TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Wednesday, May 23, 2012

MARC, MARAS, MADC WAONYWA KUWA WAADILIFU


WAKUU wa Mikoa, Makatibu Tawala wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya wameonywa juu ya haja ya wao kuwa waadilifu katika nyadhifa walizonazo kwani uongozi wa umma hauwezi kutenganishwa na maadili ya uongozi.
Wito huo umetolewa leo (Jumatano, Mei 23, 2012) katika mada tatu zilizowasilishwa leo kuhusu maadili kwa viongozi wa umma kwenye mafunzo maalum ya siku 10 kwa Wakuu wa Mikoa, Makatibu Tawala na Wakuu wa Wilaya. Mafunzo hayo ambayo leo yamefikia siku ya tatu yanafanyika kwenye ukumbi wa St. Gaspar mjini Dodoma.
Akitoa mada kwa viongozi hao, Kamishna wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Jaji (Mst.) Salome Kaganda alisema uadilifu ni zaidi ya kuzingatia sheria, taratibu na kanuni na akawataka viongozi hao kuonyesha njia kwa matendo na mwenendo mwema ili waweze kuwasimamia watendaji walio chini yao.
Naye Askofu Mkuu Mstaafu, Mhashamu Donald Mtetemelwa aliwataka washiriki wa mafunzo hayo kujiepusha na matumizi mabaya ya mamlaka walinayo kwani wasipofanya hivyo wanaweza kujikuta wakiwaumiza wengi. “Lengo la kiongozi ni kubeba maumivu ya watu na siyo kupeleka maumivu kwa wananchi,” alisema.
Alisema Tanzania kwa sasa inakabiliwa na tatizo la kukosa viongozi wengi walio waadilifu kwa sababu wengi wao wamemuacha Mungu kwa kisingizio cha kuwa na majukumu mengi. “Watu wakipewa madaraka wanajitenga na Mungu, lakini lazima wakumbuke kuwa uadilifu wao utategemea ni kwa kiasi gani wanamcha Mungu,” aliongeza.
 

No comments:

Post a Comment