TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Thursday, May 24, 2012

KUTOKA KATIKA MTANDAO WA GAZETI LA MAJIRA


Na Masau Bwire, Ikwiriri

MGOGORO mkubwa uliozuka Ikwiriri, Rufiji, mkoani Pwani kati ya wakulima na wafugaji kwa siku mbili mfululizo na kusababisha uharibifu mkubwa wa mali umemalizika jana.

Utulivu katika eneo la Ikwiriri, umerejea baada ya Mkuu wa Operesheni Maalum za Jeshi la Polisi nchini, SACP Simon Siro, kutumia njia za kidiplomasia kutatua mgogoro huo.

Juzi jioni mwanadiplomasia huyo aliwaita na kukutana faragha kwa mazungumzo ya nini kifanyike ili kuleta amani katika eneo hilo kwa kushirikisha wananchi, viongozi wa dini, wanasiasa, baadhi ya viongozi wa Serikali, wafanyabiashara wakubwa na wazee mashuhuri.

Mazungumzo hayo yaliyodumu kwa zaidi ya saa nne, yalizaa matunda baada ya viongozi hao kukubali kuwatangazia wananchi kuacha vurugu na kuingia katika meza ya mazungumzo kati yao na Jeshi la Polisi ili kurejesha amani kwa njia salama.

Kamanda Siro aliwaambia viongozi hao kuwa, amani ya Ikwiriri haitapatikana kwa mabomu ya machozi au risasi za moto bali kwa njia ya mazungumzo ili kutafuta namna ya kuondoa kasoro zilizojitokeza na kusababisha vurugu hizo.

Viongozi hao walielewa somo la Kamanda Siro na kushiriki kuwaeleza wananchi umuhimu wa kuacha vurugu na kuwasihi washiriki mkutano wa hadhara kati yao na Kamanda Siro ambao ulifanyika jana katika Viwanja vya Africana mjini hapa.

Katika mkutano huo ambao ulihudhuriwa na watu lukuki, wananchi wa pande zote mbili, wafugaji na wakulima walipewa nafasi ya kuzungumza kero zao na zikajadiliwa kwa pamoja chini ya usimamizi wa Kamanda Siro na kupatiwa ufumbuzi.

Wananchi kupitia mkutano huo, walikubaliana kuacha vurugu na kuweka maazimio matano ya nini kifanyike ili vurugu hizo zisijitokeze tena na kuazimia wafugaji warudi katika mipaka yao na wasivuke kuingia maeneo ya wakulima na viongozi wasiotekeleza majukumu yao ipasavyo wawajibishwe.

Maazimio mengine ni kuhusu viongozi, polisi na watendaji wengine wa Serikali wanaojihusisha na rushwa wachukuliwe hatua, wafugaji waliohusika katika mauaji ya mkulima, Bw.Shamte Kawangala (80), wakamatwe na wafikishwe mahakamani.

Azimio lingine ni wananchi 53 waliokamatwa na kufikishwa mahakamani mashtaka yao yachunguzwe kwa kina na wale wasiohusika waachiwe na watakaobainika kuhusika sheria ichukue mkondo wake.

Akizungumza na Majira muda mfupi kabla ya kuondoka na helikopta kutoka eneo la mkutano, Kamanda Siro alisema maazimio yaliyofikiwa katika mkutano huo yameanza kufanyiwa kazi.

Baadhi ya wakazi wa Ikwiriri walipongeza hatua ya Kamanda Siro jinsi alivyoweza kushughulikia mgogoro huo na kuupatia ufumbuzi kwa njia ya mazungumzo na maridhiano ya pamoja.

Rais Jakaya Kikwete (katikati) akimsikiliza Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Rais Kazi Maalum, Profesa, Mark Mwandosya, mara baada ya kumuapisha Ikulu, Dar es Salaam jana, kushoto ni mke wa waziri huyo, Bi. Lucy Mwandosya. (Picha na Charles Lucas)

Na Thomas Dominick

JESHI la Polisi mkoani Mara, limefanikiwa kukamata bunduki nne aina ya Short Gun, SMG na risasi 436 katika kipindi cha wiki mbili baada ya kuwakamata watuhumiwa nane wanaodaiwa kufanya uhalifu na uwindaji katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.

Akizungumza jijini , Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Robert Boaz, alisema jeshi hilo lilipata taarifa za mkazi wa Kijiji cha Bisarara, wilayani hapa Bw. Marwa Makoba (40), kuwa anamiliki silaha hivyo walikwenda kijijini hapo ili kumkamata.

“Baada ya kumkamata, tulifanya upekuzi nyumbani kwake na kupata silaha mbili aina ya SMG na risasi 228, alipofikishwa kituoni tulifanya naye mahojiano kwa kina na kusema anashirikiana na wenzake watano,” alisema Kamanda Boaz.

