……………………………………………………………………………
Veronica Simba na Rhoda James
Naibu Waziri wa Nishati na Madini (Madini), Charles Kitwanga
amewataka Maofisa wa Serikali katika sekta ya madini nchini kutumia
kanuni zinazoongoza sekta hiyo kuwabana wachimbaji wadogo wa madini
wanaokwepa kulipa kodi mbalimbali zilizowekwa na Serikali.
Kitwanga ametaka kanuni husika zitumike kuwachukulia hatua kali
wakwepa kodi hao ikiwa ni pamoja na kuwanyang’anya leseni za uchimbaji
madini wanazomiliki.
Aliyasema hayo hivi karibuni alipokutana na Viongozi wa Idara ya
Madini katika Wizara husika hivi karibuni jijini Dar es Salaam kwa
lengo la kuzungumza nao na kujionea utendaji kazi wao.
Akizungumza na Viongozi hao, Kitwanga alisema wachimbaji wadogo
wa madini, kama walivyo wafanyabiashara wengine nchini, wanawajibika
kulipa kodi zote zilizowekwa na Serikali ikiwa ni pamoja na kodi ya
huduma, mrahaba na nyingine ili kuiwezesha Serikali kupata mapato
stahiki kwa lengo la kuwaletea wananchi wake maendeleo.
“Inabidi tujenge nidhamu katika kazi, vinginevyo hatutafika
kwenye uchumi wa kati tunaoutarajia ifikapo mwaka 2025. Kama mtu anakaa
na leseni bila kulipa, tutumie kanuni kumnyang’anya. Kwa mfano, mtu
asipolipa TRA kwa biashara yake, watamwacha kweli?” alisisitiza Naibu
Waziri.
Akifafanua zaidi, Kitwanga alisema ili kupata matokeo chanya
katika kazi yoyote, inabidi kutenda yale yaliyo sahihi na siyo kutenda
mambo kwa usahihi, akitumia msemo maarufu wa lugha ya kiingereza ‘Do the
right thing, don’t do things right.’
“Inapotokea kuna sheria imepitwa na wakati, si sahihi kuendelea
kuifuata tu bila kutafuta namna ya kuirekebisha kwa manufaa ya
wananchi,” alisisitiza Kitwanga na kuongeza kuwa ni lazima kutumia
kanuni mbalimbali zilizopo kubadilisha mambo inapobidi na kutenda mambo
sawa sawa kwa manufaa ya wananchi.
Katika hatua nyingine, Naibu Waziri Kitwanga aliwataka Watendaji
katika Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) kuwasaidia wachimbaji
wadogo wa madini ili watoke katika uchimbaji mdogo na kuwa wachimbaji wa
kati na kuendelea, hivyo kukuza kipato chao na uchumi wa nchi kwa
ujumla.
“Ni lazima ifike mahala madini yetu yachimbwe na Watanzania
wenyewe hali itakayosaidia mzunguko wa fedha nchini kuwa mkubwa zaidi,”
alisema.
Aidha, Naibu Waziri Kitwanga aliwataka Stamico watakapokuwa
wanachimba madini, wahakikishe faida yote inarudi nchini ili kukuza
mzunguko wa fedha na hivyo kuinua uchumi wa nchi. “Hata wenzetu
wanapeleka fedha zote za faida kwao. Wanazobakiza hapa, ni zile tu
wanazohitaji kuendeshea biashara,” alitoa mfano.
Akizungumza na Wafanyakazi wa Wakala wa Ukaguzi Madini Tanzania
(TMAA), Naibu Waziri Kitwanga aliwataka kufanya kazi kwa juhudi ili
kuhakikisha mapato ya Serikali yanakusanywa kikamilifu.
“Leteni maoni kuhusu nini zaidi kifanyike ili kuhakikisha mapato
ya Serikali katika sekta ya madini yanaongezeka,” alisisitiza Kitwanga.
