TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Thursday, February 5, 2015

Serikali kuwasilisha Muswada wa Sheria ya Habari bunge la Aprili

MTA
Hussein Makame-MAELEZO,Dodoma
SERIKALI inatarajia kuwasilisha Muswada wa Sheria ya Habari katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania la mwezi April mwaka huu ili kujadiliwa na kupitishwa kuwa Sheria kamili.

Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Maendeleo ya Jamii Saidi Mtanda wakati akiwasilisha taarifa ya kazi za kamati yake kuanzia Januari 2014 hadi Januari 2015.
Alisema muswada huo ni moja kati ya kilio cha wadau wa habari nchini ambao unatarajiwa kuikomboa taaluma hiyo kwa kusimamia masuala yote yanayohusu taaluma hiyo muhimu duniani.
Akizungumzia huhusu Mfuko wa Maendeleo ya Vijana na Wanawake, Mwenyekiti Mtanda alipendekeza kuwa halmashauri zote nchini ambazo hazijatenga asilimia 5 ya wanawake na asilimia 5 ya vijana ziorodheshwe na zichukuliwe hatua kali.
Kwa mujibu wa takwimu zilizopo, tangu kuanzishwa kwa Mfuko wa Mandeleo ya Vijana na Wanawake mwaka 1993, ni halamashauri chache zimekuwa zikitenga fedha hizo kama inavyotakiwa.
Katika taarifa yake, Mwenyekiti Mtanda alionesha kuridhishwa na maendeleo ya Mfuko wa Maendeleo ya Vijana wa halamashauri ya Wilaya ya Temeke ulio chini ya Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo.
Alisema katika ziara ya kutembelea mfuko huo Januari 19 mwaka huu, walitembelea miradi ya vijana ya kikundi cha Sokoine Youth Development, Waungwana Youth Family na African Legends.
Kwa upande wa Mfuko wa Maendeleo ya Wanawake, Mwenyekiti alizipongeza halmashauri ya mji Korogwe na zingine ambazo zimekuwa mfano wa kuigwa kwa kutenga fedha za mfuko huo na kuzitumia kama ilivyokusudiwa.
Mbali na mradi huo, alisema kamati pia ilitembelea mradi wa vituo vya kurushia matangazo ya Redio Mafifi, Iringa na Kola Hill, Morogoro uliogharimu shilingi Milioni 200.
“Mradi wa Mafifi Gangilonga, Iringa ni katika ya miradi mikubwa ya kufunga mitambo ya kurushgia matangazo katika vituo 9…Maeneo yaliyonufaika na mradi huu ni mkoa wa Manyara, Morogoro, Moshi, Mpanda, Newala, Shinyanga, Songea na Tunduru” alisema Mtanda.
Alisema mradi huo umewezesha kupatikana kwa matangazo ya redio kwa ubora zaidi ambapo matangazo hayo yanapatikana katika masafa ya FM-TBC Taifa (107.1MHz) na TBC FM (96.2MHz).
Aliongeza kuwa mradi huo umeweza kuongeza usikivu wa matangazo ya Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) kwani kwa sasa yanasikika katika maeneo mengi zaidi nje ya mji wa Iringa.

No comments:

Post a Comment