Aliongeza kuwa, Bw. Makoba aliwataja wenzake kutoka mikoa mbalimbali ambao wakati huo walikuwa mjini Mgumu ndipo polisi walikwenda eneo hilo na kuwakamata.

Aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni, Bw. Fares Nazareti (37), Bw. Erasto Chubwa (46), wakazi wa Bukombe Geita, Magina Bathromeo (36) na Yohana Godfrey (30), wakazi wa Urambo Tabora, Bw. Japhet Bua (28) na Bw. Amosi Kagoma, wakazi wa Kibondo, mkoani Kigoma.

“Tulipofanya nao mahojiano, Bw. Kagoma alikubali kutupeleka nyumbani kwao Kibondo na kuonesha SMG moja, mwingine Bw.  Godfrey alitupeleka Tabora na kuonesha silaha nyingine,” alisema.

Kamanda Boaz alisema, katika tukio jingine ambalo lilitokea Mei 20 mwaka huu, mtu aliyejulikana kwa jina la Bw. Keringo Samara (30), baada ya kupekuliwa nyumbani kwake alikutwa na risasi sita za SMG ambapo jeshi hilo linaendelea kumuhoji ili kujiridhisha kama anaimiliki kihalali.
Na Grace Ndossa

WIZARA ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, inaendelea kufanya ukaguzi katika maeneo yote ya wazi ili kuhakikisha waliovamia maeneo hayo wanaondolewa haraka iwezekavyo.

Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Bw. Goodluck Ole Medeye aliyasema hayo Dar es Salaam juzi wakati akihojiwa katika kipindi cha dakika 45 kinachorushwa na televisheni ya ITV.

Alisema Serikali imeacha maeneo ya wazi kwa ajili ya wananchi kupata sehemu za kukaa wanapopata majanga au hatari yeyote.

“Wizara yangu imeanza kufanya ukaguzi wa maeneo ya wazi katika Wilaya ya Kinondoni ili kuwaondoa wote waliojenga majengo, ukaguzi huu utaendelea mikoani si kwa Dar es Salaam pekee.
“Matumizi ya maeneo ya wazi hayabadiliki, watu wasidanganywe, watu wengi wamejenga hulka ya kuvamia viwanja vya watu, kujenga na kuuza, tukibaini hilo nyumba itabomolewa na muhusika ataondolewa bila serikali kumpa kiwanja kingine,” alisema.

Alisema Wizara hiyo kwa sasa imeboresha nyenzo za kufanyia kazi kwa kutumia teknohama ili waweze kuweka kumbukumbu za ardhi vizuri na kuongeza kuwa, Wenyeviti  na Watendaji wanapaswa kusimamia ardhi zilizopo katika maeneo yao na hawana mamlaka ya kuuza ardhi.

Na Suleiman Abeid, Kishapu

MADIWANI wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu, mkoani Shinyanga, wamefikia azimio la pamoja na kumkataa Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri hiyo, Bw. Theonas Nyamuhanga.
Mbali ya kumkataa Mkurugenzi huyo ambaye hakuwepo katika kikao hicho, pia walimuomba Mkuu wa Polisi wa Wilaya hiyo (OCD), kuhakikisha anamtafuta Bw. Nyamuhanga na kufikishwa katika vyombo vya sheria.
Sambamba na hatua hiyo, madiwani hao pia wameagiza Benki ya NMB, Tawi la Manonga, ishtakiwe kwa kuhusika na upotevu wa fedha za halmashauri sh. bilioni 6.7.
Madiwani hao walifikia uamuzi huo jana katika kikao cha kawaida cha Baraza la Madiwani wakidai kushangazwa kwao na kitendo cha Serikali kushindwa kumchukulia hatua Mkurugenzi huyo.

Kutokana na hali hiyo, madiwani hao wametishia kufunga na kulala nje ya ofisi za Mkurugenzi ili kuhakikisha haingii tena ofisini.
“Ndugu Mwenyekiti, inasikitisha sana, huyu Mkurugenzi leo ni mara ya tatu tumekuwa tukimkataa lakini haondoki,” walisema madiwani hao na kuongeza kuwa, wameguswa na tuhuma mbalimbali zinazomkabili na kama Serikali itashinikiza aendelee na kazi basi, watajiuzulu nyadhifa zao.
Posted: 22 May 2012 11:27 PM PDT

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB Dkt. Charles Kimei, akizungumza nawaandishi wa habari (hawapo pichani) Dar es Salaam jana, kuhusu upanuzi wa huduma kwa wateja wa benki hiyo, kusho ni Naibu Mkururugenzi Mtendaji Uendesha na Huduma kwa Wateja, Bw. Saugata Bandyopadhyay. (Picha na Peter Twite)


No comments:

Post a Comment