Naibu  Katibu Mkuu Wizara ya Mawasiliano Sayansi na Teknolojia, John Mgodo akizungumza katika uzinduzi huo.
 Mtaalamu wa mradi huo kutoka Kampuni ya Nokia, Riita Vanska. (Imeandaliwa na mtandao wa www.habari za jamii.com-simu namba 0712-727062)
 Meneja
 Mkuu wa Tigo, Diego Gutierrez akizungumza katika uzinduzi huo. Kampuni 
ya Tigo, Nokia na Microsoft ndio wadau  mpango huo.
Meneja Mawasiliano wa Microsoft Mobile Devices, Lilian Nganda akitoa neno la ukaribisho kwa wageni waalikwa.
 Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Sayansi na 
Teknolojia Dk.Hassan Mshinda akizungumza katika 
uzinduzi huo.
 Viongozi mbalimbali wakiwa meza kuu wakati wa uzinduzi huo.
 Naibu
  Katibu Mkuu Wizara ya Mawasiliano Sayansi na Teknolojia, John Mgodo 
(katikati), akiangalia simu wakati akiwaelekeza namna ya kutumia simu 
wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Azania,  Peter Riima (kushoto) na 
Mrashani Katebeleza, wakati wa uzinduzi wa Programu ya kuwawezesha 
wanafunzi kujifunza somo la hisabati kwa kutumia simu za mkononi na 
vifaa vingine vya kielektroniki Dar es Salaam leo. Kulia ni Meneja Mkuu 
wa Tigo, Diego Gutierrez.
 Hapa uzinduzi huo ukifanyika.
 ‘ Ni kama anasema’ Niacheni nipo kazini nachukua tukio hili nikawahabarishe wengine, chezea mimi nyiee
 Wadau mbalimbali na wanahabari wakiwa kwenye 
hafla hiyo ya uzinduzi.
Wadau na wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana wa Jangwani wakiwa kwenye uzinduzi huo.
Dotto Mwaibale
WANAFUNZI
 nchini wametakiwa kutumia mitandao hasa ya simu za mikononi kwa ajili 
ya kujifunzia masomo mbalimbali badala ya kutumia katika matumizi 
yasiofaa.
Mwito
 huo umetolewa na Naibu  Katibu Mkuu Wizara ya Mawasiliano Sayansi na 
Teknolojia, John Mgodo wakati wa uzinduzi wa Programu ya kuwawezesha 
wanafunzi kujifunza somo la hisabati kwa kutumia simu za mkononi na 
vifaa vingine vya kielektroniki uliofanyika Dar es Salaam leo.
Alisema
 progamu hiyo imefika wakati muafaka na itawasaidia wanafunzi kujifunza 
somo hilo muhimu katika ulimwengu wa sayansi na teknolojia.
Alisema
 programu hiyo imeletwa nchini na Kampuni ya Nokia, Tigo kwa 
kushirikiana na Microsoft,  ambapo serikali kupitia Tume ya Taifa ya 
Sayansi na Teknolojia (Costech) inasimamia kwa karibu mpango huo.
Alisema
 Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi katika programu hiyo imesaidia 
kupata mahudhui ya kihisabati jambo litakalo wasaidia wanafunzi kuwa 
makini kitaaluma.
Alisema
 matumizi hayo ya simu katika kujifunza hisabati yatakuwa yakifanyika 
katika muda wa ziada baada ya masomo kwa vile licha ya wanafunzi 
kumiliki simu lakini hawaruhusiwi kuwa nazo mashuleni.
Mgodo alisema mpango huo kwa sasa upo katika majaribio ukifanikiwa wanaweza kuuingiza katika mitaala ya taifa.
Mtaalamu
 wa mradi huo kutoka Kampuni ya Nokia, Riita Vanska alisema mpango huo 
umekuwa ukiongeza weredi kwa wanafunzi katika somo la hisabati na ni 
muhimu katika kipindi hiki cha maendeleo ya Sayansi na Teknolojia.
Mkurugenzi
 Mkuu wa Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia Dk.Hassan Mshinda 
alisema tume hiyo ilifanyamchakato na kuukubali mpango huo ambao ni 
muhimu hasa katika kipindi hiki ambacho taifa linaupungufu mkubwa wa 
wataalamu wa sayansi wanaotokana na kufaulu kwa somo la hisabati.
“Mradi huu tuliona unafaa kwani utasaidia kuongeza wanasayansi hivyo tuliupokea kwa mikono miwili” alisema Dk.Mshinda.
No comments:
Post a Comment