WANACHAMA 75 kutoka Chama Cha 
Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Kata ya Msasani Jimbo la Kawe akiwemo 
Katibu Mwenezi wa Baraza  la Wanawake Chadema Kawe  (BAWACHA) wamejiunga
 na chama cha Alliance for Change and Transparent (ATC-Tanzania).
Hayo yamebainishwa na Mwenyekiti
 wa ACT-Tanzania Mkoa wa Dar es Salaam Khamis Chambuso wakati 
akiwakabidhi kadi za chama hicho leo jijini Dar es Salaam.
Chambuso alisema wanachama hao 
pamoja na wanachama wengine kutoKA Chama Cha Mapinduzi (CCM) na CHAUMA 
wamejiunga na ACT- Tanzania kwa mapenzi yao bila kushawishi na kitu 
chochote.
Alisema kwa siku jana wamepokea 
wanachama 78 ambapo mmoja anatokea mkoa wa Kigoma na wengine wanatokea 
mkoa wa Dar es Salaam wengi wao wakiwa ni kutoka CHADEMA.
“Kimsingi tunajisikia faraja 
kuona Watanzania waliowengi wanaanza kutambua umuhimu wetu na wameamua 
kujiunga na ACT- Tanzania hivyo wanatuongeza nguvu ya kufanya mabadiliko
 ya nchi”, alisema.
Alisema ACT-Tanzania kina 
dhamira yua kweli ya kuhakikisha kuwa mfumo mzima wa nchi unabadilika 
ikiwa nin pamoja na kushirikisha jamii ya Watanzania inafaidika na 
rasilimali zilizopo hapa nchini.
Chambuso alisema ACT- Tanzania 
haijaja kwa ajili ya kubomoa vyama vingine ila misingi yake ndio chanzo 
cha watu kutoka vyama mbalimbali kuhitaji kujiunga nao.
Mwenyekiti huyo aliwataka 
wachama hao wapya kuhakikisha kuwa ni sehemu ya mafanikio ya 
ACT-Tanzania kwa kuongeza wanachama zaidi.
Kwa upande wake Mhandisi 
Mohammed Ngulangwa ambaye ni kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa  siku 
nyingi tangu mwaka 1997 alisema kilichomuondoa CCM ni chama hicho 
kushindwa kutekeza sera zake.
Ngulagwa ambaye mwaka 2010 
aliingia katika kinyang’anyiro cha kugombea Ubunge ndani ya chama Jimbo 
la Temeke alisema kimsingi chama cha ACT-Tanzania ndicho chenye misingi 
sahihi ya kidemokrasia.
Alisema juhudi zake katika siasa
 atazionyesha kwa nguvu zote ili kuhakikisha kuwa chama hicho kipya 
kinafanya vizuri katika medani za siasa hapa nchini.

No comments:
Post a Comment