TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Wednesday, January 15, 2014

TAIFA STARS KUIKABILI NAMIBIA FIFA DATE

7 
Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) itacheza mechi ya kirafiki dhidi ya Namibia (Brave Warriors) ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya michuano ya kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Afrika (AFCON) zitakazochezwa mwakani nchini Morocco.
Stars na Brave Warriors zitacheza mechi hiyo Machi 5 mwaka huu jijini Windhoek, Namibia. Mechi hiyo ipo katika kalenda ya mechi za kirafiki za Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA)
Makubaliano ya kucheza mechi hiyo yamefikiwa kutokana na mazungumzo kati ya Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi na Rais wa Chama cha Mpira wa Miguu Namibia (NFA), John Muinjo.
Benchi la Ufundi la Brave Warriors linaongozwa na kocha mzawa Ricardo Mannetti, na mechi hiyo itachezwa ama Uwanja wa Sam Nujoma au Uwanja wa Uhuru jijini Windhoek.
Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager inafundishwa na kocha Kim Poulsen kutoka Denmark na inatarajia kuanza kucheza mechi za mchujo za AFCON Septemba mwaka huu.

No comments:

Post a Comment