Mahmoud Ahmad Arusha
Sakata la kuhamisha makaburi lachukuwa sura mpya baada ya KAMATI ya kusimamia makaburi ya waislamu yaliyopo eneo la Levolosi jijini Arusha, kusisitiza kuwa haijafanya mazungumzo yeyote na halmashauri ya jiji la Arusha, kuhusu kufukuliwa kwa makaburi hayo yaliyopo eneo la Levolosi na badala yake kujengwa kituo kikubwa cha mabasi madogo yanayotoa huduma zake jijini Arusha na maeneo ya jirani, Daladala.
Mwenyekiti wa kamati hiyo, Ustaadhi Omari Bokolo, akizungumza kwenye eneo la makaburi hayo amesema eneo hilo halijabadilishwa matumizi na wala hawana mpango huo wa kubadili matumizi ya eneo hilo kwa sasa .
Sakata la kuhamisha makaburi lachukuwa sura mpya baada ya KAMATI ya kusimamia makaburi ya waislamu yaliyopo eneo la Levolosi jijini Arusha, kusisitiza kuwa haijafanya mazungumzo yeyote na halmashauri ya jiji la Arusha, kuhusu kufukuliwa kwa makaburi hayo yaliyopo eneo la Levolosi na badala yake kujengwa kituo kikubwa cha mabasi madogo yanayotoa huduma zake jijini Arusha na maeneo ya jirani, Daladala.
Mwenyekiti wa kamati hiyo, Ustaadhi Omari Bokolo, akizungumza kwenye eneo la makaburi hayo amesema eneo hilo halijabadilishwa matumizi na wala hawana mpango huo wa kubadili matumizi ya eneo hilo kwa sasa .
Amesema kuwa eneo hilo la 
makaburi sio mali ya halmashauri ya jiji la Arusha kama ilivyodaiwa.bali
 eneo hilo linamilikiwa mtu binafsi ambae ni marehemu Said Sela Said 
tangia mwaka 1940, ambae kabla hajafariki aloilitoa wakfu kwa waislamu 
watakaokuwa wakifariki jijini Arusha  kuzikwa hapo .
Ustaadhi Bokolo, amesema kamati hiyo ya kusimamia makaburi ya waislamu katika jiji la Arusha, imeshutushwa na tamko la mkurugenzi wa jiji la Arusha Idd Juma, alilolitoa mwishoni mwa wiki kuwa tayari ameshazungumza na viongozi wa kiislamu na kukubaliana eneo hilo kubadilishwa matumizi kutoka makaburi na kujengwa kituo cha daladala.
Ustaadhi Bokolo, amesema kamati hiyo ya kusimamia makaburi ya waislamu katika jiji la Arusha, imeshutushwa na tamko la mkurugenzi wa jiji la Arusha Idd Juma, alilolitoa mwishoni mwa wiki kuwa tayari ameshazungumza na viongozi wa kiislamu na kukubaliana eneo hilo kubadilishwa matumizi kutoka makaburi na kujengwa kituo cha daladala.
Amesema kamati inazo nyaraka 
zote za tangia mwaka 1940 hadi leo na kuutaka uongozi wa halmashauri ya 
jiji kurejea kwenye kumbu kumbu ili kuelewa umiliki halali wa eneo hilo 
.Amesema kuwa mwaka 2006 baada ya kutokea mgogoro wa  umiliki kutokana 
na mbinu chafu zilizofanywa na baadhi ya watendaji wa halmashauri hiyo 
kwa kushirikiana na baadhi ya madiwani, kamati hiyo ilimwandikia waziri 
wa Ardhi wakati huo, Dakta John Magufuli, ambae alithibitisha kuwa eneo 
hilo haikuwa mali ya halmashauri ya manispaa ya Arusha kwa wakati huo na
 kuitaka kamati hiyo kuliendeleza .
Ameongeza kuwa mwaka 2013 waziri
 wa Ardhi ,Profesa Anna Tibaijuka, katika mlolongo huo aliiagiza 
halmashauri ya jiji la Arusha kukaa  na kamati hiyo kutatua mgogoro huo 
lakini hilo halijawahi kufanyika  na badala yake halmashauri ya jiji 
inatangaza kubadilisha matumizi ya eneo hilo.
Wajumbe wa kamati hiyo wamehoji 
 uhalali wa halmashauri kumiliki eneo hilo sanjari na kushangazwa na 
hatua ya kutaka kujenga kituo cha daladala kati kati ya jiji badala ya 
huduma hiyo kujengwa maeneo ya pembezoni ambayo hayana msongamano na 
wakaitaka halmashauri kusitisha mara moja mpango huo vinginevyo 
wataiburuza mahakamani .
Mwishoni mwa wiki mkurugenzi wa 
jiji ,Idd Juma, amesema kuwa wanakusudia kubadili matumizi ya eneo hilo 
kutoka makaburi na kujengwa kituo cha daladala ili kuondoa msongamano  
wa daladala katikati ya jiji la Arusha.
No comments:
Post a Comment