TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Friday, October 3, 2014

Makaa ya Mawe ya Ngaka kuanza kutumika kupikia


169Mtaalamu wa viwango kutoka mgodi wa Ngaka, Boscow Mabena akionyesha tofali maalumu (briquette) zilizobuniwa na mgodi huo kwa ajili ya matumizi ya kupikia majumbani na katika taasisi. Tofali hizo zina uwezo wa kuwaka kwa zaidi ya saa nne.
………………………………………………………………
Na Mohamed Saif – Mbinga
Mgodi wa Makaa ya Mawe wa Ngaka uliopo wilayani Mbinga mkoani Ruvuma upo mbioni kuanza kuuza makaa yanayozalishwa na mgodi huo kwa ajili ya matumizi ya kupikia katika taasisi na majumbani.
Hayo yalielezwa hivi karibuni na Mtaalamu wa Viwango katika mgodi huo, Boscow Mabena alipokuwa akizungumza na ujumbe kutoka Wizara ya Nishati na Madini uliofanya ziara mgodini hapo kwa lengo la kufanya ukaguzi wa kimazingira.
Mabena alieleza kuwa utafiti wa kupunguza joto katika Makaa hayo ili kuweza kutumika kwa ajili ya kupikia umefanywa kwa kushirikiana na kikundi cha kina Mama cha Mbarawala Women Group kilichopo wilayani humo pamoja na Chuo cha VETA- Ruvuma.  
Aliongeza kuwa utafiti huo umefanyika kwa kipindi kirefu na tayari umekamilika na hivi sasa kinachosubiriwa ni kibali kutoka Shirika la Viwango Tanzania (TBS) ili makaa hayo yaanze kuuzwa.
Mtaalamu huyo alieleza kuwa wamebuni tofali maalumu (briquette) kutokana na makaa hayo ambazo zitatumika kwa ajili ya matumizi ya kupikia kwa kutumia majiko maalumu ambayo yamebuniwa na wataalamu kutoka Chuo cha VETA.
Aidha, alibainisha kuwa tofali moja la mkaa huo (briquette) lina uwezo wa kuwaka kwa saa zisizopungua nne na hivyo kumuwezesha mtumiaji kupika vyakula mbalimbali kwa kutumia tofali kimoja.
Kuhusu suala la bei, Mabena alifafanua kuwa kila tofali litauzwa kwa kuanzia shilingi mia mbili na majiko yatatofautiana bei kulingana na mahitaji ya mtumiaji. “Unajua kuhusu jiko, inategemea mtu anahitaji jiko la namna gani, kuna majiko makubwa ya taasisi na pia madogo, hivyo mteja atatuambia anahitaji jiko la namna gani maana tuna uwezo wa kumjengea jiko maalumu lisilohamishika,” alisema.
Mabena alisema matumizi ya mkaa huo yanatazamiwa kupunguza uharibifu wa mazingira hususan ukataji hovyo wa miti kwa ajili ya mkaa na kuni.
Alieleza kuwa, tayari taasisi mbalimbali zimeonyesha nia ya kutumia majiko hayo. Mtaalamu huyo alizitaja baadhi ya taasisi kuwa ni Magereza wilayani Songea pamoja na Chuo cha Ualimu cha Songea. “Tulikuwepo siku ya Maonesho ya Nane Nane hapo Songea na wananchi wengi walivutiwa na mkaa huu na hii ilitusaidia tushike nafasi ya kwanza kwa ubunifu,” aliongeza.

No comments:

Post a Comment