TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Monday, January 13, 2014

TAARIFA YA TAHADHARI YA MVUA KUBWA NA UPEPO

220px-Coat_of_arms_of_Tanzania.svg
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA UCHUKUZI MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA
Simu: 255 22 2460735/2460706
FAKSI: 255 22 2460735/2460700 S.L.P. 3056
Barua pepe: met@meteo.go.tz DAR ES SALAAM
Tovuti: www.meteo.go.tz
……………………………………………………..
Taarifa kwa umma: Kunatarajiwa kuwepo na upepo mkali, mawimbi makubwa na mvua kubwa.
Taarifa Na.
201401-03
Muda wa Kutolewa
Saa za Afrika Mashariki
Saa 4 Asubuhi
Daraja la Taarifa:
Tahadhari
Kuanzia:
Tarehe
14 Januari, 2014
Mpaka:
Tarehe
16 Januari, 2014
Aina ya Tukio Linalotarajiwa
1. Hali ya Upepo mkali unaozidi kilomita 40 kwa saa pamoja na mawimbi makubwa zaidi ya mita 2.0
2. Vipindi vya mvua kubwa (zaidi ya mm 50 ndani ya saa 24)
Kiwango cha uhakika:
Wastani (60%)
Maeneo yanayotarajiwa kuathirika
1. Upepo mkali: Pwani ya mikoa ya Tanga, Dar es Salaam, Pwani, Lindi, Mtwara pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba
2. Mvua kubwa: Mikoa ya Rukwa, Mbeya , Njombe, Ruvuma, Mtwara pamoja na kusini mwa mkoa wa Morogoro
Maelezo:
Hali hii inatokana na kuimarika kwa mfumo wa mgandamizo mdogo wa hewa kusini magharibi mwa Bahari ya Hindi, maeneo ya mkondo wa Msumbiji. Mfumo huu unatarajiwa kuvuta upepo kutoka Pwani ya Somalia na misitu ya Congo.
Angalizo:
Watumiaji wa bahari na wakazi wa maeneo hatarishi wanashauriwa kuchukua tahadhari.
Maelezo ya Ziada
Mamlaka ya Hali ya Hewa inaendelea kufuatilia hali hii na itatoa mrejeo pale itakapobidi.
Imetolewa na
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania.

No comments:

Post a Comment