TAN
Bayport
Kikoa
Myway entertainment
FORE PLAN CLINIC
MPINGA CUP 2016
Mashujaa Fm 89.3, Lindi
Saturday, March 7, 2015
Kitwanga aagiza wachimbaji madini wasiolipa wanyang’anywe leseni
Naibu Katibu Mkuu wa UDP Zanzibar amvaa Maalim Seif
kuu wa UDP Zanzibar Juma Khamis Fakih amemvaa Katibu Mkuu wa Chama Cha Wananchi CUF Maalim
Seif
Sharif Hamad na kuigwaya kauli yake ya kuwataka wananchi kutoshiriki
zoezi la upigaji wa kura ya maoni juu ya katiba inayopendekzwa .
Amesema
kuwa kauli ya Katibu Mkuu wa CUF haina nia njema na wananchi wa
Zanzibar na haifai kutolewa na Kiongozi wa juu wa Serikali kama huyo
ambaye amepewa dhamana ya kuwaongoza na kuwatumikia wazanzibar .
MAFUNZO YA SIKU TATU KWA WAFANYAKAZI WA SEKTA YA AFYA ZANZIBAR JUU YA KUKABILIANA NA UGONJWA WA EBOLA YAFUNGWA.
ZI 10000 KUNUFAIKA NA UKARABATI BWAWA LA KALEMAWE
Na Mwandishi Wetu
Thursday, March 5, 2015
WADAIWA SUGU BILI WASABABISHA WANANCHI KUKOSA MAJI KATIKA MJI WA MPWAPWA, WAMO NMB
Nyaraka
hizo zina orodha kubwa ya wadaiwa zikiwemo taasisi za serikali ,
makampuni zikiweno benki kama vile NMB inayodaiwa fedha ndogo ambayo
jumla yake ni shilingi elfu 79.179.50 fedha ambayo ni ndogo sana ikiwa
ni bili ya mwezi wa pili 2015.
Sauala
hilo limekuja baada ya malalamiko ya wananchi katika mkutano huo ambapo
walimweleza Katibu Mkuu wa CCM kuwa maji hayatoki, lakini kila mwezi
wanadaiwa bili ya maji jambo ambalo limekuwa kero kubwa kwao, Akielezea
sakata hilo mbele ya Katibu Mkuu wa CCM, Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji
Mpwapwa Bw. Shadrack Matemba amesema mradi huo ni mkubwa na unatosheleza
mahitaji ya maji kwa wananchi wa mji wa Mpwapwa. tatizo ni kwamba
Taasisi na makampuni mengi hayalipi bili zao kwa wakati jambo ambalo
linafanya uendeshaji kuwa mgumu huku akikabidhi nyaraka za wadaiwa hao
mbele ya Kinana
Balozi wa Marekani Nchini amtembelea mwanasheria Mku wa Serikali
KIJIJI CHA GONGONI WILAYANI KILOSA WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI, WANAWAKE WAPATA HATI MILIKI ZA ARDHI
Angelina
Mziray Katibu Mkuu wa Women and Poverty Alleviation in Tanzania ,
Akiwakaribisha wageni Mbalimbali waliofika katika Sherehe za Kuazimisha
Siku ya Wanawake Duniani ambapo wao wameadhimisha mapema,Katika Ufunguzi
Alisema kuwa Shirika lisilo ka Kiserikali la Waupata wakishirikiana na
OXFAM wamesaidia Kijiji hicho katika kuleta maendeleo mbalimbali Tangu
mwaka 2006 ikiwa ni pamoja na Kilimo cha mpunga, Matumizi Bora ya Ardhi,
Ambapo Pia aliwashukuru OXFAM kwa kuleta ufugaji bora wa kuku wa
kienyeji, na ujenzi wa masoko mawili ya kisasa, Pia kusaidia wanawake
kupata hati milili za Ardhi ambapo wanawake 186 watapata Hati hizo.
Mwisho alishukuru taasisi zengine zisizo za Kiserikali ikiwemo
Mviwata,Ungo,Tupawaki pamoja na Mwayodeo kwa jitihada zao za kusaidia
wanawake na wanakijiji cha Gongoni katika maendeleo ya kijiji hicho.
