Mgombea
 wa Urais wa Msumbiji kupitia chama cha FRELIMO Mh.Filipe Nyusi akipokea
 zawadi kutoka kwa Jumuiya ya watu wa Msumbiji wanaoishi Zanzibar.
Mgombea
 wa Urais wa Msumbiji kupitia chama cha FRELIMO Mh.Filipe Nyusi 
akizungumza na Wananchi wa Msumbiji wanaoishi Tanzania ambapo alitumia 
fursa hiyo kuwaomba wampigie kura kwani amekuja na mikakati mizuri ya 
kuboresha uchumi ambapo amedhamiria kuiondoa Msumbiji kwenye orodha ya 
nchi masikini,pia aliahidi kuwawezesha wakina Mama wa Msumbiji.
Wananchi
 wa Msumbiji wanaoishi Zanzibar wakisikiliza sera za Mgombea wa Urais wa
 Msumbiji kupitia chama cha FRELIMO Mh.Filipe Nyusi kwenye mkutano 
uliofanyika katika Hotel ya Zanzibar Beach Resort.
Mgombea
 wa Urais wa Msumbiji kupitia chama cha FRELIMO Mh.Filipe Nyusi 
akiongozana na Mwenyekiti wa Jumuiya ya watu wa Msumbiji wanaoishi 
Zanzibar Asilia Lunji baada ya kumaliza mkutano wake wa kampeni kwa 
wapiga kura wanaoishi Zanzibar,Nyusi aliwaambia kuwa amefanya mkutano wa
 kwanza nchini Tanzania kwa sababu ya mahusiano mazuri baina ya Msumbiji
 na Tanzania




No comments:
Post a Comment