TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Thursday, May 24, 2012

WASHINDI WENGINE WASHINDA ZAWADI NONO ZA SBL, MMOJA ACHOMOKA NA GARI MPYA, WA PILI PIKIPIKI MPYA,HUKU WA TATU AKIIBUKA NA JENERETA MPYA KABISA

 Mkurugenzi wa Masoko wa Kampuni ya bia ya Serengeti Bw. Ephraim Mafuru akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kumpata mshindi wa gari aina ya Ford Figo, Pikipiki na Genereta katika droo ya mwezi ya "Vumbua Dhahabu chini ya Kizibo" inayoendeshwa na kampuni ya bia ya Serengeti, kwenye makao makuu ya kampuni hiyo Oysterbaym kulia ni Mkurugenzi wa Masoko wa kampuni ya Diageo kanda ya Afrika Bi. Cristina Diezhandino na kushoto ni aBakari Maggid Afisa msimamizi wa michezo ya Kubahatisha.
 Mkurugenzi wa Masoko wa kampuni ya Diageo kanda ya Afrika Bi. Cristina Diezhandino akibonyeza kitufe kwenye kompyua ili kuchezesha bahati nasibu kwa ajili ya kupata mshindi wa gari aina ya Ford Figo leo.
Kampuni ya bia ya Serengeti imekuwa ikizunguka katika mikoa mbalimbali hapa nchini kukabidhi zawadi kwa washindi mbalimbali wa promosheni  kubwa na ya kipekee kabisa kutokea hapa nchini Tanzania  ‘VUMBUA HAZINA CHINI YA KIZIBO’ambayo ama kwa hakika inashuhudia watanzania wengi wakinufaika na kupiga hatua mbele kimaisha.
Asubuhi ya leo droo ya nne katika promosheni hiyo ‘VUMBUA HAZINA CHINI YA KIZIBO’ imechezeshwa katika ofisi za kampuni ya bia ya Serengeti SBL zilizopo maeneo ya Oysterbay jijini na kupata kuhudhuriwa na waandishi wa habari, wasimamizi kutoka Bodi ya Bahati Nasibu Tanzania, wadau kutoka ndani na nje ya kampuni hiyo, wakiwemo kampuni ya kuendesha Bahati Nasibu ya PUSH MOBILE, wahakiki na wakaguzi kutoka PWC-Price Water House Coopers.
Kampuni ya bia ya Serengeti kupitia vinywaji vyake aina ya Serengeti premium Lager, Tusker Lager na Pilsner Lager inaendesha promosheni nchi nzima ijulikanayo kama “ VUMBUA HAZINA CHINI YA KIZIBO.’ambapo kwa mara ya kwanza wadau,washiriki na watanzania wote wameshuhudia mmoja wa washindi wa droo ya nne akiibuka na gari mpya aina FORD FIGO huku mwenzake akichomoka na Jenereta mpya.
 Bi. Teddy Mapunda, Mkurugenzi wa mawasiliano na mahusiano wa kampuni ya bia ya Serengeti ( SBL) alikuwa na haya ya kusema“  najisikia furaha sana kuona kila tunapochezesha droo yetu tunapata washindi ambao mpaka sasa tumeshawapata washindi watatu wa jenereta,mshindi mmoja wa pikipiki na washindi wawili wa Bajaj ambapo tayari tumewakabidhi zawadi zao,”alisema Mapunda
“ Bado tunaendelea kuwahamasisha wateja wetu na watanzania wote wenye umri unaruhusu kshiriki katika promosheni hii waendelee kushiriki bila kukata tamaa kwani bado kuna zawadi nyingi sana hadi zifikie milioni 780 kwa zawadi pekeyake  na milioni 380 pesa taslim zinaendelea kushindaniwa.
Washindi wetu katika droo ya nne ni Rogers Kavishe kutoka mkoa wa Kilimanjaro ambaye amejishindia jenereta  kupitia bia ya Serengeti Lager, wa pili ni bw. Oktavian Changula kutoka mkoani Iringa ambaye  amejinyakulia pikipiki mpya kupitia bia ya Tusker lager  wa tatu ni  bw.Isack Juvenari kutoka mkoa wa Morogoro  ambaye amejishindia gari mpya kabisa aina ya FORD FIGO
Kwa upande wake meneja wa bia ya Serengeti bw. Allan Peter Chonjo aliwapongeza washindi wote katika droo hiyo na kuwataka watanzania waendelee kunywa bia za Serengeti ambazo zimeainishwa katika promosheni hiyo ili kuendelea kushinda na hatimaye kupiga hatua katika maisha yao.
Kupitia mawasiliano kwa simu ya mezani mshindi huyo wa gari mpya hakuweza kujieleza kwa mara moja kutoka na hali halisi alioonekana nayo baada ya kupata taarifa ya kushinda gari alipagawa na kupelekea mawasiliano hayo kuyumba kwa muda lakini baadaye aliweza kutulia na kujieleza vizuri.Gari hilo litakabidhiwa kwa mshindi huyo siku chache zijazo.

No comments:

Post a Comment