Mkurugenzi
Mkazi wa Oxfam Tanzania Jane Foster
MWANAHARAKATI WA SIKU NYINGI WA WANYAMAPORI NCHINI TANZANIA AMPONGEZA RAIS KENYATTA
Mwanaharakati wa siku nyingi wa
wanyama pori na mazingira nchini Tanzania Kidon Mkuu, akiwa Philipine
Manila December 2014 kwenye harakati zake za matatembezi ya kupinga
kuuwawa kwa Tembo na Faru akiwa na wanaharakati wenzake wa huko
Philipine
Mwanaharakati wa siku nyingi wa
wanyama pori na mazingira nchini Kidon Mkuu, akiwa Philipine Manila
December 2014 kwenye matatembezi ya kupinga kuuwawa kwa Tembo na Faru
akiwa na Susan Jaylo
Rais Kikwete amtembelea Rubani wa ndegevita Hospitali ya Jeshi Lugalo
UFAFANUZI JUU YA HALI YA AFYA YA NAIBU SPIKA
Ukweli ni kwamba Naibu Spika wa
Bunge, Mhe. Job Ndugai ni Mzima wa afya na hivi sasa yuko jimboni kwake
Kongwa, Mkoani Dodoma akifanya maandalizi ya Mwisho ya Ziara ya Katibu
Mkuu wa CCM Ndg. Abdulrahman Kinana itakayofanyika mwishoni mwa wiki hii
na hasa Jimboni Kongwa, Dodoma.
Ofisi ya Bunge inapenda kuwatoa
hofu Wananchi wote na kuwataka kuzipuuza taarifa hizo kwa kuwa si za
kweli bali ni uvumi unaonezwa na watu wachache wenye nia ovu ya kujenga
hofu miongozni mwa Wananchi kupitia mitandao ya kijamii.
Aidha tunapenda kutoa rai kwa watu
wote kuacha kusambaza taarifa hizo potofu na badala yake kama kuna
taarifa zozote kuhusu Ofisi ya Bunge au Viongozi wake wafanye jitihada
za kuthibitisha taarifa hizo kwenye Mamlaka husika kabla za kuzisambaza.
Ofisi ya Bunge inao utaratibu
rasmi wa kutoa taarifa muhimu kwa wananchi na umma kwa ujumla, hivyo si
vyema kwa watu kusambaza taarifa potofu kuhusu Bunge na viongozi wake
ambazo zinaweza kuleta usumbufu miongoni mwa Viongozi na baadhi ya
wananchi.
Imetolewa na:
Idara ya Habari, Elimu kwa Umma na Uhusiano wa Kimataifa
Ofisi ya Bunge
DAR ES SALAAM
4 MACHI 2015
MAONESHO YA UTALII YA ITB YAANZA RASMI UJERUMANI
Komba alikuwa Makamu Mwenyekiti SHIWATA
MTANDAO wa Wasanii Tanzania
(SHIWATA) unaungana na watanzania wote kuomboleza kifo cha Makamu
Mwenyekiti wao, John Komba aliyefariki Jumamosi na kuzikwa jana nyumbani
kwao kijiji cha Litui, Mbinga mkoa wa Ruvuma.
Mwenyekiti wa SHIWATA, Cassim Taalib katika salamu zake za
rambirambi alisema mtandao huo umempoteza kiongozi mwadilifu aliyetumia
kipaji chake cha usanii kuwaunganisha makundi ya wanamichezo,waigizaji,
wasanii wa luninga, bongo movie,wacheza sarakasi na waandishi wa habari
kuunda mtandao huo.
Alisema Kepteni Komba siku zote za
maisha yake aliamini sanaa ni mkombozi wa wanyonge katika jamii ambako
alitumia fani yake ya ualimu kufundisha wasanii wa fani mbalimbali
alipokuwa na kikundi cha Tanzania One Theatre (TOT), aliunda Kwaya,
maigizo, sarakasi, taarab na muziki wa dansi.
Marehemu Komba akiwa na kikundi
chake cha TOT aliibua vipaji vya wasanii mbalimbali waliotamba zamani na
wengine bado wanaendelea kutamba katika kama Nasma Hamisi Kidogo, Laila
Khatib, Sheba Juma, Selemani Pembe, Banza Stone, Mohamed Mrisho, Badi
Makule, Ali Star, Khadija Kopa, Othman Sudi, Abdul Misambano, Mwanamtama
Hamisi na Haji Boha.
