TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Friday, January 17, 2014

TAARIFA KUTOKA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA TFF


tff_LOGO1TFF YANOA MAKATIBU MABORESHO TAIFA STARS
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limeandaa semina ya siku mbili kwa makatibu wa vyama vya
mpira wa miguu vya mikoa kuhusu maboresho ya timu ya Taifa (Taifa Stars).
Semina hiyo inafanyika ukumbi wa Singida Motel, mjini Singida kuanzia kesho (Januari 18 mwaka huu) ambapo mada mbalimbali zitawasilishwa kwa washiriki kuhusu maboresho hayo.
TFF imeandaa mpango wa maboresho kwa Taifa Stars ambapo pamoja na mambo mengine umepanga kusaka vipaji nchini nzima kwa lengo la kupanua wigo wa kupata wachezaji wanaoweza kuchezea timu hiyo.
Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premiu Lager mwaka huu inakabiliwa na mechi za mchujo za Kombe la Afrika (AFCON) ambalo fainali zake zitafanyika mwakani nchini Morocco.
Mechi hizo za mchujo zitachezwa kati ya Septemba na Novemba mwaka huu ili kupata timu 16 zitakazofuzu kucheza fainali hizo.
WASOMALI KUCHEZESHA YANGA, WACOMORO
Shrikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) limeteua waamuzi kutoka Somalia kuchezesha mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika kati ya Yanga ya Tanzania na Komorozine Sports ya Comoro.
Mechi hiyo ya kwanza ya raundi ya mchujo itafanyika jijini Dar es Salaam kati ya Februari 7 na 9 mwaka huu wakati ile ya marudiano itachezwa kisiwani Comoro kati ya Februari 14 na 16 mwaka huu.
Mwamuzi wa kati atakuwa Hassan Mohamed Hagi wakati wasaidizi wake ni Hamza Hagi Abdi, Bashir Abdi Suleiman na Bashir Olab Arab. Kamishna wa mechi hiyo atakuwa Eugene Musoke kutoka Uganda.
Timu ambazo zimeingia moja kwa moja katika raundi ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa ni Coton Sport ya Cameroon, El Ahly (Misri), TP Mazembe (Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo- DRC), El Hilal (Sudan), Club Sportif Sfaxien (Tunisia) na Esperance (Tunisia)
Nayo mechi ya kwanza ya raundi ya mchujo kati ya Azam ya Tanzania na Ferroviario Da Beira ya Msumbiji itakayofanyika Dar es Salaam kati ya Februari 7 na 9 mwaka huu itachezeshwa na waamuzi kutoka Sudan.
Waamuzi hao ni Mutaz Abdelbasit Khairalla atakayepuliza filimbi, Waleed Ahmed Ali, Aarif Hasab Elton na El Fatih Wadeed Khaleel. Kamishna wa mechi hiyo ni Hassan Mohamed Mohamed kutoka Somalia. Mechi ya marudiano itachezwa Msumbiji kati ya Februari 14 na 16 mwaka huu.
Timu zilizotinga moja kwa moja katika raundi ya kwanza ya michuano hiyo ni Asec Mimosas ya Ivory Coast, Ismailia (Misri), Wadi Degla (Misri), Djoliba (Mali), MAS (Morocco), Bayelsa United (Nigeria), El Ahly Shandy (Sudan), E.S.S. (Tunisia), C.A.B. (Tunisia) na Zesco United (Zambia).
WATANZANIA KUCHEZESHA MECHI ZA CL, CC
Watanzania wanane wameteuliwa kuchezesha mechi mbili za marudiano za raundi ya awali za Ligi ya Mabingwa Afrika (CL) na Kombe la Shirikisho (CC) zitakazochezwa wikiendi ya Februari 14 na 16 mwaka huu.
Waamuzi hao walioteuliwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) ni Israel Mujuni atakayechezesha mechi ya CL kati ya Rayon Sport ya Rwanda na AC Leopards de Dolisie ya Congo itakayofanyika jijini Kigali.
Mujuni atasaidiwa na Josephat Bulali, Samwel Mpenzu na Ramadhan Ibada, wakati Kamishna wa mechi hiyo atakuwa Jean Marie Hicuburundi wa Burundi.
Naye Waziri Sheha ataongoza jopo lingine kwenye mechi ya CC kati ya FC MK ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC) na El Ahly Atbara ya Sudan. Mechi hiyo itachezwa jijini Kinshasa.
Sheha atasaidiwa na Ferdinand Chacha, John Kanyenye na Israel Mujuni. Kamishna wa mechi hiyo ni Chayu Kabalamula kutoka Zambia.
SEMINA YA KUPANDISHA MADARAJA WAAMUZI JAN 21
Semina kwa ajili ya kupandisha madaraja waamuzi itafanyika Januari 21 na 22 mwaka huu katika vituo vitatu vya Dodoma, Mwanza na Songea.
Waamuzi watakaoshiriki katika semina hizo ambazo pia zitahusisha mitihani ya utimamu wa mwili (physical fitness test) watajigharamia wenyewe na wanatakiwa kufika vituoni siku moja kabla. Waamuzi hao ni wa daraja la pili na tatu.
Kituo cha Dodoma kitahusisha waamuzi kutoka mikoa ya Arusha, Dar es Salaam, Dodoma, Kilimanjaro, Manyara, Morogoro, Pwani, Singida na Tanga. Wakufunzi katika kituo hicho ni Paschal Chiganga, Said Nassoro na Soud Abdi.
Wakufunzi wa kituo cha Mwanza kwa ajili ya waamuzi wa mikoa ya Geita, Kagera, Katavi, Mara, Mwanza, Shinyanga, Simiyu na Tabora ni Alfred Kishongole, Kanali Issarow Chacha, Saloum Chama na Zahra Mohamed.
Kituo cha Songea ni kwa ajili ya waamuzi kutoka Iringa, Lindi, Mbeya, Mtwara, Njombe, Rukwa na Ruvuma. Wakufunzi katika kituo hicho ni Charles Ndagala, Joseph Mapunda, Riziki Majala na Victor Mwandike.
Waamuzi wote wanatakiwa kwenda katika kituo walichapangiwa. Vilevile wanatakiwa kuwa na barua kutoka kwa makatibu wa Vyama vya Waamuzi wa Mpira wa Miguu Tanzania (FRAT) wa mikoa yao ikiwatambulisha pamoja na kuonesha madaraja yao. 

