TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Saturday, March 7, 2015

Gharama za kuunganisha umeme shilingi 177,000. Atakayetoza zaidi ya hapo kufikishwa polisi – Ndassa

NDA1\Meneja Miradi kutoka Shirika la Umeme Nchini (Tanesco) Mhandisi Khalid James (kulia) akiieleza Kamati ya   Bunge ya Nishati na Madini hatua iliyofikiwa ya   ujenzi wa miundombinu ya umeme katika   mikoa ya Iringa, Dodoma, Singida hadi   Shinyanga inayosimamiwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) Awamu ya Pili. Kamati ya Bunge inafanya ziara katika mikoa ya Dodoma, Singida, Arusha na Kilimanjaro kwa ajili ya kukagua miradi ya umeme   ili kujionea maendeleo yake pamoja na kuzungumza na wananchi
NDA2Meneja Miradi kutoka Shirika la Umeme Nchini (Tanesco) Mhandisi Khalid James (katikati) akitoa maelezo mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kuhusu maendeleo ya ujenzi wa njia kuu za umeme unaofanywa na kampuni ya Jyoti Structures Limited kutoka India katika eneo la Nara mkoani Dodoma
………………………………………………………………………….

Na Greyson Mwase, Bahi – Dodoma
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini , Richard Ndassa amewaambia wakazi wa kata ya Ibihwa iliyopo Bahi mkoani Dodoma kuwa gharama za kuuunganishiwa huduma ya umeme zimeshuka hadi shilingi 177,000 na iwapo ikatokea wakatozwa zaidi ya kiwango hicho, na watumishi wasio waaminifu basi wana haki ya kumfikisha mbele ya vyombo vya kisheria.
Ndassa alisema hayo wakati Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini ilipotembelea wilaya ya Bahi kwa ajili ya kukagua miradi ya umeme pamoja na kuzungumza na wananchi.
Ndassa alisema kuwa Serikali imekuwa ikijitahidi kupunguza gharama za kuunganishiwa umeme hasa maeneo ya vijijini kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ili kuhakikisha kila mwananchi anapata nishati muhimu na kujiletea maendeleo.
Alisema kuwa kama juhudi ya Serikali katika kuhakikisha kila mwananchi anaondokana na umasikini, Serikali kupitia REA iliamua kupunguza gharama za kuunganishiwa umeme kwa wananchi wanaoishi vijijini ili waweze kupiga hatua kimaendeleo, na kuwataka kuchangamkia fursa hiyo kwa kujiandaa na uwekezaji wa viwanda vidogo vidogo.
Alifafanua kuwa iwapo watatokea watumishi wasio waaminifu na kutaka kuwatoza fedha zaidi ya kiasi kinachotakiwa kulipwa, basi wana wajibu wa kuwafikisha katika vyomvbo vya sheria.
“ Iwapo atatokea mtumishi na kuwatoza gharama zaidi ya ile inayohitajika kulipwa kisheria, basi mna haki ya kumfikisha polisi ili afunguliwe mashtaka,” alisema Ndassa
Aliendelea kusema kuwa umefika wakati wa watanzania kuchangamkia fursa mbalimbali zinazojitokeza mara baada ya kukamilika kwa miradi ya umeme kwani umeme ndio kitovu cha ukuaji wa uchumi katika nchi yoyote.
“ Kuna vijiji ambayo vimeshaanza kunufaika na huduma ya umeme, nawasihi muanzishe viwanda vidogo vidogo vya kukoboa nafaka, kukamua mafuta ya alizeti ili kujiongezea kipato”, alisema Ndassa.
Wakati huo huo akizungumza kwa niaba ya wakazi wa kata hiyo , Mtendaji wa Kata, Jenipha William alisema kuwa katika utekelezaji wa miradi ya umeme ya REA Awamu ya Pili pamekuwepo na changamoto ya vijiji vingine kurukwa hali inayopelekea wananchi wachache kupata umeme.
Alisema kuwa hali hiyo inapelekea baadhi ya vijiji kupiga hatua kubwa kimaendeleo huku vijiji vingine vikibaki gizani
Akifafanua jinsi Shirika la Umeme Nchini (Tanesco) lilivyojipanga kukabiliana na changamoto hiyo mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Meneja wa Tanesco Dodoma, Zakayo Temu alisema kuwa kazi ya kujenga miudombinu ya umeme chini ya REA Awamu ya Pili imekuwa ikifanywa kwa awamu kulingana na fedha na uwiano na mikoa mingine.
Temu alisema ili kukabiliana na changamoto hiyo, shirika limetenga bajeti ya mwaka ujao wa fedha kwa ajili ya vijiji vilivyokosa umeme.

No comments:

Post a Comment