Taalib alisema SHIWATA imempoteza
kiongozi aliyekuwa msaada mkubwa katika kuimarisha mtandao huo kwa hali
na mali na kuwashawishi wasanii wake wa TOT kujiunga na mtandao huo ili
kushirikiana katika kujenga kijiji cha wasanii cha Mwanzega, Mkuranga.
Marehemu Komba ambaye alikuwa
mwanachama mwenye kadi namba moja wa SHIWATA kati ya wanachama 8,000 wa
mtandao huo alikuwa akilipia michango yake na kuwa mfano kwa wengine.
Taalib alisema SHIWATA imewapoteza
wanachama maarufu katika kipindi cha karibuni na hivyo kuongeza pengo
katika utendaji wake kama Ibrahim Muchacho, Fundi Said (Mzee Kipara),
Seteven Kanumba, Hamisi Amigolas na Amina Ngaluma.
Alisema katika uongozi wa marehemu
Komba amesaidia kujengwa kwa nyumba 104 za wasanii katika kijiji cha
Mwanzega ambapo wasanii wanaendelea na ujenzi.
HOSPITALI KUU YA MNAZI MMOJA YAZIDUA UPIMAJI, USIKIVU WA WATOTO WACHANGA.
Waziri
wa Afya wa Zanzibar Rashid Seif Suleiman akikata utepe kuzindua mpango
wa upimaji usikivu wa watoto wachanga katika hafla iliyofanyika
Hospitali Kuu ya Mnazimmoja Mjini Zanzibar, wa kwanza (kushoto)
mwakilishi wa WHO Zanzibar Dkt. Ghirmay Andemichael na (wakatikati)
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Afya Zanzibar Bi. Halima Maulid Salum.
Daktari
Asma Ame Hassan akimpima usikivu mtoto Nour Sabri Al hilal katika
uzinduzi wa kuwapima usikivu watoto wachanga hafla iliyofanyika
Hospitali kuu ya Mnazimmoja.
Wafanyakazi
wa Afya waliopatiwa mafunzo maalum ya kuwapima usikivu watoto wachanga
wakimsikiliza Waziri wa Afya (hayupo pichani) katika uzinduzi huo.
Waziri
wa Afya Rashid Seif Suleiman akisitiza jambo wakati wa uzinduzi wa
kuwapima usikivu watoto wachanga. (kulia) Mkurugenzi wa Hospitali Kuu ya
Mnazimmoja Dkt. Jamala Adam Taib na (kushoto) Naibu Katibu Mkuu Wizara
ya Afya Zanzibar Bi. Halima Maulid Salum.
Baadhi
ya wageni walioalikwa katika uzinduzi wa kuwapima usikivu watoto
wachanga wakifuatilia uzinduzi huo uliofanyika Hospitali ya Mnazimmoja.
…………………………………………………………………….
Na Ali Issa Maelezo Zanzibar.
Waziri wa Afya wa Zanzibar Rashid
Seif Suleiman amesema sikio, mdomo na macho ni sehemu muhimu sana
katika maisha ya binaadamu hivyo unapokuwa na wataalamu wa
kushughulikia viungo hivyo ni neema kubwa inayopaswa kuenziwa.
Haya ameyasema jana katika
Hospitali kuu ya Mnazi Mmoja Mjini Zanzibar wakati wa uzinduzi wa
kuwapima usikivu watoto wachanga mara baadaya kuzaliwa ili kujua
matatizo yao.
Amesema uchunguzi wa watoto
wachanga kujua usikivu wao mapema ni mpango mzuri ambao utalisaidia
Taifa kuwa na watoto wenye usikivu mzuri na njia rahisi ya kuwapatia
matibabu kwa watakaogundulika na matatizo hayo.
“Kujua tatizo la kiafya mapema na
kuanza kulishughulikia kunapunguza gharama za matibabu hivyo nawanasihi
wazazi kuwapeleka watoto wenu mara baada ya kujifungua, ”alisisitiza
Waziri wa Afya.
Amesema maradhi ya usikivu
yamekuwa yakiwasumbua watoto wengi Zanzibar na iwapo kila mzazi
atatimiza wajibu wake wa kumpeleka mtoto wake kupata vipimo yataweza
kupungua.
