TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Friday, May 25, 2012

SIMBA ITAKAVYOSHEREHEKEA USHINDI DAR LIVE JUMAPILI

Makamu Mwenyekiti wa Simba SC Geoffrey Nyange ‘Kaburu’, akizungumzia maandalizi ya sherehe hiyo.
 
KLABU ya mpira wa miguu ya Simba leo imezungumzia juu ya sherehe ya ubingwa wa kombe la Tanzania bara 2012 walilolitwaa hivikaribuni.
Akizungumza na waandishi wa habari, Makamu Mwenyekiti wa klabu hiyo, Geoffrey Nyange ‘Kaburu’, alisema maandalizi ya sherehe hiyo tayari yameshakamilika na kinachosubiriwa hadi sasa ni siku husika ambayo ni Jumapili ya wiki hii, tarehe 27.
Alisema wapenzi na mashabiki wa klabu hiyo watatakiwa siku ya Jumapili hii kukusanyika makao makuu ya klabu hiyo, Mtaa wa Msimbazi, asubuhi tayari kwa safari ya kuelekea katika Ukumbi wa Dar Live Mbagala jijini Dar es Salaam, ambapo sherehe hizo zitafanyika.
Mmoja wa waratibu wa sherehe hiyo wa Dar Live, Luqman Maloto (kulia), akielezea jinsi walivyojiandaa kufanikisha sherehe hiyo.
Baadhi ya waandishi wa habari wakifuatilia kwa makini maelezo ya Nyange katika ukumbi wa klabu hiyo uliopo Mtaa wa Msimbazi, Kariakoo, jijini Dar.

No comments:

Post a Comment