TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Wednesday, May 23, 2012

KUTOKA KATIKA MTANDAO WETU WA GAZETI LA MAJIRA,



Mkurugenzi Mwendeshaji wa Bodi ya Utalii Tanzania Dkt. Aloyce Nzuki (katikati), akizungumza na Naibu Waziri wa Utalii wa Afrika Kusini, Bi. Tokozile Xasa, alipotembelea banda la Tanzania, katika maonesho ya utalii ya INDABA yaliyofanyika Durban, Afrika Kusini hivi karibuni. (Na Mpigapicha Wetu)

Mkuu wa Operesheni Maalum za Jeshi la Polisi Tanzania,(SACP), Simon Siro ,(kulia), akishirikiana na mwananchi wa Ikwiriri (jina halikufahamika), kuondoa mawe katika Barabara ya Kilwa, eneo la Ikwiriri, wilayani Rufiji, Mkoa wa Pwani jana, mawe hayo yaliwekwa na wananchi wenye hasira ili kuzuia magari yanayopita wakati wa vurugu kati ya wakulima na wafugaji. (Picha na Masau Bwire)

Waziri wa Maliasili na Utalii Balozi, Khamisi Kagasheki, akiteta na Naibu Waziri wa wizara hiyo, Bw. Lazaro Nyarandu, wakati wa uzinduzi wa Bodi ya Huduma za Wakala wa Misitu (TFS) Dar es Salaam jana. (Picha na Charles Lucas)

Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Bw. Seif Suleiman Rashid (katikati) akiongozana na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Bima ya Afya wa Taifa (NHIF), Bw. Emmanuel Humba na Naibu Mkurugenzi wa mfuko huo, Bw. Hamis Mdee wakati wa ziara ya kuangalia utendaji na kuongea na wafanyakazi wa mfuko huo, Dar es Salaam jana. (Picha na Charles Lucas)

MKAZI wa maeneo ya Kasanga wilayani Morogoro Mkoa wa Morogoro Bw. Lucas Robert (48) amefariki dunia mara baada ya kulipukiwa na taa ya chemli aliyokuwa akiiwasha.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro Bi. Adolphina Chialo tukio hilo lilitokea Aprili 17, mwaka huu, majira ya saa 12.45 alasiri maeneo ya Kasanga na kusababisha kifo chake wakati akipatiwa matibabu katika hospitali ya mkoa.

Hata hivyo, Kamanda huyo alisema chanzo cha tukio hilo kinachunguzwa zaidi.
Wakati huohuo Jeshi la Polisi mkoani Morogoro linaendelea kumfanyia uchunguzi utingo wa gari anaedaiwa kulishwa chakula chenye madawa ya kulevya huko maeneo ya Mikumi wilayani Kilosa.
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi mkoani Morogoro Bi. Adolphina Chialo tukio hilo lilitokea Mei 20, mwaka huu, majira ya saa 10.00 jioni huko maeneo ya Mikumi Wilaya ya Kilosa.
Kamanda Chialo alisema Bw. Ramadhani Salumu (33) ambaye ni dereva wa gari lenye namba za usajili T 509 ARS aina ya Scania Trela, alikuwa akitokea nchini Zambia kuelekea jijini Dar es Salaam na alitoa taarifa kuwa utingo wake aliyefahamika kwa jina Bw. Saimon Mashaka (21) amelishwa chakula kinachodaiwa kuwa na madawa ya kulevya.
Hata hivyo Kamanda huyo alisema utingo huyo amelazwa katika Hospitali ya Mkoa wa Morogoro na uchunguzi zaidi unaendelea kuhusiana na tukio hilo.

Meneja wa Benki ya NBC Tawi la Morogoro Bw. Jasson Shumbusho (kulia),
akikabidhi Hundi ya Sh Mil 5.1, kwa Mkurugenzi wa Kampuni ya Ngoma Afrika Bw. David Kitururu (wa pilia kushoto), kwa ajili ya Tamasha la Paukwa kwa Wanafunzi wa Shule za Msingi za Manispaa ya Morogoro, litakalofanyika Uwanja wa Jamhuri wiki hii. Jumla ya shule 20 zitashiriki. (Picha na Aziz Msuya)

Askari Polisi wa Kikosi cha Usalama Barabarani, akimwelekeza dereva wa gari la polisi namba PT O152 kulisogeza mbele eneo la Mchicha Barabara ya Nyerere Dar es Salaam jana, baada ya kugongwa na daladala (halipo pichani) namba T 342 AWQ, linalosafiri kati ya Gongolamboto na Mwenge. (Picha na Prona Mumwi)
Na Lilian Justice, Morogoro

MWENDESHA pikipiki anaedaiwa kuwa Ofisa Usalama Manispaa ya Morogor mkoani Mrogoro amefariki dunia baada ya kugongana na mwendesha pikipiki mwenzake huko katika maeneo ya Mizani Kihonda katika manispaa hiyo.


