Mbunge wa Kawe Mh. Halima Mdee ambaye pia ni Mwenyekiti wa BAWACHA taifa.
……………………………………………………………..
Kipimo Abdallah
ALIYEKUWA Katibu Mwenezi wa 
Baraza la Wanawake Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (BAWACHA) Jimbo la 
Kawe, Batuli Kivuma ambaye amejiunga na chama cha Alliance for Change 
and Transparent (ACT-Tanzania amesema kilichomuondoa CHADEMA ni ukabila 
ulioota mizizi kwa muda mrefu.
Kivuma ambaye awali alikuwa 
mwanachama wa Chama Cha Wananchi CUF alisema aliamini kuwa chama hicho 
kinasimamia demokrasia jambo ambalo limeshindikana hasa ukiwa hotekei 
mkoa wa Kilimanjaro.
Alisema tangu ajiunge katika 
chama hicho amekuwa na juhudi za kukijenga chama hasa Kata ya Msasani na
 jimbo zima la Kawe ila juhudi zake zimekuwa zikikwamishwa kwa misingi 
ya ukabila.
Katibu Mwenezi huyo wa zamani wa
 BAWACHA alisema katika kudhihirisha hilo alishiriki kwenye  mchakato wa
 kugombea nafasi ya Udiwani viti maalum mwaka 2010 ambapo alishinda ila 
aliondolewa kwa kigezo cha yeye ni Mdigo na wakapewa nafasi hiyo 
Wachaga.
“Kusema ukweli suala la kuhama 
vyama sio zuri ila inafikia mahali unashindwa kuvumilia kwani nimekuwa 
nikionewa mara kwa mara katika chaguzi na ukiangalia vizuri msingi wake 
ni ukabilia ambao unawabeba Wachaga” , alisema.
Kivuma  alisema alikuwa 
akikipenda sana chama hicho lakini ubaguzi uliopo amefikia mwisho wa 
uvumilivu na kwamba anahitaji kuonyesha jitihada zake kwingine.
Alisema suala hilo la ukabila 
lilikidhiri katika uchaguzi mkuu ambao ulifanyika hivi karibuni hasa 
katika upande wa BAWACHA ambapo juhudi zilifanywa kuanzia ngazi ya chini
 hadi Taifa.
Mwenezi huyo wa zamani wa 
BAWACHA alisema hata upatikanaji wa Mwenyekiti wa BAWACHA wa sasa Halima
 Mdee ulitawaliwa na ukabila ikiwa ni agizo la Mwenyekiti Taifa Freeman 
Mbowe.
“Unajua hili neno demokrasia 
wanalielewa je bwana kwani kwa ufahamu wangu ni kuhakikisha kuwa jamii 
inaacha pale inapofanya maamuzi yake ila huku ni kinyume”, aliongezea 
Kivuma.
Kivuma alisema atahakikisha kuwa anakibomoa CHADEMA hasa katika Jimbo la Kawe ambapo amefanya kazi za kisiasa kwa muda mrefu.
Kwa upande wake aliyekuwa Mjumbe
 wa Mtaa Serikali ya Mtaa wa Matofalini Ujiji Kigoma Yassin Mohamed 
alisema ni vema vyama vikatambua kuwa hakuna uadui baina yao na kuhama 
chama ni haki ya mtu.
Alitolea mfano hali ya kisiasa 
ilivyokuwa siku za nyuma kati ya chama na CHADEMA na CUF hali ambayo kwa
 sasa haipo na vinafanya kazi pamoja.
Mohamed alisema ameamua kujiunga na ACT-Tanzania na kuondoka CHADEMA ili kupata uhuru wa kupigania demokrasia ya kweli.

No comments:
Post a Comment