TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Thursday, May 24, 2012

MAKAMU WA RAIS DKT. MOHAMMED GHARIB BILAL AMWAKILISHA RAIS KATIKA MKUTANO WA MAENDELEO ENDELEVU AFRIKA JIJINI GABOFRONE, BOTSWANA


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Dkt. Mohammed Gharib Bilal amemwakilisha Rais Jakaya Kikwete katika mkutano wa Maendeleo Endelevu Afrika unaolenga katika kujumuisha thamani ya Rasilimali Asilia katika kupima maendeleo ya kiuchumi katika nchi za Afrika.
Katika mkutano huo, Tanzania imeunga mkono kuanzishwa kwa mfumo wa kujumuisha thamani ya raslimali asilia ambao utahusishwa kwenye tathmini ya pato la taifa kwa manufaa ya vizazi vya sasa na  vijavyo.
Makamu wa Rais alisema wakati akihutubia mkutano huo leo Alhamis Mei 24, 2012 kuwa, mchango wa rasilimali asilia zina nafasi kubwa katika kuchangia katika pato la taifa lakini ili mchango wake utambulike, nchi zinahitajika kuwa na utaratibu wa kuzifanyia tathmini hasa kuhusu matumizi yake na faida zake katika uchumi huku pia athari zake zikitazamwa hasa zile zinazotokana na kupoteza uhalisia wa mazingira ama kuharibu mazingira ya nchi.
“Ni imani ya serikali ya Tanzania kuwa mpango huu utasaidia kutoa nafasi ya nchi kujikagua hasa kwa kuzingatia rasilimali zinazotumika na faida inayopatikana. Tena mpango huu utatoa nafasi kwa nchi kujiuliza kama matumizi ya rasilimali zake yanalenga kutambua faida ya sasa na siku zijazo ili kuhakikisha kuwa mazingira yanabakia kuwa salama kwa ajili ya vizazi vijavyo,” anasema Mheshimiwa Makamu wa Rais Katika hotuba yake.

MAKAMU WA RAIS DKT BILAL AHUDHURIA MKUTANO WA WAKUU WA NCHI ZA AFRIKA KUHUSU MAENDELEO NDANI YA BARA LA AFRIKA GABORONE

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Mohammed Gharib Bilal akiwa katika picha ya pamoja na Wakuu wa Nchi pamoja na wawakilishi  kutoka nchi za Afrika waliohudhuria mkutano wa Maendeleo Endelevu katika Bara la Afrika.(PICHA NA VPO)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Mohammed Gharib Bilal akizungumza na Rais wa Liberia Bibi Ellen Johnson Sirleaf kwenye mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika kuhusu Maendeleo Endelevu Barani Afrika leo mjini Gaborone
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Mohammed Gharib Bilal akihutubia kwenye mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika kuhusu Maendeleo Endelevu katika Bara la Afrika leo mjini Gaborone.

No comments:

Post a Comment