Akizungumzia tukio hilo Kamanda wa Polisi mkoani hapa Bi. Adolphina Chialo alisema tukio hilo lilitokea Mei 19, mwaka huu majira ya saa 11.30 jioni huko katika maeneo ya Mizani Kihonda mjini hapa.

Bi. Chialo alisema pikipiki yenye namba za usajili T 699 BFU SUNLG amabayo ilikuwa ikiendeshwa na Bw. Richard Feliciana (35) mkazi wa Chamwino mjini hapa ilikuwa ikitokea Mkundi kuelekea mjini na iligongana na pikipiki nyingine yenye namba za usajili T 281 AQU Honda iliyokuwa ikendeshwa na Bw. Singoli Elia, ambaye alifariki dunia na kudaiwa alikuwa Ofisa Usalama na mkazi wa Forest.

Kwa mujibu wa Kamanda huyo, marehemu alikuwa akitokea maeneo ya mjini kuelekea Mkundi na chanzo cha ajali hiyo kinachunguzwa zaidi.

Hata hivyo, taarifa za awali za Kikosi cha Usalama Barabarani kimebaini chanzo cha ajali hiyo ni marehemu kuendesha pikipiki yake kulia zaidi mwa barabara.

Wakati huohuo, mtembea kwa miguu amefariki dunia mara baada ya kugongwa na gari mali ya Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA) kilichopo mjini hapa.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoani Morogoro Bi. Adolphina Chialo, tukio hilo lilitokea Mei 18 mwaka huu, majira ya saa 12.30 jioni huko maeneo ya Magubike wilayani Kilosa.

Bi. Chialo alisema gari lenye namba za usajili SU 36224 Toyota Land Cruiser ikiendeshwa na Bw. Kassim Urasa (53) mkazi wa Kihonda, ilikuwa ikitokea Mkoani Singida na ilimgonga mtembea kwa miguu Emanueli Godfrey (7), mwanafunzi wa darasa la Kwanza katika Shule ya Msingi Magubike na kufariki dunia papo hapo.

Hata hivyo, Kamanda huyo alisema chanzo cha ajali hiyo ni mwendo kasi wa dereva na uchunguzi zaidi unaendelea.

Shekhe Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhaj, Alhad Salum, akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) Dar es Salaam juzi, mara baada ya kufanyika ibada ya kumbukumbu (Hitma) ya mwaka mmoja tangu kufariki kwa aliyekuwa Mtabiri wa Nyota Afrika Mashariki Shekhe Yahya Hussein. (wa pili kushoto) ni mtoto wa marehemu Bw. Hassan Yahya Hussein na kulia ni mmoja wa maofisa wa taasisi mtabiri huyo, Shekhe, Hamisi Kondo.  (Picha na Charles Lucas)                             
Kaimu Mkurungenzi wa Shirika la (TANESCO),Bw. Boniface Njombe(aliyeinama) akimwonesha Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Bw. Said Mwambungu moja ya kifaa kilichoharibika katika moja ya mashine za kuzalisha umeme na kusababisha kupungua kwa uzalishaji wa umeme katika Mji wa Songea mkoani Ruvuma juzi. Kwa sasa upatikanaji wa nishati hiyo muhimu katika mji wa huo imekua kero kubwa.Picha na kassian Nyandindi

JESHI la Polisi mkoani Morogoro linawashikilia wakazi wawili ambao ni ndugu katika maeneo ya Kihonda Kilimanjaro Manispaa ya Morogoro mkoani humo kwa kosa la kukutwa na nyara za Serikali kinyume cha sheria.

Akizungumzia tukio hilo jana Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro Bi. Adolphina Chialo alisema lilitokea Mei 19, mwaka huu, majira ya saa 9.00
alasiri huko maeneo ya Kihonda mjini hapa.


Alieleza kuwa askari waliokuwa doria waliwakamata Bw. Omari Mohamedi (56), mkazi wa Kilimahewa na Bw. Salumu Mohamed (52) mkazi wa Nunge ambao ni wanandugu wakiwa na ngozi za chui nne kinyume cha sheria huku wakiwa wamezipakia kwenye baiskeli.

Hata hivyo, Kamanda huyo alisema watuhumiwa hao wamekamatwa na thamani ya ngozi hiyo bado haijafahamika kwani uchunguzi maalumu bado unasubiriwa kutoka Idara ya Maliasili kuhusiana na tukio hilo ili kuweza kufanya tathimini halisi ya ngozi hizo.

Wakati huo huo imeelezwa Mei 19, mwaka huu majira ya 12.45 jioni huko maeneo ya Melela, Wilayani Mvomero, mkazi wa eneo hilo Bw. Bakari Rombo (29) ambaye ni mfugaji alitoa taarifa kwa Jeshi la Polisi kuhusu kuibwa kwa ng'ombe wake
watano wenye thamani ya sh. milioni 2.5 wakiwa zizini.

Hata hivyo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro Bi. Adolphina Chialo alisema chanzo cha tukio hilo kinachunguzwa na mpaka sasa hakuna aliyekamatwa kuhusiana na tukio hilo.

No comments:

Post a Comment