TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Thursday, March 5, 2015

MAANDALIZI YA KUPANDA MLIMA KILIMANJARO-MAAFISA NA ASKARI WA JESHI LA MAGEREZA

MAG1Baadhi ya Maafisa na Askari wa Jeshi la Magereza wakiwa katika mazoezi ya kukimbia katika viunga vya manispaa ya Moshi ikiwa ni maandalizi ya kupanda mlima Kilimanjaro March 6, 2015. Maafisa hao wameweka kambi katika eneo la Gereza Karanga-Moshi.
MAG3Sehemu ya Maafisa na Askari wa Jeshi la Magereza wakiwa katika mazoezi makali katika mitaa ya mji wa Moshi ikiwa ni maandalizi ya kupanda mlima Kilimanjaro ifikapo Machi 6,2015. Katikati (mwenye vazi jeupe) ni Kamishna Msaidizi wa Magereza Alexander Mmasy kutoka Makao Makuu ya Magereza, wa kwanza kulia ni Mrakibu Msaidizi wa Magereza Mbezi Ramadhani kutoka Ofisi ya Mkuu wa Magereza Mkoa wa Tanga na wa kwanza kushoto ni Mkaguzi wa Magereza Jamhuri Yassin kutoka Makao Makuu ya Magereza, Dar es salaam.
MAG4Baadhi ya Maafisa na Askari wa Jeshi la Magereza wakiwa katika mazoezi ya kutembea katika viunga vya Manispaa ya Moshi ikiwa ni maandalizi ya kupanda mlima Kilimanjaro mnamo Machi 6, 2015. Kutoka kushoto ni Mkaguzi wa Magereza Vicent Magessa kutoka Gereza Bagamoyo Mkoa wa Pwani, Mkaguzi wa Magereza Tumaini Kihampa na Mkaguzi wa Magereza Jamhuri Yassin wote kutoka Makao Makuu ya Magereza.
MAG5Maafisa na Askari na baadhi wa watumishi raia wa Jeshi la Magereza wakiwa katika mazoezi makali ya kupita katika njia ngumu ikiwa ni maandalizi ya kupanda mlima Kilimanjaro ifikapo Machi 6, 2015. Wa sita kutoka mbele ni Mhasibu Mkuu wa Jeshi la Magereza Estomiah Hamis na wa mwisho ni Mkaguzi wa Magereza Abas Mikidadi.
MAG6Maafisa na Askari na baadhi wa watumishi raia wa Jeshi la Magereza wakiwa katika mazoezi makali ya kupita katika njia ngumu ikiwa ni maandalizi ya kupanda mlima Kilimanjaro ifikapo Machi 6, 2015.
MAG7Baadhi ya Maafisa na Askari wa Jeshi la Magereza wakiwa katika mazoezi ya viungo baada ya kutembea na kukimbia katika viunga vya Manispaa MAG8Wakipata chakula MAG9Wakipiga picha ya pamoja na baadhi ya watalii.

No comments:

Post a Comment