Waziri wa Afya aliwataka wazazi
kuwa na utamaduni wa kuzalia Hospitali ili kupata huduma hiyo kwa
urahisi na watakaozalia majumbani kuwapeleka watoto wao kuchunguzwa
usikivu mara baada ya kuzaa.
Aidha Waziri huyo aliwataka
madaktari waliopatiwa mafunzo ya kutoa huduma hiyo kuwa waadilifu
katika kutekeleza kazi zao kwani huduma za watoto wachanga na wazazi
zinahitaji uvumilivu.
Waziri alisema tatizo la uskivu
huazia mtoto anapochelewa kulia mara baada ya kuzaliwa ama wanapopata
homa ya manjano, kutopatiwa chanjo, mzazi kuchelewa kuzaa baada ya
uchungu wa muda mrefu na kuzaliwa mtoto bila ya ya kufika muda wa
kuzaliwa.
Nao madaktari walio patiwa mafuzo
hayo walisema kuwa wana uwezo mzuri wa kuwapima usikivu watoto na
kubaini matatizo yao na kuishauri Serikali kuandaa utaratibu mzuri wa
kuwafikia watoto watakaozaliwa vijijini.
Mradi huo wa kupima watoto usikivu
ulipokea msada wa vifaa vya kisasa vya uchunguzi kutoka Jumuiya ya
Madaktari wanotoa huduma za matibabu vijijini ( ZOP) ambavyo vina
thamani vya Dola elfu 50 za kimarekani.
SHIRIKA LA EfG LAWAWEZESHA WANAWAKE WAJASIRIAMALI KUTOKA LUSHOTO MKOANI TANGA NA TEMEKE KUFANYA ZIARA YA MAFUNZO YA SIKU TATU KATIKA MASOKO YA MANISPAA YA ILALA JIJINI DAR ES SALAAM
Ofisa
wa Shirika la Equality for Growth (EfG), Pauline Mdendemi akizungumza
na wanawake wafanyabiashara masokoni katika soko la Mchikichini Dar es
Salaam jana kutoka Wilaya ya Lushoto ambao wamekuja Manispaa ya Ilala
kwa mafunzo ya siku tatu kuhusu mambo mbalimbali pamoja na masuala ya
vicoba.
Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Soko la Mchikichini, Betty Mtewele (katika), akizungumza na wanawake wajasiriamali.
Katibu wa Umoja wa Wanawake Soko la Mchikichini, Juliana Richard akizungumza wakati wa mafunzo hayo.
Mjasiriamali kutoka Lushoto Tanga, Magreth Mkomwa (katikati), akiuliza swali katika mafunzo hayo.
Wanawake wajasiriamali wakiwa kwenye mafunzo hayo.
Wanawake wajasiriamali wakiwa kwenye mafunzo hayo.
Mwenyekiti wa Soko la Lukozi lililopo wilayani Lushoto, Zakati Tendwa akichangia jambo.
Washiriki wa mafunzo hayo wakiwa katika picha ya pamoja.
Wajasiriamali hao wakitembelea soko la Mchikichini kuona kazi za wenzao zinauzwa katika soko hilo.
Hapa wakiangalia nguo aina ya batiki zinazotengenezwa na wenzao wa soko hilo.
Hapa wakifurahia gauni la batiki katika soko hilo.
Dotto Mwaibale
WANAWAKE
wafanyabiashara katika masoko wametakiwa kujenga tabia ya kutunza
kumbukumbu zao na kufanya vikao vya mara kwa mara jambo litakalosaidia
kuwapunguzia changamoto za kazi zao.
Mwito
huo ulitolewa na Ofisa wa Shirika la Equality for Growth (EfG), Pauline
Mdendemi wakati akizungumza na wanawake wafanyabiashara masokoni Dar es
Salaam jana kutoka Wilaya ya Lushoto mkoani Tanga na Manispaa ya Temeke
ambao wapo Manispaa ya Ilala kwa ziara ya siku tatu ya mafunzo mbalimbali pamoja na masuala ya vicoba yaliyofikia tamati jana.
“Jengeni
tabia ya kutunza kumbukumbu zetu pamoja na kufanya vikao vya mara kwa
mara itawasaidia kujua changamoto mlizonazo na kuzitatua ” alisema
Mdendemi.