Simba VS Mtibwa kesho kiingilio sh.5000

imagesMABINGWA wa michuano ya mtani Jembe, timu ya Simba,
kesho  inashuka katika Uwanja wa Taifa kuvaana na timu ya

Mtibwa Sugar, huku kiingilio cha chini kikiwa sh.5000.

Mchezo huo utakaoanza saa 10 jioni, ukiwa wa kirafiki,

kwa ajili ya kuziweka timu hizo sawa kabla ya kuanza kwa

Ligi Kuu tanzania Bara, inayoanza kutimua vumbi wiki

ijayo.

Simba inaingia dimbani ikiwa inatoka kwenye mashindano

ya Mapinduzi, ambapo Simba ilichukua ushindi wa pili.

Katika mchezo huo Simba iliyopo chini ya kocha Zdravko

Logarusic akisaidiana na Suleiman Matola, imepanga

kutumia wachezaji wake, wote ili kiwe kipimo tosha kabla

ya Ligi Kuu.

Timu hiyo inayoshika nafasi ya nne katika msimamo wa

Ligi, imejipanga kuhakikisha inavuka mpaka nafasi ya

kwanza huku kocha wao Logarusic, akisema ana uhakika

kikosi chake kitaibuka na ushindi.

Logarusic, alisema kuwa mchezo huo ni moja ya mtihani

wake wa kutambua kikosi chake, kabla ya kuanza kwa ligi

kuu.

Alisema ameambiwa kuwa Mtibwa Sugar, ni moja ya timu

nzuri hivyo anajua kwake ni kipimo kizuri.

“Nina amini mchezo wetu na Mtibwa Sugar, utakuwa mzuri

, kutokana na ubora wa timu hiyo, ninajua itasaidia timu

yangu kupata mazoezi mazuri”alisema Logarusic.

Nae kocha wa Mtibwa Sugar, Mecky Mexime, alisema ana

amini mchezo huo utakuwa mzuri kwake kutokana na

wapinzani wao kutoka katika mashindano.

Mexime alisema kuwa amepata nafasi ya kucheza na timu

kubwa, ambayo itampa mazoezi mazuri.

“Nina amini mchezo huo utakuwa mzuri kwangu kwa kuwa

nacheza na timu kubwa ambayo imetoka kwenye

mashindano”alisema Mexime.

Katika mchezo huo viingilio vitakuwa shilingi 20,000 VIP A,

shilingi 10,000 katika VIP B, wakati VIP C itakuwa shilingi

7,000 na sehemu ya viti vya orange na bluu itakuwa

shilingi 5000.

The Commonwealth Games Queen’s Baton Arrives in Dar es Salaam on 18 January

index
The Glasgow 2014 Commonwealth Games, British High Commission, Tanzania Olympic Committee and UNICEF Team up to Stop Violence Against Children in Tanzania
The Glasgow 2014 Commonwealth Games Queen’s Baton will arrive in Dar es Salaam on Saturday, 18 January. The actual run is planned for Sunday, 19 January, and will kick off from the National Stadium at 2.00 pm to State House where it will be presented to H.E. President Jakaya Kikwete. It is expected that over 300 people will be involved in the 12.4 km race.
Tanzania Olympic Committee’s Secretary General, Filbert Bayi, the British High Commissioner to Tanzania, Dianna Patricia Melrose, and the UNICEF Tanzania Representative, Dr. Jama Gulaid, will kick off the Relay, and be amongst the guests at State House.
This year, the Glasgow 2014 Commonwealth Games, the Commonwealth Games Federation and UNICEF have launched a ground-breaking partnership globally. In Tanzania, the event represents a unique opportunity for the Tanzania Olympic Committee, the British High Commission, UNICEF and other partners to harness the power of sport to help children grow up healthy, happy and safe.
The Queen’s Baton relay in Tanzania will be themed around the slogan: “Stop Violence Against Children, Let Them Play!”.
Speaking ahead of the Queen’s Baton Relay, British High Commissioner Dianna Melrose said:The Glasgow 2014 Commonwealth Games is teaming up with UNICEF to transform children’s lives across the Commonwealth. It’s the first time a charity affiliation to the Games has taken place. I am delighted the UK is supporting this excellent cause. Violence against children is a worrying issue and we must do all we can to stop it.”
The aim is to use the event as a catalyst to create awareness and better understanding of the issue of violence against children amongst a more general audience in Tanzania”, says the Tanzania Olympic Committee’s Secretary General, Filbert Bayi.
The Tanzania Violence Against Children Study, released by the Government and UNICEF in 2011 revealed that in Tanzania, violence affects a majority of children, everywhere. Some of the key findings are:
· one in three girls and one in seven boys in Tanzania experiences sexual violence before the age of eighteen; · most sexual assaults occur at home or in school – and children often know their sexual


No comments:

Post a Comment