemea maovu kama mauaji ya vikongwe na walemavu wa ngozi 'albino'.

"Binaadam anatakiwa kubaki na heshima yake, kwani hakuna maisha bora ambayo yanatokana na kuwaua na kuwakata viungo wenzao, si ubinaadam kabisa tunatakiwa tumrudie Mungu kwani ndio kimbilio," alisema Mabula.Mabula alisema Tamasha la Pasaka limebeba ujumbe wa neno la Mungu hivyo ni nafasi kwa wakazi wa Ilemela na maeneo ya jirani na hata mikoa mingine kujitokeza kwa wingi kufanikisha tamasha hilo.

Aidha Mabula alisema thamani ya Tamasha la Pasaka ni kubwa hivyo Watanzania ni nafasi yetu Watanzania kumfikishia Mungu sala zetu.Naye Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Tamasha la Pasaka, Alex Msama alisema maandalizi ya kuelekea tamasha hilo yanaendelea vizuri, hivyo wakazi wa mikoa ya Kanda ya Ziwa wakae mkao wa kula.

Msama alisema Tamasha la Pasaka litaanza Machi 26 mkoani Geita na kufuatiwa jijini Mwanza Machi 27 na kumalizia Machi 28 mjini Kahama

No comments:

Post a Comment