MBUNGE
 wa Ilemela, Angelina Mabula ametoa wito kwa wakazi wa jiji la Mwanza na
 maeneo ya karibu kujitokeza kwa wingi kwa sababu ya unyeti wa Tamasha 
la Pasaka linalotarajia kufanyika Machi 27 kwenye uwanja wa CCM Kirumba 
jijini Mwanza.
Akizungumza
 jana, Mabula alisema Tamasha la Pasaka ni la Watanzania wote, lakini 
mwaka huu wamepata bahati ya kufikiwa na ujumbe wa neno la Mungu ambao 
utakemea maovu kama mauaji ya vikongwe na walemavu wa ngozi 'albino'.
"Binaadam
 anatakiwa kubaki na heshima yake, kwani hakuna maisha bora ambayo 
yanatokana na kuwaua na kuwakata viungo wenzao, si ubinaadam kabisa 
tunatakiwa tumrudie Mungu kwani ndio kimbilio," alisema Mabula.Mabula 
alisema Tamasha la Pasaka limebeba ujumbe wa neno la Mungu hivyo ni 
nafasi kwa wakazi wa Ilemela na maeneo ya jirani na hata mikoa mingine 
kujitokeza kwa wingi kufanikisha tamasha hilo.
Aidha 
Mabula alisema thamani ya Tamasha la Pasaka ni kubwa hivyo Watanzania ni
 nafasi yetu Watanzania kumfikishia Mungu sala zetu.Naye Mwenyekiti wa 
Kamati ya Maandalizi ya Tamasha la Pasaka, Alex Msama  alisema 
maandalizi ya kuelekea tamasha hilo yanaendelea vizuri, hivyo wakazi wa 
mikoa ya Kanda ya Ziwa wakae mkao wa kula.
No comments:
Post a Comment