TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Saturday, December 28, 2013

ASASI YA “NEW LIFE IN CHRIST” YAKABIDHI MISAADA MBALIMBALI YA KIBINADAMU KWA WAFUNGWA WALIOPO MAGEREZANI LEO MKOANI KILIMANJARO

1 Mkurugenzi wa Doricas Aide International – Tawi la Tanzania, Bi. Stella Sozigwa(kushoto) akikabidhi Misaada ya Kibinadamu ya Wafungwa Waliopo Magerezani kwa Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini, John Casmir Minja. Hafla fupi ya Makabidhiano ya Misaada hiyo imefanyika leo Desemba 27, 2013 katika Viwanja vya Gereza Kuu Karanga – Moshi, Mkoani Kilimanjaro.2 Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini, John Casmir Minja akitoa hotuba fupi wakati wa hafla ya kupokea Misaada ya Kibinadamu kwa Wafungwa waliopo Magerezani iliyotolewa na Asasi ya “New Life In Christ” leo Desemba 27, 2013 katika Viwanja vya Gereza Kuu Karanga – Moshi, Mkoani Kilimanjaro.3  
Baadhi ya Askari wa Jeshi la Magereza wa Gereza Kuu Karanga – Moshi wakisikiliza hotuba ya Mgeni rasmi Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini, John Casmir Minja(hayupo pichani) wakati wa Makabidhiano ya Misaada ya Kibinadamu ya Wafungwa waliopo Magerezani iliyotolewa na Asasi ya “New life In Christ”.4  
Aina mbalimbali ya Misaada ya Kibinadamu iliyotolewa kwa Wafungwa waliopo Magerezani na Asasi ya “New Life In Christ”. Hafla ya Makabidhiano ya Misaada hiyo imefanyika leo Desemba 27, 2013 katika Viwanja vya Gereza Kuu Karanga, Moshi ambapo Mgeni rasmi alikuwa ni Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini, John Casmir Minja.5 
Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini, John Casmir Minja(katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi Wawakilishi wa Asasi ya “New Life In Christ” mara baada ya kupokea Misaada ya Kibinadamu ya Wafungwa waliopo Magerezani (wa tatu kulia) ni Mwenyekiti wa New Life In Christ Mkoani Kilimanjaro, Bi. Elly Makyao(wa pili kushoto) ni Mkurugenzi wa Doricas Aide International – Tawi la Tanzania, Bi. Stella Sozigwa(wa tatu kushoto) ni Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Magereza, Dkt. Juma Malewa( wa pili kulia) ni Mkuu wa Magereza Mkoani Kilimanjaro, Kamishna Mwandamizi Msaidizi wa Magereza, Hamis Nkubasi na wa kwanza kulia ni Mratibu wa Huduma za Magereza toka Asasi ya “New Life In Christ”, Bw. Charles Shang’aa(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).

No comments:

Post a Comment