TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Friday, May 25, 2012

Salim Said Salim:Zanzibar kuna habari nyingi sana

Na Miza Chande-Maelezo Zanzibar 

WAANDISHI wa habari Zanzibar wametakiwa kubadilika katika uandishi wao kwa kuandika habari zinazogusa zaidi maslahi ya jamii badala ya kuandika habari za kupamba viongozi na watu maarufu nchini.

Imefahamika kuwa kuna habari nyingi za kuziandikia zenye maslahi na jamii ya Zanzibar ambazo zitakapojulikana kunaweza kupelekea mabadiliko makubwa katika jamii jambo ambalo litachochea maendeleo na kasi ya uwajibikaji.

Wito huo umetolewa na Mshauri wa Wanahabari Zanzibar Salim Said Salim wakati wa mafunzo ya siku nne iliyofanyika katika ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo Zanzibar, juu ya uandishi bora na namna ya kuzingatia maadili.

Salim amesema miongoni mwa mambo ambayo yamekuwa yakigusa hisia za wazanzibar ni pamoja na uingizwaji wa bidhaa mbovu ambazo zinapelekea wananchi kuwa na shaka katika matumizi na hata kupata maradhi mbalimbali.

Amesema kama waandishi watakuwa wakitekeleza kazi zao vizuri na kuweza kufichua masuala kama hayo Zanzibar haitaweza kuingizwa bidhaa hizo mbovu na wale ambao watafanya hivyo wataweza kufichuliwa na kuchukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria za Nchi.

Hivyo waandishi wa habari ni watu muhimu katika jamii kwani kalamu yao wakiitumia vizuri kwa maslahi ya nchi basin nchi inaweza kupiga hatua za haraka sana na mambo maovu kama hayo na mengineyo hayataweza kutendeka.

Amewasisitiza waandishi kujiamini katika kazi zao kwa kuzingatia maadili ya taaluma yao ambayo ndio muongozo katika kutekeleza kazi zao vizuri bila ya kujali habari hizo imemgusa nani.

Akifunga mafunzo hayo Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo Zanzibar Yussuf Omar Chunda amewataka waandishi hao kutekeleza yale yote waliyoyapata katika mafunzo hayo ili kutoa habari zenye kuvutia.

Amesema kuwa anaamini kuwa Taaluma waliyoipata itasaidia Taifa na kuwajengea hadhi waandishi na taasisi zao ili ziwe zinakubalika na jamii.

Chunda amesema kuwa Idara ya Habari Maelezo Zanzibar itaendelea kutoa mafunzo kwa waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari nchini viwe vya Serikali au binafsi kwani vyombo hivyo vyote ni vya Zanzibar na vinahudumia Wazanzibari hivyo  niwajibu wote kupata elimu ya habari ya kisasa

Mafunzo hayo ni ya pili kutayarishwa na Idara ya habari Maelezo ZanzĂ­bar na yakwanza yalifanyika Jijini Dar es Salaam mwezi wa Machi mwaka huu ambayo yalikuwa yamejikita katika uandishi wa habari za kibiashara na uchumi kwa kushirikiana na Ubalozi wa Uingereza nchini

No comments:

Post a Comment