Mawaziri
 wanaoshughulikia Nishati kutoka nchi za Zambia, Tanzania na Kenya 
wakisaini Mkataba wa Makubaliano kuonesha dhamira ya Serikali ya nchi 
hizo kujenga miundombinu ya pamoja ya kusafirisha umeme na kufanya 
biashara ya kuuziana umeme wa ziada baina ya nchi hizo. Mkataba huo 
umesainiwa jijini Dar es Salaam leo na Waziri wa Nishati na Madini 
Tanzania, Profesa Sospeter Muhongo (katikati), Waziri wa Wizara ya 
Migodi, Nishati na Maendeleo ya Maji wa Zambia , Christopher Yaruma 
(kushoto) na Waziri wa Nishati na Petroli Kenya , Davis Chirchir (kulia)
 . Wanaoshuhudia kutoka kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Migodi , 
Nishati na Maendeleo ya Maji Zambia, Charity Mwansa, Katibu Mkuu Wizara 
ya Nishati na Madini , Tanzania , Eliakim Maswi na Katibu Mkuu Wizara ya
 Nishati na Petroli Kenya, Mhandisi Joseph Njoroge.
Mawaziri
 wanaoshughulikia Nishati kutoka nchi za Zambia, Tanzania na Kenya , 
Waziri wa Wizara ya Migodi, Nishati na Maendeleo ya Maji wa Zambia , 
Christopher Yaruma (kushoto) Waziri wa Nishati na Madini , Profesa 
Sospeter Muhongo Tanzania (katikati) na Waziri wa Nishati na Petroli 
Kenya, Davis Chirchir (kulia) wakibadilishana Mkataba wa Makubaliano 
kuonesha dhamira ya Serikali ya nchi hizo kujenga miundombinu ya pamoja 
ya kusafirisha umeme na kufanya biashara ya kuuziana umeme wa ziada 
baina ya nchi hizo mara baada ya kusaini.
Mawaziri
 wa wanaoshughulikia Nishati kutoka nchi za Zambia, Tanzania na Kenya , 
Waziri wa Wizara ya Migodi, Nishati na Maendeleo ya Maji wa Zambia , 
Christopher Yaruma (kushoto) Waziri wa Nishati na Madini, Profesa 
Sospeter Muhongo Tanzania (katikati) na Waziri wa Nishati na Petroli 
Kenya, Davis Chirchir (kulia) wakionesha Mkataba wa Makubaliano mara 
baada ya kusaini.
Sehemu
 wa wadau walihudhuria hafla ya kusaini Mkataba wa Makubaliano kuonesha 
dhamira ya Serikali ya nchi za Zambia, Tanzania na Kenya kujenga 
miundombinu ya pamoja ya kusafirisha umeme na kufanya biashara ya 
kuuziana umeme wa ziada baina ya nchi hizo. Mbali na Wataalamu kutoka 
katika nchi hizo, hafla hiyo imehudhuriwa uwakilishi wa COMESA, 
Mashirika ya Umeme kutoka nchi hizo na baadhi ya washirika wa Maendeleo 
wakiwemo Benki ya Dunia, Umoja wa Ulaya, Ubalozi wa Norway, Shirika la 
Maendeleo la Japani (JICA), African Development Bank (AfDB), Ubalozi wa 
Ufaransa.  
Asteria Muhozya, Dar es Salaam 
Nchi za Zambia, Tanzania na Kenya zimesaini Mkataba wa Makubaliano 
kuonesha dhamira ya Serikali ya nchi hizo kujenga miundombinu ya pamoja 
ya kusafirisha umeme (ZTK) na kufanya biashara ya kuuziana umeme wa 
ziada baina ya nchi hizo na nchi nyingine barani Afrika. Akiongea katika
 hafla hiyo Waziri wa Nishati na Madini, Tanzania Profesa Sospeter 
Muhongo ameeleza kuwa, mradi huo wa pamoja unalenga kuondoa tatizo la 
upungufu wa nishati ya umeme baina ya nchi hizo na nchi nyingine barani 
Afrika jambo ambalo litachangia katika kukuza uchumi wa mataifa hayo. 
Naye, Waziri wa Migodi, Nishati na Maendeleo ya Maji wa Zambia , 
Christopher Yaruma ameeleza kuwa, utekelezaji wa mradi huo sio tu 
utaziwezesha nchi hizo kufanya biashara bali pia utafungua fursa za 
uwekezaji na kusaidia katika kuondoa umaskini miongoni mwa nchi 
wanachama kutokana kuzitumia fursa mbalimbali zinazotokana na nishati ya
 umeme. Kwa upande wake Waziri wa Nishati na Petroli Kenya, Davis 
Chirchir amewataka washirika wa maendeleo kusaidia katika kuwezesha 
utekelezaji wa mradi huo wa kujenga miundombinu ya pamoja ya kusafirisha
 umeme baina ya nchi hizo kutokana na manufaa yake kwa bara la Afrika na
 kuongeza kuwa, kutokana na uwepo wa rasilimali asilia za kutosha katika
 nchi hizo hakuna sababu ya kuwepo tatizo la nishati katika nchi hizo na
 barani Afrika. Naye, Katibu Mkuu Msaidizi wa Jumuiya ya Soko la pamoja 
la nchi za Mashariki na Kusini mwa Afrika anayeshughulikia miradi 
(COMESA), Dkt. Kipyego Cheluget amezipongeza nchi hizo kwa kuuendeleza 
utekelezaji wa mradi huo ambao umechukua kipindi kirefu na kuueleza 
kuwa, ni miongoni mwa miradi 16 ya kipaumbele na kimaendeleo kwa Afrika.
 Aidha, kwa upande wao Washirika wa maendeleo waliohudhuria hafla hiyo, 
wameonesha kufurahishwa kwao na dhamira ya nchi hizo na kuahidi 
kushirikana na nchi hizo kuhakikisha mradi huo unatekelezwa. Miongoni 
mwa washirika wa maendeleo waliohudhuria ni pamoja na uwakilishi wa 
Umoja wa Ulaya, Benki ya Dunia, Ubalozi wa Norway, Shirika la Maendeleo 
la Japani (JICA), African Development Bank(AfDB) na Ubalozi wa Ufaransa.
No comments:
Post a Comment