Mdendemi
alisema shirika hilo la EfG limefanikiwa kwa kiasi kikubwa utekelezaji
wa programu ya “Sauti ya Mwanamke Sokoni” kwa Manispaa ya Ilala ambapo
wanawake wajasiriamali wameweza kupaza sauti ya kupinga vitendo vya
kinyanyasaji dhidi yao.
Alisema
shirika hilo lilifanya mradi wa miaka mitatu katika manispaa hiyo
ambayo sasa imekuwa ya mfano na ndio maana wafanyabiashara wanawake
kutoka Lushoto mkoani Tanga wamefika kujifunza ili nao elimu hiyo
waipeleke kwa wenzao.
Alisema
lengo la mafunzo ni kuwapa fursa washiriki hao kuweza kujifunza kutoka
kwa wanawake wajasiriamali sokoni katika manispaa ya Ilala masuala
mbalimbali ikiwemo mbinu za kufanya ushawishi na utetezi ili kuboresha
mazingira ya ufanyaji kazi katika masoko.
Alitaja
malengo mengine kuwa ni namna ya kuongeza wanachama wa umoja na vicoba,
uendeshaji vikao vya umoja sokoni na namna mfumo wa kuweka na kukopa
(Vicoba) unavyoweza kuwasaidia wanawake wajasiriamali kukuza vipato vyao
na kuboresha biashara na maisha yao kwa ujumla.
Mdendemi
alitaja wajasiriamali walionufaika na mafunzo hayo kuwa ni wanawake
wanne kutoka wilaya ya Lushoto, Lukozi Lushoto watatu, Chamazi watatu na
Temeke Sterio watatu.
Mwenyekiti
wa soko la Lukozi kutoka Wilaya ya Lushoto mkoani Tanga, Zakati Tendwa
alisema mafunzo hayo yamewafumbua macho kwani walikkuwa hawajui chochote
kuhusu masuala ya vicoba na kwa niaba ya wenzake amelishukuru shirika
la EfG kwa kuwapigania wanawake wajasiriamali masokoni. (Imeandaliwa na mtandao wa www.habari za jamii.com)
Fwd: KATIBU MKUU KIONGOZI AFURAHISHWA NA UWEPO WA SACCOS MAKAZINI
PICHA NA IKULU
========================
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue amefurahishwa na
uwepo wa vyama vya Ushirika vya Akiba na mikopo (SACCOS) katika taasisi
na idara za serikali, akisema kuwa hilo ni jambo la maana kwa kuwa
inatoa fursa kwa watumishi kuwa na kipato cha ziada kitachosaidia
kuwaletea ahueni kwani mishahara pekee haikidhi matakwa yao yote.
Amesema SACCOS ni
kama
benki ya mtu mnyonge, na kusisitiza kwamba mifuko ya aina
hiyo inaposimamiwa vizuri faida yake kwa wanachama ni kubwa sana kwani
humpa mtumishi ahueni na kumfanya afanye kazi kwa moyo na bila wasiwasi
ama usongo wa mawazo.
Balozi Sefue ameyasema hayo Jumanne Machi 3, 2015 jioni alipokuwa akiongea na uongozi wa Ikulu SACCOS,
uli
omtembelea ofisini kwake Ikulu Dar es salaam kumkabidhi rasmi
kitabu chake cha uanachama kufuatia kujiunga kwake na ushirika huo.
“Mishahara yetu ndani ya utumishi wa umma haitoshi kukidhi
mahitaji yetu yote, kwa hiyo mipango yote hii ya SACCOS, Mfuko wa
Rambirambi na Mfuko wa Ushirika
iliyopo hapa Ikulu
inafanya maisha ya mtumishi yawe na ahueni sana na kumfanya afanye kazi kwa moyo.
“Hayo ni mambo ambayo nayaamini sana na nayaunga mkono; na
naamini hata Mhe Rais mwenyewe anayaunga mkono na ndio maana amekuwa
mwepesi kujiunga na ushirika ”, amesema Balozi Sefue baada ya
kukabidhiwa kitabu namba 2 na Makamu Mwenyekiti wa Ikulu SACCOS, Bw.
Deodatus Gaudio. Kitabu namba moja amekabidhiwa Rais Jakaya Mrisho
Kikwete.
