TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Tuesday, September 30, 2014

JAMII ITII SHERIA BILA SHURUTI.

Katika maisha ya kila siku, mwananchi anapaswa kutambua wajibu wake katika jamii ikiwa ni pamoja na kutii Sheria bila shuruti.
Katika maisha ya sasa nchini kumekuwa na vitendo vya ukiukwaji wa Sheria katika jamii na jamii imekuwa ikihusika katika matendo makubwa ya kijinai ambayo ni kinyume na sheria.
Hali hii imekuwa ikitokana na aidha jamii kutojua sheria, na muda mwingine ni kupuuzia tu maagizo na sheria mbalimbali.
Siku za hivi karibuni kumekuwepo na ukatili mkubwa ukitendeka katika jamii kwa kutokea kwa mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi ambapo wasiojua nini maana ya utu kwa makusudi wanakatiza uhai wa maisha ya binadamu wenzao na wengine kuwakata baadhi ya viungo vyao kwa tamaa ya kujipatia fedha pamoja na imani za kishirikina.
Jamii sio tu inaelewa kuwa kumdhuru mtu ni kosa la jinai bali pia jamii inatambua kuwa kuua pia ni kosa kubwa la jinai ambapo katika Sheria ya Kanuni ya adhabu Sura ya 16 kifungu cha 197 kimeeleza jinsi ambavyo kosa la kuua kwa kukusudia linamgharimu mtu adhabu ya kifo, lakini licha kuwepo kwa sheria hiyo, bado jamii inajihusisha na makosa ya kuua kila kukicha.
Katika mikoa ya Kanda ya Ziwa Victoria, suala la mauaji ya watu wenye Ualbino limekuwa ni tatizo kubwa kwani mauaji haya yanafanyika katika mazingira tu ya watu kuwa na imani potofu za kuukwaa utajiri wa haraka haraka.
Wakili wa kujitegemea Bwana Edwin Webiro anaeleza kuwa watu wengi wanafahamu kuwa kuua ni kosa kubwa lenye adhabu ya kifo ama kifungo cha maisha, bado watu hao hawajali juu ya uwepo wa Sheria ya kunyonga kwasababu wamekuwa wakiiona haitekelezwi ipasavyo, jambo linalowafanya wao waone ni haki kwao kufanya unyama wowote kwa watu wasio na hatia (watu wenye ulemavu).
Katika hali nyingine jamii pia imekuwa ikikiuka Sheria na kusababisha madhara makubwa pale ambapo ajari nyingi zimekuwa zikitokea mfululizo hivi karibuni na kusababisha vifo na kuacha ulemavu wa kudumu wa jamii.
Ajali hizi zimekuwa zikisababishwa na uzembe wa baadhi ya madereva wa mabasi pamoja na magari madogo kwani kumekuwa na ukiukwaji wa Sheria za barabarani ambapo kwa makusudi madereva hao wamekuwa wakikiuka sheria mbalimbali na kufanya mambo yanayosabisha ajari.
Sheria ya Usalama barabarani Sura ya 168 Kifungu cha 44 Inazuia mtu kuendesha chombo cha moto akiwa ametumia kilevi, lakini Sheria hii inajulikana vema kwa madereva lakini kwa makusudi hawaijali wala kuizingatia na badala yake wamekuwa wakitumia kilevi kabla ama wakati wakiwa wanaendesha vyombo vya moto.
Swali la kujiuliza ni kwamba, kwanini madereva wamekuwa wakitumia kilevi wakiwa wanaendesha magari?
Josephat Munishi ni Dereva wa daladala moja linalofanya safari zake Jijini Dar es Salaam anaeleza kuwa kutumia kilevi wakati wa kuendesha gari ni kosa kisheria.
“Muda mwingine kilevi kinakupa nguvu na kujihisi kutochoka na unapata hamasa ya kuendesha gari, kama unavyojua kazi yetu ni ngumu kutwa nzima unasumbuana na abiria, sasa bila kinywaji kidogo hauwezi pata nguvu ya kufanya kazi’’, alisema Munishi.
Jamii kwa mara nyingeine imekuwa ikikiuka Sheria na kujikuta katika maovu makubwa ambapo baadhi ya wasichana wamekuwa wakijihusisha na utoaji mimba (Abortion)kinyume na Sheria.
Kwa hali ilivyo sasa wasichana wadogo hasa wanafunzi na hata watu wazima wamekuwa wakijihusisha sana na utoaji mimba kinyume na sheria huku wengi wao wamekuwa ni wale ambao wamepata mimba hizo katika mazingira ambayo hawakutegema.
Watoto wengi wa kike wamekuwa wakijihusisha na mapenzi wakati bado wakiwa shule, na pindi wanapojigundua kuwa wana ujauzito njia pekee ambayo wanahisi ni bora kuepukana na matatizo hayo wamekuwa wakitoa mimba, kitu ambacho ni kinyume na Sheria za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Katika kifungu cha 219 Cha Sheria ya Kanuni ya adhabu Sura ya 16, kinaeleza wazi kuwa kitendo cha kuharibu ujauzito ambao unapelekea kukatisha maisha ya mtoto ambaye angezaliwa, ni kosa la jinai lakini sababu kubwa ambayo wamekuwa wakiitoa wanawake wengi ni kuwa mimba hizo zinakuwa ni zile ambazo hazikupangwa kutokea (unplanned pregnancy).
Jamii inapaswa kuzingatia Sheria mbalimbali na iepuke kutoa sababu na visingizio za kutojua sheria hizo, kwani ni vema kutii sheria bila shuruti kama vyombo vyetu vya Usalama vinavyotutaka.

No comments:

Post a Comment