TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Saturday, January 18, 2014

CCM YAZIDI KUJICHANGANYA NDANI YA MAKUNDI YA WANAOWANIA URAIS 2015

 Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa.
Dar es Salaam. Makundi ya Urais wa 2015 yanaendelea kuivuruga CCM baada ya Mwenyekiti wa chama hicho Mkoa wa Singida, Mgana Msindai kuibuka na kusema atamburuta mahakamani Mwenyekiti mwenzake wa Mkoa wa Geita, Joseph Kasheku ‘Msukuma’ asipomwomba radhi kwa kumchafua kwa kumwita mpuuzi.
Hata hivyo, Kasheku amesema Msindai anaweza kwenda mahakamani huku akisisitiza kwamba hawezi kumwomba radhi kwa kuwa anaamini kwamba alichofanya ni kinyume cha taratibu za chama na vikao.
Juzi, Kasheku alimponda Msindai mbele ya waandishi wa habari kwa kitendo chake cha kusema kuwa wenyeviti wa CCM wa mikoa yote ya Tanzania wanamuunga mkono, Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa katika safari yake ya urais wa 2015 wakati wa sherehe ya mwaka mpya huko Monduli, Arusha.
Msindai alisema jana kuwa amemtaka Kasheku aitishe mkutano wa waandishi wa habari na kumwomba radhi. “Asipofanya hivyo ndani ya siku saba nitampeleka mahakamani,” alisema Msindai.
Msindai pia alikanusha kuwa aliwekwa kitimoto katika mkutano wa wenyeviti wa CCM wa mikoa uliofanyika Zanzibar.
Msindai aliyekuwa Mbunge wa Iramba Mashariki kwa miaka 15, alikiri kuwa alialikwa pamoja na wenyeviti wenzake sita katika sherehe ya mwaka mpya iliyoandaliwa na Lowassa huko Monduli.
Katika sherehe hizo, Lowassa alitangaza kuwa ameanza safari ya matumaini, kauli ambayo wachambuzi wa masuala ya kisiasa waliitafsiri kama tangazo la kuwania urais mwaka 2015.
Msindai alikanusha kutangaza kuwa wenyeviti wote wa CCM wa mikoa wanamuunga mkono Lowassa wakati wa sherehe hiyo... “Mimi ni Mwenyekiti wa wenyeviti wa CCM, lakini sikuwahi kuzungumza kuwa wenyeviti wote wanamuunga mkono Lowassa katika Uchaguzi Mkuu 2015... kikubwa tulichozungumza ni kumuunga mkono katika safari yake ya mafanikio katika kuendeleza elimu, maji, ujenzi wa zahanati.”
Msindai alisema wanamwangalia Lowassa kutokana na uwezo wake katika kusimamia mipango yake ya maendeleo na zaidi katika kupigania elimu pana kwa Watanzania.
“Alipokuwa Wizara ya Maji alichangia maji kupatikana Dar es Salaam na mikoani na maendeleo mengi, uwajibikaji kwenye jimbo lake na aendelee hivyo...hayo ndiyo tuliyomsifia. Nilizungumza haya na sitabadilika,” alisema Msindai, ambaye alisema haogopi kufukuzwa.
“Mimi si mpya ndani ya CCM kama ‘Msukuma’. Nina miaka zaidi ya 40, ninaelewa taratibu zote za chama za udiwani, ubunge na urais. Kama ni kampeni ni baada ya chama kumpitisha mtu na sisi tutamuunga mkono... hata mimi ninaweza kuwania urais,” alisema.
Siombi radhi
Kwa upande wake Kasheku alisema hamwombi radhi Msindai, kwani si wenyeviti wote wa CCM wanaomuunga mkono Lowassa katika safari yake aliyoiita ya matumaini.
“Siombi radhi na hata sasa hivi anaweza kushtaki, tulipokutana Zanzibar alitueleza kuwa alitoa kauli ya kuumuunga mkono Lowassa kimakosa na kusema alikuwa akimaanisha yeye na wenzake aliokwenda nao Monduli ndiyo wanamuunga mkono Lowassa,” alisema Kasheku.
Kasheku alifafanunua kuwa Msindani alisema kuwa wanahabari walikosea kumnukuu baada ya kuandika katika vyombo vya habari kuwa alisema wenyeviti wote wanamuunga mkono Lowassa.
Alisema baada ya Msindai kukiri jambo hilo, wenyeviti waliokuwa Zanzibar waliandaa tamko la pamoja na kuagiza lisomwe na Msindai mbele ya wanahabri katika Ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo, Dar es Salaam.
“Katika huo mkutano ilitakiwa niwepo mimi (Kasheku), Msindai na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam, Ramadhan Madabida, ila cha ajabu mwenzetu (Msindai) alitukimbia na tulipomtafuta akasema yupo Singida, hivyo sisi tuliamua kutoa tamko lile,” alisema Kasheku.
Alisema kauli aliyoitoa Msindai ni kinyume na maagizo ya wenyeviti wote wa CCM, huku akimtaka kabla ya kwenda mahakamani, ahakikishe kuwa amewasilisha malalamiko yake ndani ya chama ili Kamati ya Maadili ya chama ikae na kutoa uamuzi.
“Hatuna ugomvi na Lowassa, tuna ugomvi na yeye aliyetuweka nyuma yake na kusema wote tunamuunga mkono Lowassa, nani alimwambia maneno hayo na ilikuwa katika kikao gani?,” alihoji Kasheku na kuongeza:
“Kama kuna watu wapo nyuma ya Lowassa au mtu yeyote ni siri yao, iweje yeye atulazimishe sisi kuwa nyuma yake kwa mgongo wa Mbunge wa Monduli”.
Mgeja amtetea Msindai
Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Shinyanga, Hamis Mgeja ambaye pia alikuwa Monduli, alimtetea Msindai akisema hakuwahi kuzungumzia suala la urais katika mkutano huo wa Monduli zaidi ya kumsifu Lowassa kwa mafanikio aliyoleta kwenye jimbo lake na maeneo mengine alipokuwa Waziri Mkuu.
Alisema hakuna dhambi kwa kumpenda mtu yeyote, wote wanaotoa kauli za kukanusha ni dalili za woga, wivu, kutokujiamini na inawezekana wana watu nyuma yao.
 MWANANCHI

No comments:

Post a Comment