TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Wednesday, October 1, 2014

Katibu Mwenezi (BAWACHA) Kawe ajiunga na ACT

index
Mbunge wa Kawe Mh. Halima Mdee ambaye pia ni Mwenyekiti wa BAWACHA taifa.
……………………………………………………………..
Kipimo Abdallah
ALIYEKUWA Katibu Mwenezi wa Baraza la Wanawake Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (BAWACHA) Jimbo la Kawe, Batuli Kivuma ambaye amejiunga na chama cha Alliance for Change and Transparent (ACT-Tanzania amesema kilichomuondoa CHADEMA ni ukabila ulioota mizizi kwa muda mrefu.
Kivuma ambaye awali alikuwa mwanachama wa Chama Cha Wananchi CUF alisema aliamini kuwa chama hicho kinasimamia demokrasia jambo ambalo limeshindikana hasa ukiwa hotekei mkoa wa Kilimanjaro.
Alisema tangu ajiunge katika chama hicho amekuwa na juhudi za kukijenga chama hasa Kata ya Msasani na jimbo zima la Kawe ila juhudi zake zimekuwa zikikwamishwa kwa misingi ya ukabila.
Katibu Mwenezi huyo wa zamani wa BAWACHA alisema katika kudhihirisha hilo alishiriki kwenye  mchakato wa kugombea nafasi ya Udiwani viti maalum mwaka 2010 ambapo alishinda ila aliondolewa kwa kigezo cha yeye ni Mdigo na wakapewa nafasi hiyo Wachaga.
“Kusema ukweli suala la kuhama vyama sio zuri ila inafikia mahali unashindwa kuvumilia kwani nimekuwa nikionewa mara kwa mara katika chaguzi na ukiangalia vizuri msingi wake ni ukabilia ambao unawabeba Wachaga” , alisema.
Kivuma  alisema alikuwa akikipenda sana chama hicho lakini ubaguzi uliopo amefikia mwisho wa uvumilivu na kwamba anahitaji kuonyesha jitihada zake kwingine.
Alisema suala hilo la ukabila lilikidhiri katika uchaguzi mkuu ambao ulifanyika hivi karibuni hasa katika upande wa BAWACHA ambapo juhudi zilifanywa kuanzia ngazi ya chini hadi Taifa.
Mwenezi huyo wa zamani wa BAWACHA alisema hata upatikanaji wa Mwenyekiti wa BAWACHA wa sasa Halima Mdee ulitawaliwa na ukabila ikiwa ni agizo la Mwenyekiti Taifa Freeman Mbowe.
“Unajua hili neno demokrasia wanalielewa je bwana kwani kwa ufahamu wangu ni kuhakikisha kuwa jamii inaacha pale inapofanya maamuzi yake ila huku ni kinyume”, aliongezea Kivuma.
Kivuma alisema atahakikisha kuwa anakibomoa CHADEMA hasa katika Jimbo la Kawe ambapo amefanya kazi za kisiasa kwa muda mrefu.
Kwa upande wake aliyekuwa Mjumbe wa Mtaa Serikali ya Mtaa wa Matofalini Ujiji Kigoma Yassin Mohamed alisema ni vema vyama vikatambua kuwa hakuna uadui baina yao na kuhama chama ni haki ya mtu.
Alitolea mfano hali ya kisiasa ilivyokuwa siku za nyuma kati ya chama na CHADEMA na CUF hali ambayo kwa sasa haipo na vinafanya kazi pamoja.
Mohamed alisema ameamua kujiunga na ACT-Tanzania na kuondoka CHADEMA ili kupata uhuru wa kupigania demokrasia ya kweli.

No comments:

Post a Comment