Lundega akifafanua jambo kwa umakini mbele ya Wanahabari (hawapo pichani).
Lundenga
 amesema kuwa katika uzinduzi wa msimu huo mpya,utawakutanisha wadau 
mbalimbali wa tasnia ya Urembo  wakiwemo Wabunifu wa Mavazi,Mawakala 
wanaoandaa mashindano ya Miss Tanzania katika ngazi mbalimbali hapa 
nchini.kama vile haitoshi Lundenga alibainisha kuwa pia Wakurugenzi wa 
makampuni mbalimbali ambao miongoni mwao wanatarajia kuwa Wadhamini wa 
shindano hilo kwa mwaka huu.
Katika
 kunogesha uzinduzi huo utakaokuwa wa aina yake,Lundemga amesema kuwa 
burudani kadhaa zitakuwepo akiwemo msanii wa kizazi kipya Linah Sanga 
pamoja na msanii wa ngoma za asili Wanne Star.
Lundenga
 alisema kuwa mara baada ya uzinduzi huo kufanyika jijini Dar,utahamia 
mkoa wa Arusha ambako pia kutakuwa na aina nyingine ya uzinduzi," 
Uzinduzi huo ukikamilika itafuata ratiba ya semina ya mawakala na kuanza
 kwa mashindano ya urembo katika ngazi za vituo,Wilaya,Mikoa na 
Kanda",alisema Lundenga.
Amesema
 kuwa mpaka sasa Wadhamini kadhaa wamejitokeza na kuonesha nia ya kutaka
 kudhamini shindano hilo katika ngazi ya Taifa.Lundenga ameyataja 
makampuni ambayo yamedhamini uzinduzi huo wa shindano la urembo la Miss 
Tanzania 2016 kuwa ni Ramada Resort Dar,Naf Beach hotel Mtwara,Kitwe 
General Trader,CXC Africa,MMI Tanzania,Mwandago Investment Ltd,Break 
Point pamoja na GSM Media. 
No comments:
Post a Comment