Awali, mshauri Mkuu na Mlezi wa Ushirika huo wa Ikulu, Bw.
Joseph Sanga, alimfahamisha Katibu Mkuu Kiongozi kwamba mifuko ya
SACCOS, Ushirika wa Nyumba na Rambirambi ya watumishi wa Ikulu iko
imara na inaendelea kunufaisha wanachama wake kwa ufanisi.
Bw. Sanga amesema malengo makuu ya mifuko hiyo ni kuleta
ustawi kwa watumishi na kwamba wote wanaelewa kuwa mikopo ya SACCOS yao
sio kwa ajili ya kununulia chakula ama mavazi bali ni ya kuwekeza kwenye
miradi itayowaongezea kipato.
“TUnataka kwenda mbali zaidi kwa kushirikiana na mfuko wetu
ya Ushirika wa Nyumba ambo tayari umepeleka maombi ya ardhi kwa
wanachama wake ambapo viwanja vikipatikana tuna mategemeo ya kuwapa
mikopo kuvununua. Mpango huu una faida kwani ni wa amana kubwa na riba
ndogo”, alisema Bw. Sanga alipokuwa anafafanua kuhusu mipango ya Ikulu
SACCOS.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo ahimiza watumishi wake kuendelea kuwa wabunifu katika kutekeleza majukumu yao
WANANCHI WATAKIWA KUCHANGIA ELIMU
Mkurugenzi wa tigo nyanda za juu
kusini, Jackson Kiswaga akikabidhi moja ya bati alizotoa kwa shule
mbalimbali za jimbo la Kalenga wilaya ya Iringa
…………………………………………………………………………..
NA DENIS MLOWE, IRINGA
WANANCHI wa jimbo la Kalenga
wametakiwa kujenga utamaduni wa kuchangia maendeleo ya sekta ya elimu,
badala ya kujikita kuchangia sherehe za harusi na mambo mengine
yasiyokuwa na tija katika maendeleo ya jimbo hilo.
Hayo yamezungumzwa na mdau wa
maendeleo, Jackson Kiswaga wakati akikabidhi mabati 50 na mifuko ya
saruji 30 kwa shule ya sekondari ya Nyabula inayomilikiwa na kanisa
katoriki parokia ya Nyabula katika sherehe ya kuchangia ujenzi wa
maabara ya Shule hiyo iliyoko katika wilaya ya Iringa vijijini.
Kiswaga alisema kuwa urithi
pekee kwa watoto ni elimu hivyo ni jukumu la wazazi kuchangia sekta ya
elimu kuliko kusubiri serikali ambayo ina mzigo mkubwa kwa faida ya
vizazi vilivyopo na vijavyo katika kukuza uwezo wa wanafunzi katika
mambo ya masomo.
“Mzazi unaweza kumwachia kijana
wako mali, lakini itakwisha, ukimwachia elimu hakika huu ndiyo urithi
pekee watanzania wenzangu, tujitoe kuchangia sekta ya elimu kama ambavyo
tunafanya katika sherehe na kumbuka maisha ya sasa bila elimu
utasababisha mwanao awe katika maisha magumu hapo mbeleni hivyo
tusisubiri serikali tuwe na utamaduni wa kuchangia katika sekta hii ya
elimu ndugu zangu,” alisema Kiswaga.
Alisema kuwa juhudi za wananchi
na mashirika pamoja na serikali zinahitajika ili kuwajengea wanafunzi
mazingira bora ya kujifunzia na ili waweze kufaulu vizuri katika masomo
yao hivyo kuchangia maabara itasaidia sana kukuza uwezo wa mwanafunzi
katika masomo ya sayansi pindi yakikamilika.
Kiswaga aliongeza kuwa sekta ya
elimu ni sekta muhimu sana kwa maendeleo ya nchi ambapo inabidi juhudi
zaidi ziongezeke kuweza kuifanya elimu kuwa silaha bora itakayowasiadia
vijana kuondokana na umaskini.
Naye Padri wa Parokia ya Nyabula
Philipo Kindole alimshukuru Kiswaga kwa msaada wa mabati na saruji na
kuwataka wananchi wengine kuiga mfano huo kwa maendeleo ya elimu katika
mkoa wa
Subscribe to:
Posts (Atom)