TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Saturday, December 13, 2014

Uharibifu wa mazingira kutokana na wingi wa mifugo mkoani Katavi wawa tishio

unnamed1
DC Mpanda Paza Mwamlim akiwahutubia wafugaji katika kijiji cha Sibwesa Wilayani Mpanda na kuwasisitiza umuhimu wa hifadhi mazingira na kuwaasa wafugaji.
kupunguza mifugo yao wafuge ufugaji wenye tija,
unnamed 
Baadhi ya maeneo yaliyoathiliwa na uharibifu wa mazingira kutokana na wingi wa Mifugo Katika Halamshauri ya Wilaya ya Wilaya ya Mpanda.(Picha na Kibada Kibada Katavi
………………………………………………….
Na Kibada Kibada –Katavi
Makala
Sekta ya Mifugo Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda Mkoani Katavi inakabiliwa na Changamoto mbalimbali  hali inayofanya sekta hiyo kutafuta mbinu na mikakati ya kukabiliana na changamoto hizo ikiwemo uharibifu mkubwa wa mazingira kutokana na wingi wa mifugo uliopo kuliko ukubwa wa eneo la kufugia mifugo hiyo.
Baadhi ya Changamoto hizo ni kuwepo idadi kubwa ya mifugo katika halmashauri,Uzalishaji mdogo wa mazao ya mifugo kama nyama na maziwa na kipato kinachotokana na uwepo wa mifugo hiyo katika Halamshauri.
Changamoto nyingine ni upatikanaji  mdogo wa mbegu bora za mifugo hususani ng’ombe,eneo dogo la malisho ukilinganisha na Idadi ya  mifugo iliyopo kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda.
Pamoja na kuwepo kwa wingi wa mifugo  pia magonjwa mengi ya mifugo kama ndorobo,ndigana kati na homa ya mapafu nayo ni moja ya changamoto inayoikabili sekta ya mifugo Katika Halmashauri ya Mpanda.
Halmashauri ya Mpanda ambayo ni moja ya Halmashauri katika Mkoa wa Katavi ina idadi ya Ng’ombe wapatao 87,928,mbuzi 44,348,Kondoo 8,712,Nguruwe 2,237, mbwa 7425,na kuku 141.832  hata hivyo uwepo wa mifugo hiyo bado haijatumiwa  vizuri na kubadili maisha ya wakazi wa Halmashauri hiyo na mkoa kwa ujumla kiuchumi na kuinua pato lao kiuchumi.
Tafiti zinaonesha iwapoidadi ya mifugo hiyo iliyopo ikitumiwa vizuri inaweza kuleta tija na kuwaondolea umasikini wananchi katika maeneo husika.
Kwa mantiki hiyo wataalam wa sekta ya mifugo wanayo kazi kubwa mbele yao kuhakikisha wanatumia elimu yao kuwabadili wafugaji waweze kufuga ufugaji wenye tija tofauti na ilivyo kwa sasa ambapo ufugaji umekuwa wa kutokuwa na tija na kila kukicha imekuwa ni mivutano na migogoro kati ya wakulima na wafugaji ingawa hali hiyo bado haijatokea katika Halmashauri ya Mpanda lakini tunashuhudia maeneo mengi hapa nchini hususani Mkoani Morogoro,wilaya ya Kilosa na Kilombero,Mkoani Pwani ,na Arusha na Tanga wakulima na wafugaji migogoro ya kila mara.
Uwepo wa mifugo mingi katika Halamshauri ya wilaya ya Mpanda pia kumeambatana nanUharibifu wa  mazingira  kutokana na wafugajinhao kuhamahama  na wengine kutumia njia hiyo kwa kufyeka miti na mistu kwa shughuli za kilimo kwa kuwa wafugaji walioko katika Halmsahauri ya Mpanda hao hao ndio wakulima.
Uchunguzi uliofanyika kwa baadhi ya maeneo Mbalimbali Wilayani Mpanda inaonesha maeneo mengi yanaoonekena kuathiri na Uharibifu wa mazingira  na iwapo hatua za  makusudi hazitachukuliwa kwa haraka maeneo hayo yanaweza kugeka jangwa.
Baadhi ya maeneo yaliyoathirwa na uharibifu wa mazingira kutokana na mifugo  ni bonde la Mto Katuma ambao ni tegemeo  kwa wakazi wa Mkoa wa Katavi hususani Mbuga ya Katavi ya Katavi ambayo wanyama walioko huko hutegemea kupata maji kutoka bonde la mto huo ambalo hutiririsha maji yake kupitia vijito vyake kupeleka hifadhi ya Katavi.
Mbali ya kutegemewa kwa ajili ya maji ya wanyama kama viboko na wengineo pia bonde la mto huo wa Katavi ndilo linalotegemewa kwa kilimo cha mbuga unaozalishwa kwa wingi katika maeneo ya Bonde hilo na kuwasaidia kuwaingizia pato wananchi Mkoani humo.
 
Continue reading →

No comments:

Post a Comment