TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Wednesday, October 1, 2014

Idadi ya watu walioathirika na ulaji wa chakula na unywaji wa togwa katika Kijiji cha Litapwasi yamefikia 325.

index
Kipimo Abdallah
 
IDADI ya watu walioathirika na ulaji wa chakula na unywaji wa togwa katika Kijiji cha Litapwasi  Kata Mpitimbi Wilaya ya Songea Vijijini Mkoa wa Ruvuma imefikia 325.
 
Kati ya hao hadi tunakwenda mitamboni jana jioni watu 100 bado walikuwa wamelazwa ambapo 29 walikuwa katika hospitali ya Peramiho na wengine 71 walikuwa wamelazwa katika kituo maalum katika shule ya Msingi ya Kiwalawala.
 
Akizungumza na mwandishi wa gazeti hili kwa njia ya simu jana, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma, Kamishna Msaidizi wa Polisi Mihayo Msikhela alisema hadi kufikia jana watu 225 waliokumbwa na kadhia hiyo walikuwa wameruhusiwa kutoka kwenye vituo vya matibabu.
 
Kamanda Msikhela alisema tukio hilo lilitokea katika sherehe ya kipaimara juzi jumapili kijijini Litapwasi na  limeacha majozi kwa watu wengi pamoja na ukweli kuwa hamna mtu aliyepoteza maisha hadi sasa.
Msikhela alisema wataalamu wa afya wanaendelea kuwapatia matibabu waathirika hao ili kuhakikisha kuwa wanapata nafuu wote na kurejea majumbani mwao.
Kamanda huyo alisema hadi sasa wamewashikilia watu watano ambao wanasadikiwa kuhusika na tukio hilo ambapo mmoja wapo ni baba wa mtoto aliyekuwa anafanyiwa sherehe, Enes Nungu ambaye pia ni mwathirika.
 
Msikhela alisema vyakula na vimiminika vingine ambavyo vilivyohusika vitafikishwa Dar es Salaam kwa Mkemia Mkuu wa Serikali kwa uchunguzi zaidi ambapo majibu yake yatakuwa na mwanga wa kuwaongoza kwenye uchunguzi wao.
 
Katika tukio jingine, Kamanda huyo alisema mwanachi mmoja aliyejulikana kwa jina la Nicolaus Pokela amekutwa amekufa nje ya nyumba ya mdogo wake Gidion Pokela baada ya kunywa sumu ambayo hutumika kuuwa wadudu wanaharibu kahawa.
 
Kamishna Msaidizi alisema taarifa za awali zinaonyesha kuwa marehemu alikuwa anatuhumiwa kuchoma nyumba ya mkewe ambaye walikuwa na ugomvi.
 
Pia Kamishna Msaidizi alisema jana majira ya saa tatu usiku vijana wawili waliuwawa na wananchi baada ya kuiba pikipiki na kukimbia nayo ambapo mmoja wao alinusurika na kukimbia kusikojulikana
 
Msikhela alitoa wito kwa wananchi kuacha tabia ya kuchukua sheria mkononi kwani kufanya hivyo ni uvunjifu wa sheria za nchi na kuwataka watoe taarifa Polisi pindi wakiwakamata watuhumiwa.

No comments:

Post a Comment