TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Wednesday, May 23, 2012

NMB NA SERENGETI ZAICHANGIA TWIGA STARS MILIONI THELATHINI

Katika kuendeleza soka Tanzania, leo hii Benki ya NMB kwa kushirikiana na kampuni ya Bia ya Serengeti imesaidia maandalizi  ya Twiga Stars kwa kutoa  jumla ya shilingi Milioni Thelathini. Pia NMB na Serengeti wamekabidhi vifaa  vyenye  thamani ya Milioni Tano kwa timu hiyo ya Twiga Stars.
Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, Mkuu wa idara ya Masoko na Mawasiliano wa NMB Bw. Imani Kajula alisema; NMB imekua  mbele  katika  kuchangia soka Tanzania, leo hii NMB ikishirikiana na Serengeti tunachangia maandalizi ya Twiga Stars”.
NMB inatambua kuwa Twiga Stars ikiwezeshwa inaweza ikafanya vizuri zaidi. Ili kutimiza lengo hili, NMB Ikiwa ndiyo  benki yenye mtandao mpana wa matawi mengi Tanzania nzima pia imeanzisha akaunti maalum kwa ajili ya kuchangia Twiga Stars. Yeyote atakayeguswa kuchangia Twiga Stars anaweza kuchangia kupitia akaunti namba 22310001185 yenye jina CHANGIA TWIGA STARS ACCOUNT
 Naibu Mkurugenzi wa michezo, Bi. Juliana Yasoda (kulia) akipokea vifaa vya michezo kutoka kwa  Mkurugenzi wa Masoko wa Serengeti, Bw. Ephraim Mafuru (kati) na Mkuu wa Idara  ya  Masoko na Masiliano wa NMB, Bw. Imani Kajula (Kushoto). Wanaoshuhudia  tukio hilo ni Mkurugenzi wa Ufundi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Bw. Sunday Kayuni (pili kushoto) na kocha msaidizi wa Twiga Stars Bi. Nasra Mohamed.

No comments:

Post a Comment