TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Saturday, May 26, 2012

SERIKALI YATAKIWA KUJENGA VYUO ZAIDI KWA AJILI YA KUTOA WALIMU WA WATOTO WENYE ULEMAVU

MWANDISHI WETU
 
SERIKALI imetakiwa kujenga Vyuo vitakavyozalisha walimu wakutosha kwa ajili ya watu wenye ulemavu wa ‘Viziwiwasiona’.
Kauli hiyo ilitolewa jijini  Dar es Salaam leo , na Mwalimu wa Kitengo cha walemavu katika shule ya Uhuru Mchanganyiko, Anjelica Mtwale wakati alipokutana Mwakilishi Mkazi wa Shirika la ‘Sense International’ lenye makao yake makuu nchini Uingereza.
Alisema pungufu huo wa walimu maalum umetokana na kukosekana kwa vyuo vya kutosha, ambavyo vingesaidia kutoa taaluma hiyo na kupatikana walimu wengi ambapo wangetumika kutoa elimu kuanzia elimu ya awali hadi elimu ya juu.
Aidha, Anjelica alisema kutokana na baadhi ya wazazi kupata mwamko wa kuwapeleka watoto hao shule kwa ajili ya kupata elimu, bado kitengo chake kinashindwa kumudu kutoa mafunzo  kwa kiwango kinachohitaji kutokana na upungufu huo.
“Unajua katika kuwaelimisha watoto hawa yani Viziwiwasiona kunahitajika walimu wa kutosha kwa kuwa uelimishaji wao ni kwamba kila mtoto mmoja mwalimu mmoja”alisema Mwalimu Anjelica.
Anjelica alisema katika shule hiyo, kuna wanafunzi 13 huku walimu wakiwa 8 na walezi wa kujitolea wanne ambapo kwa utaratibu mzima wa kuwatuza watoto hao hawatoshi.
Akitaja mafanikio tangu kuanzishwa kitengo hicho mwaka 1994, Anjelika alisema wapo watoto waliofanikiwa kupata elimu ya sekondari hadi kidato cha pili, kuishia kidato hicho kumetokana na kukosekana walimu wenye elimu hiyo ya watu maalumu katika shule mbalimbali.
Aidha, Anjelica alitoa shukran kwa shirika la Sense International  kwa kushiriki katika kutoa misaada mbalimbali ya kielimu na afya kwa watoto hao.
Alisema Shirika hilo limekuwa la kwanza nchini katika kujishughulisha katika utoaji wa mafunzo kwa walimu wa watu wa aina hiyo pia limehusika katika kuwapeleka walimu katika mafunzo ndani na nje ya nchi.
Naye Mwakilishi Mkazi wa Shirika hilo, Christopher Andendekisye alisema Shirika hilo limekuwa likifanya shughuli zake kwa kushirikiana na serikali.
Alitoa wito kwa Watanzania kuwafikiria watu hao kwa huruma kwani ni watu wenye ulemavu wakusikitisha, alisema “Hebu fikiria mtu huyo haoni hasikii na hawezi kusema hivyo ni wakati kwa baadhi ya taratibu za upatikanaji wa elimu ya walimu kuekebishwa ili iwe rahisi katika kupatikana walimu  wingi”

No comments:

Post a Comment